Nawezaje kuacha uraibu wa kubeti (Betting)?

[emoji2][emoji2] huku kuna njia ya kuingia tu kutoka nooo..

Ila betting usiichukulie kama njia ya kujipatia mapato ODDS mbili zinakutosha, ukiona shetani la kununua Bugatti kwa hela ya muindi linakujia kazi ndio ipo hapa WEWE vs WEWE
 
Mpaka umeleta humu, ni njia ya kuelekea kuacha.

Betting inapoteza hela sana.
Kikubwa pia nakushauri "Uache kuangalia live score na kufatilia ratiba za mpira" yaani kama una App ya mipira, ifute...usijue fulani anacheza lini na nani.Itakusaidia.

Maana ukiingia tu livescore ama App ya kubeti, lazima utamani kubeti.
 
Embu acheni utani jamani, hv unaachaje kubet kwa mfano, kuna mambo mengi tunayafanya na sio ya muhimu yanamaliza pesa lkn hayajadili harafu mnajadili kuacha kubet?

Hivi boys anayenunua Malaya kwa elfu50 mpaka laki na upuuzi na wengine mpaka milioni na mm ninaye bet nani ana afadhali

Embu tazama sport pesa zigo lishafika bilioni kadhaa na upuuzi Fulani ukiliotea mbona kanisani unaitwa mzee wa kanisa hata kama uko under 18

Usiache kubeti mwana, kamua mpaka tumtie hasara kanjibayi
 

Soma vzr nilichoandika mkuu, nimesema kama unapata faida ni ww na sikukatazi kuendelea kubet, nachohitaji ni ushauri wa mm na wengine tunaohitaji kutoka namna gani tunaweza kutoka kwenye huu mchezo
 

Shukrani sana, hii nitaifanyia kazi
 
Hata Mimi tatizo Hili limenikumba sana naomba msaada Sanaa mnisaidie maaana mm hapa... Nilikua na mtaji wa milioni 3 yaan M3 nilipo Anza kubeti tu hivii nikala lakin Moja Kwa buku nikasema kumbe huku Kuna faida ya haraka hivii kumbe?

Basi nikaenderea kubeti nikawa nashawushika kubeti Kwa Hela kubwa maana mimi mwanzo kiwango changu cha juu kubeti ni 2000 lakin ilifika hatua nikawa na Beti kwa laki Moja daaaah 😭😭😭 basi Kuna siku Moja nikasema niweke laki Moja nipate lakin mbili Kwa odds 2 lakini chaajabu nililiwa aiseee 😭 kesho yake nilikua na laki 2 mbili nikasema nitafute odds 1.50 niweke nirudishe laki Moja yanguu chaajabu nayo pia ikaliwa πŸ˜­πŸ™„ hiyo siku naliwa laki mbili sikulala usiku maana ndo mala yangu ya kwanza kuliwa Hela ndefu kiasi hicho kweli nilitamani nijinyonge Ili maumivu nisiya sikie ya kupotelewa na Hela kubwa kiasi hicho ..... Basi mtaji wangu ukawa unashuka2 mpaka ukafika milioni Moja daah maisha yakaaanza kuharibika kwangu Yani Kwa siku nilikua na natumia 10k kubet kila siku na naliwa lakin nasema niweke tena niludishe Hela yangu lakin yakawa Yale yale2......

Kuna siku nikamfta dokita alikua rafiki yangu nikamweleza kuhusu kubeti vyote nika nikamwomba ushauri njia gani ya kutumia niache kubeti.

(1)....Moja akaniambia nayeye alikua anabeti pindi anasoma lakin ilimchukua mda sana kuacha kubeti
(A)...akaniambia futa zote app zako.
(B)....pili uza simu Yako kubwa yaan smartphone.
(C)...Tatu laini zako zote tupa ambazo ulikua unatumia kubeti usajiri ingine usiwe unaletewa matangazo ya kubeti sajiri lain ingine nunua simu ndogo yaana kiswaswadu.

Kweli alinishauli vitu vingi sana siwez kuvisema vyote hapa...

Kweli mm kwenye kubeti yangu Hela ya kula kubwa ilikua laki 3 do Hela kubwa kwangu lakini Hela niliyo poteza kalibia M2 nimepoteza hiyo Hela mm bila kujua...

Kweli nilifanikiwa kufuta app zote nikauza simu kwenye laini hapo siku tupa nikawa nachukuua namba za makampuni ya kubeti nawapiga nawaambia naomba hiii namba muifungie daima milele isije ikabeti maishani mwote.... Kwel nilifanikiwa kufanya hivo nikanunua simu ndogo simu ndogo nikakaanayo miezi 6 bila simu kubwa.... Ndo kitu ambacho nilifanikiwa kuacha kubeti mawazo yote yakatiweka Kabsa kuhusu kubeti kufatilia mipira nikaacha labda za kibongo2........




Mtaji wangu uliludi nikawa powa SAIVI sijui kubeti aiseee πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ .


Ahsanteni sana πŸ™πŸ™πŸ™πŸ™
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…