Nawezaje kuachana na mwenza wa miaka mingi tuliyezaa watoto 5 pamoja?

Andiko Lako FUPI,SAFI na LINAELEWEKA.Msalimie DINGI.Mwambie Asante kwa Kunileta Duniani.
 
Hii imenikumbusha stori ya wiki iliyopita.

Kuna kituo huwa napata usafiri wa umma. Sasa ikatokea kama mratatu nakutana na Kijana yuko na mzee wake anayeumwa ana kidonda kiunoni karibu na takoni cha asukari.

Baada ya kukutana mara kwa mara tukaanza kuzoeana.

Nikamuuliza vipi hii hali ya mzee mbona inazidi kudhoofu na ninakuona una hangaika naye peke yako huna dugu zako wengine??
Daah aisee kama nimechokoza nyuki, yule kijana alikuwa na mengi kichwani ila hana wa kusimulia.

Kwa kifupi tu alisema yule Mzee Baba yake alikuwa mtu wa kitengo, akawazaa wako 6. Then akaoa mtoto mbichi akawatelekeza wao na mama yao.
sasa mzee ameshastafu pesa tena hakuna na ana Kisukari na vidonda ndugu.

Watoto wa bibi mdogo ni watoto bado wanajitafuta, watoto wa bibi Mkubwa wote hakun anayejali wanamlipiza kisasi baba Yao sasa huyo anayempeleka hosp ni Kijan wa Mwisho ndio kajitolea ila kashachoka hela hakuna na hosp usafiri wa kila siku hakuna pia.

Na vile vidonda anasema havioneshi matumaini kama vinapona leo wala kesho.

Mzee aliharibu Future yake mwenyewe kwa kujifanya kitombi na starehe.
 
Nilichojifunza,Kwenye Maisha Majuto hayaepukiki.Ukiwalea vizuri ukawajali sana wanaweza kuwa mabumunda Ukasema BORA Ningezaa wengi zaidi.Na Ukiwa mtu wa mengi naye majuto yamo mule mule.Cha Muhimu ni kufahamu kwamba Mzazi ana maisha yake na Mtoto ana maisha yake na wote ni Viumbe kamili waliokamilika SO maamuzi tunayofanya kuna wakati yanakuwa sahihi ila hayakosi kasoro na Majuto
 
Hii imenikumbusha stori ya wiki iliyopita.

Kuna kituo huwa napata usafiri wa umma. Sasa ikatokea kama mratatu nakutana na Kijana yuko na mzee wake anayeumwa ana kidonda kiunoni karibu na takoni cha asukari.

Baada ya kukutana mara kwa mara tukaanza kuzoeana.

Nikamuuliza vipi hii hali ya mzee mbona inazidi kudhoofu na ninakuona una hangaika naye peke yako huna dugu zako wengine??
Daah aisee kama nimechokoza nyuki, yule kijana alikuwa na mengi kichwani ila hana wa kusimulia.

Kwa kifupi tu alisema yule Mzee Baba yake alikuwa mtu wa kitengo, akawazaa wako 6. Then akaoa mtoto mbichi akawatelekeza wao na mama yao.
sasa mzee ameshastafu pesa tena hakuna na ana Kisukari na vidonda ndugu.

Watoto wa bibi mdogo ni watoto bado wanajitafuta, watoto wa bibi Mkubwa wote hakun anayejali wanamlipiza kisasi baba Yao sasa huyo anayempeleka hosp ni Kijan wa Mwisho ndio kajitolea ila kashachoka hela hakuna na hosp usafiri wa kila siku hakuna pia.

Na vile vidonda anasema havioneshi matumaini kama vinapona leo wala kesho.

Mzee aliharibu Future yake mwenyewe kwa kujifanya kitombi na starehe.
 
Hizi Comments hizi zinafanya Watu tutafakari ule wimbo wa Wanaume "Tumeumbwa Mateso"
 
Kweli inasikitisha.
 
Nimemuonea huruma maana hapa mnampa kisago cha kisaikolojia...
Hatumpi kisago wala nini...ila kiukweli ameacha au na kutengezza makovu ya kudumu katika mioyo yetu watoto wake kwa kitendo chake kile cha kutukimbia...

Ni yeye tu anakumbuka ule msemo wa mbegu ya haladari kwenye mafundisho ya biblia. Dingi alikuwa mseminari haswa ila kuna kisa kimoja kilimponza huko na akaachana kabisa na habari za kanisani. Hata Hata mimi niklikuwa mseminari sana, ila nikaambiwa utakuja kuwa kama baba yako, na nikapigwa chini kuendelea na habari za upadri. ni stori ndefu sana ndugu yangu, nimeadhibiwa sana kwa makosa ya mzee wangu na hili la kuadhibiwa haya yeye analijua. siwezi sema haya mambo humu maana yapo deep sana na ni ya familia.

Nili comment tu kumpa onyo mtoa mada kama yupo tayari watoto wake waadhibike au waadhibiwe kwa makosa ya wazazi wao... mimi ni living proof wa hili ambo.

Mama alikuwa hohehahe- primary school teach watoto 11 na akastaafu kwa lazima ya ugonjwa mwaka 1985 mimi nikiwa na miaka 9. Nikaanza la kwanza nikiwa 11 yrs kwa sababu mama hakumudu elfu 7 ya wakti huo, ingawaje wakati mwingine serikali muda huo ilikuwa inatupa madaftari bure huko primary school.
Baba akakimbia familia- -ugonjwa wa mama na hali ngumu ya Maisha- kufyatua wengi kunahusika.
watoto tukaishi kama kuku wa kienyeji- free range hadi tumetoboa sote na maisha ni safi.
baada ya kuona tumetoboa ndio sasa mzee anarudi kuomba msamaha- ni mtihani mkubwa sana.

Ilifika mahala sisi watoto tukawa tunajadiri namna ya kunywa sumu tuondokane na mateso ya dunia.
chakula kilikuwa taabu sana- chai ya rangi iliyotengezwa kwa mtama ilikuwa ya kugombania
wali ulikuwa unapikwa xmas pekee bila maharagwe au nyama na kwa jinsi tulivyo kuwa wengi ilikuwa ni sagura sagura ya uhakika, tonge moja tu na unaridhika.

haya mambo yasikie tu kwa wengine ndugu yangu. Niki- reflect nilipotokea, nilipo na ninapo jwenda , nazidi kumtukuza Mungu Muumba, maana alinipitisha katika yote na bila yeye, sijui kama ningekuwa hapa kuandika habari hizi. Nahisi hata unyonge kufikiria tu nilipo toka, ila kwa sasa, Namshukuru Mungu sana, na hawajahi kunitupa kwa kweli katika shida zangu zote - achana na habari hizi za dingi. Mungu yupo na ni wa kweli. Nimemuona katika maisha yangu ya utotoni, ujanani na sasa uzeeni nikikaribia kustaafu kazi.

Ni hayo. Pokea litakalo kufaa.
 
Amejisaga mwenyewe mbona matunzo wanampa
Na tunampa matunzo ya maana sio hizi habari za laki moja kwa week. Ni zaidi ya Mil 2.5 kwa mwezi na yuko kijijini. Kawekewa hata na mfanya kazi wa ndani. Ni yeye tu akituona tunavyo mtendea wema aanza kulia kwa kukumbuka makosa yake ya ujanani... fainali uzeeni kwa kweli.
 
'Watatuonaje?' Amani ya mioyo yetu kwanza....vingine vipo tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…