Hii issue Vodacom hawajaiboresha. Kadi yao inadumu kwa mwezi mzima nqdhani. Ikiisha muda wake ukarenew account hauwezi kufanya tena malipo, linabaki jina tu. Nina line mbili zote nimejiunga na mpesa MasterCard ila zilishagoma kufanya malipo ninazo kama pambo tu. Wakati nafungua kwamara ya kwanza zilifanya kazi vzri tu ila baada ya kuisha muda wake na kuzisasisha , mpaka leo ni karibu mwaka sipati huduma PayPal, ukilipia unaambiwa blabla nyingi. Ubaya customer care wao wanajiona wameyapatia maisha, kiasi kwamba ukipiga unaambiwa tembelea duka la Vodacom 😠😠 fikiria uko km za kutosha toka walipo, ulipe usafiri kwenda kurekebishiwa line tu na pengine ukifika wanakupiga kiswahili. Kama una account crdb nenda activate online payment tu mkuu, voda wazinguaji tu