Complicator
JF-Expert Member
- Aug 23, 2013
- 2,198
- 3,580
Poleni na shughuli za utafutaji wajasiriamali.
Mimi ni kijana mjasiriamali,kwa sasa natengeneza sabuni za maji na pia Niko mbioni kutengeneza za vipande na kisha mafuta ya ngozi na nywele.
Ninapenda sana uzalishaji wa bidhaa na biashara yake,lakini tangu nimeanza kuna changamoto kadhaa ninazipata kiasi cha kuja hapa kuomba ushauri.
1.Upatikanaji wa Malighafi na Gharama zake.
Hii ni moja kati ya changamoto za msingi sana
Kwa hapa Mbeya tunategemea maduka mawili au matatu tu kwa ajili ya kununua malighafi za kutengeneza bidhaa tajwa.
Hali hii ya uchache wa maduka haya imepelekea malighafi hizi kuuzwa bei juu sana na bei zake kutokua na consistency, kila siku zinaongezwa bei bila utaratibu.
Hii inafanya nifikiri pia kuswitch kutoka biashara yangu na kufanya hii ya malighafi,lakini kama kuna mtu anafikiri anaweza ungana na Mimi kufanya hii tuwasiliane tuunganishe nguvu.
Pia naomba kwa mwenye kujua chimbo la bidhaa hizi ni lipi kwa huko DSM...Ili siku moja niwe nazifata mwenyewe,hii itasaidia sana kupunguza gharama za uzalishaji.
3. Uhakika na Muendelezo kwenye masoko.
Changamoto nyingine ni hii,kiuhalisia bidhaa hizi zina wateja lakini shida ni namna ya kua na soko la uhakika kiasi cha kuweza kuingiza fedha Mara kwa Mara,kwa sasa unaweza kuuza Lita 20 kila baada ya wiki mbili au tatu,hii si nzuri kibiashara.
Hapa pia naomba kwa mwenye kuweza kuniunga mkono anunue bidhaa zangu kwani nazitengeneza kwa uaminifu mkubwa tofauti kabisa na bidhaa zingine sokoni.
3. Kupata uhalali wa kuuza bidhaa hizi.
Hapa nazungumzia kupata vibali toka SIDO,TFDA NA TRA na kisha kuwa huru na halali kufanya biashara hii ambayo inahusisha afya za watu.
Kwa mwenye kujua utaratibu wa kupata vibali hivi anisaidie.
Nawasilisha.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi ni kijana mjasiriamali,kwa sasa natengeneza sabuni za maji na pia Niko mbioni kutengeneza za vipande na kisha mafuta ya ngozi na nywele.
Ninapenda sana uzalishaji wa bidhaa na biashara yake,lakini tangu nimeanza kuna changamoto kadhaa ninazipata kiasi cha kuja hapa kuomba ushauri.
1.Upatikanaji wa Malighafi na Gharama zake.
Hii ni moja kati ya changamoto za msingi sana
Kwa hapa Mbeya tunategemea maduka mawili au matatu tu kwa ajili ya kununua malighafi za kutengeneza bidhaa tajwa.
Hali hii ya uchache wa maduka haya imepelekea malighafi hizi kuuzwa bei juu sana na bei zake kutokua na consistency, kila siku zinaongezwa bei bila utaratibu.
Hii inafanya nifikiri pia kuswitch kutoka biashara yangu na kufanya hii ya malighafi,lakini kama kuna mtu anafikiri anaweza ungana na Mimi kufanya hii tuwasiliane tuunganishe nguvu.
Pia naomba kwa mwenye kujua chimbo la bidhaa hizi ni lipi kwa huko DSM...Ili siku moja niwe nazifata mwenyewe,hii itasaidia sana kupunguza gharama za uzalishaji.
3. Uhakika na Muendelezo kwenye masoko.
Changamoto nyingine ni hii,kiuhalisia bidhaa hizi zina wateja lakini shida ni namna ya kua na soko la uhakika kiasi cha kuweza kuingiza fedha Mara kwa Mara,kwa sasa unaweza kuuza Lita 20 kila baada ya wiki mbili au tatu,hii si nzuri kibiashara.
Hapa pia naomba kwa mwenye kuweza kuniunga mkono anunue bidhaa zangu kwani nazitengeneza kwa uaminifu mkubwa tofauti kabisa na bidhaa zingine sokoni.
3. Kupata uhalali wa kuuza bidhaa hizi.
Hapa nazungumzia kupata vibali toka SIDO,TFDA NA TRA na kisha kuwa huru na halali kufanya biashara hii ambayo inahusisha afya za watu.
Kwa mwenye kujua utaratibu wa kupata vibali hivi anisaidie.
Nawasilisha.
Sent using Jamii Forums mobile app