Nawezaje Nunua Hisa za Jamiiforums

Mchambuzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2007
Posts
4,850
Reaction score
9,434
Ja hakuna mpango wa kupeleka mafanikio ya mtandao huu kwa umma kupitia kuuza hisa kadhaa na sisi wengine proudly tupate nafasi kuwa sehemu ya JF?
 
Anza kwa kuchangia kwanza uendeshaji wake,mkuu hata elfu tano tu umeshindwa hisa ndo utaweza?
Au umetumwa na wakuu wa magamba ili muitafishe?
Tunatosha tulio na hisa,wata kao ongezeka zaidi ni virusi na spys,...we don't need them!
Changia JF,mkono mtupu haulambwi
 
Vipi ya 'JF' ya kwenu haijaanzwa kurushwa hewani?!
 
Vua kwanza hilo shati la kijani halafu ukimaliza ndo utafikiriwa vinginevyo jf ni maintelijensi kuliko unavyofikiria.
 
Haya bwana, ilikuwa ni swali tu. Basi hata njia za kusaidia elfu mbili ,elfu tano uwekwe wazi, nina hakika wenye kujua umuhimu wa JF wapo wengi na watasaidia, mimi nikiwa mmoja wapo. Vinginevyo kama mmetosha, haina shida. Na kuhusu JF yetu, una maana ya CCM? Mimi sina taarifa yoyote, mimi ni mwanachama tu niliejaribu gombea ubunge, ikaishia hapo. Na Chadema wenye hali kama yangu najua mpo wengi humu - mnakipenda chama au ni wana chama lakini hamtatendewa haki mkiulizwa mtoe maelezo ya yanayotokea kwenye chama chenu unless muwe na nafasi ya uongozi.
 
Hivi RA ndio alinunua Habari Corporation?

Na wewe ni nani unataka kuinunua JF?
 
hapa patamu..... na hoja nzuri but again kwa nini umeweka hii thread kwenye siasa? is this politics au unataka majibu ya kisiasa.?

Anyway naelewa sababu watu wengi tuko kisiasa zaidi so usishangae hata majibu ya wachangaji wengi yakawa ya kisiasa.



Naomba kutofautiana na wewe kuchangia sio lazima kuchangia kwa mshiko tu yaani hard money. Sasa tukitaka michango ya mshiko tu tusimshange Jk anayezunguka nchi mbali mbali kuomba misaaasa ya fedha.

Nimewai kutoa wazo fulani kwa jf management crew ambalo naamini wangelifanyia kazi ulikuwa ni mchango tosha kwao na kwa taifa. But again msisitizo wao zaidi uko kwenye mkono mtupu haulambwi. So to them ni bora nichangie 20,000 Tsh kuliko wazo amablo wagefanyia kazi may be thamani ya faida yake ni mamilioni ........... sio tu kwa jf but kwa taifa

Tuendelee kukubali kutofautiana kwa hoja.
 

Boss kuna link pale juu umepewa ya jinsi ya kuchangia JF,
itakua vyema sana,ila usitoe hela nyingi sana mwisho wa siku uanze kudai
habari za ccm kuandikwa kwa lazima because umetoa hela nyingi,...

bofya hapa:
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/22767-changia-jf-mkono-mtupu-haulambwi.html
 


Yeye inaonesha ana itaka JF kwa manufaa ya kisiasa zaidi,...
hiyo inatupa mtazamo kwamba ndo mwendelezo wa Mukama kutaka "waidhibiti" JF,..
Angekua yupo kibiashara zaidi,toka 2007 yeye ni mwana JF anawajua moderators humu ange waPM,or kama hawajui basi kuna jukwaa la uchumi na biashara,...
duh,umenoa mkuu
 
Achana na wanaoleta habari za CHADEMA au CCM hapa.

Kwa taarifa yako, mmoja wa OWNER(mie huwaita wadhamini) wa JF ni William Malecela ambaye ni member wa CCM waziwazi......

Kama utataka kununua kipande cha JF, ningelipendekeza uwasiliane na Max Mello au W. Malecela, Steven Diallo, na wengine ambao kama upo Dar, sidhani kama ni shida sana kuwapata hao wadhamini wa JF.

Vinginevyo kuja hapa JF na kumwaga hilo swali, unataka tu wakushambulie na mambo ya CCM Vs Chadema.

Haya mambo sidhani kama huwa yanaongelewa BARAZANI. Mnaongelea ndani na mwishoni inatoka tu habari kuwa Mwana CCM mwingine amenunua hisa za Jamiiforums.
 
JF kuweni makini na watu wanaotaka kununua hisa wengi wao lengo lao si zuri, nadhani mtakuwa na kumbukumbu za waraka ulioitaja jf kuwa moja ya vizingiti kwa ccm, akili mkichwa
 


Changia kwanza ndo uhulize mambo ya hisa
 
Pole sana kwa yanayokukuta, Ila ukweli ni kwamba wengi wangatamani kuwa na hisa humu JF ila wahusika watakuja kukujibu naamini.

Michango inaweza kutumwa kwa njia kuu nne:

1. Kwa walio nje wanaweza kutumia PayPal au Credit Cards au Debit Cards kwa kufuata link hii ( https://www.jamiiforums.com/payments.php) iliyo kwenye sahihi yangu (linapoonyesha dole gumba) na pindi mchangiaji anapoweka chochote tunakuwa notified nasi tunafanya kuwasiliana na mhusika ili aweze kupandishwa kwenda katika group la Premium Members.

Paypal users:

Details will follow

2. Njia ya pili ni kutumia Western Union au Money Gram na kutuma kwenda kwa Maxence Melo Mubyazi wa Dar es Salaam.

3. Njia ya tatu ni kutumia Bank accounts za Maxence kama ifuatavyo:

NBC:

Acc #: 033201064359
Jina: Maxence Melo Mubyazi

CRDB:

Account Name: Maxence Melo Mubyazi
Bank: CRDB Pugu Road Branch
Swift Code: CORUTZTZ
Acc No: 01J2092391800

4. Njia ya nne:

Unaweza kutuma recharge vouchers za tiGO, Zain, VodaCom au Zantel au ZAP, M-PESA, tiGO PESA, Z-PESA n.k kwenda kwa Maxence - 0713444649 naye atakufahamisha kuwa kazipokea. Namba za ZAP, M-PESA na Z-PESA anaweza kukupa ukiwasiliana naye.

=================================

Ikumbukwe, SI LAZIMA kuandika jina lako la kweli na SI LAZIMA kwenda mwenyewe bank kutuma pesa hizo (kwani unaweza kumpa unayemwamini na kumpa account details na jina lako ambalo ungependa aandike).

Tunaweza kuandika mengi lakini ukweli unabakia pale kuwa JF inahitaji michango yenu kwa sana tu.

Kwa wenye maswali zaidi wanaweza kuwasiliana na Maxence kupitia namba yake ya simu +255713444649.
 
Hivi RA ndio alinunua Habari Corporation?

Na wewe ni nani unataka kuinunua JF?

Yeah,katika mchakato wa "kudhibiti" media ambazo inaonekana zinapendwa na vijana na
zina sababisha ccm kuto pendwa!
New habari ilikuaga na habari kweli kweli,
ilikua inauza kweli,ilikua inakubalika kweli kwa habari zake,...
Mh,ilivo ingia mikononi mwa gamba duh,....hata vichwa vyake vya habari havipendeki,...
JF management issingie kwenye mtego wa kujiua kuilaini,ni laana
 

Hayo yote ana yafahamu,haiwezekani asiwajue wanahisa wa JF toka 2007,hata kabla wewe huja jiunga na JF hadi leo,..
au ange wa PM mods wange mwambia cha kufanya,..
au angeenda jukwaa la uchumi na biashara,...huyu katumwa kivingine na kakosea njia!
Na sidhani kama anajua biashara kwa approach yake hii,.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…