Nayapenda sana maisha ya instagram

Nayapenda sana maisha ya instagram

four eyes

JF-Expert Member
Joined
Jan 11, 2017
Posts
905
Reaction score
1,408
Instagram, sio Facebook au JamiiForums, ni Instagram. Hapa ndipo ambapo kila umuonae yuko very smart kimavazi, pamba kali kali na simu za gharama zipo humo katika maisha ya Instagram.

Ni humo ndipo ambapo watu wanakula maisha kwelikweli, picha za kuthibitisha za viwanja vikali na misosi mizuri ya bei mbaya imo humo Instagram.

Hakuna mwenye shida insta jamani, kila mmoja ana kazi nzuri na anaishi pazuri na anamiliki gari tena sio mkweche bali gari zuri mno la kuvutia.

Ndio huko kwenye mabinti wazuri karibu wote, sura na figa nzuri nzuri kama za kuchora utazikuta huko, rangi za ngozi za kuvutia na ngozi laini zipo huko kwa wanaotaka wake.

Kwa wenye uchu wa mapenzi madalali wa mabinti poa wapo kibao humo wewe tu, mabinti wadangaji wapo kibao na picha zao za nusu uchi zimejaa humo wewe tu.

Familia za insta ni Familia bora za mfano, ni Familia za watanashati zenye furaha, mababa na mama wa Familia insta wanapendana mno mpaka wanavaa saresare na watoto wao baba king, mama queen, mtoto prince au princess.

Hakuna stress za magu katika maisha ya insta ni full Bata na mafanikio.kuna watu wa aina tofauti kule ni jukumu lako wewe kuamua unataka kumuiga nani, kuna wale wanaojivunia uvaaji wao, kuna wale wanaojivunia bata mbalimbali mfano kina tunda, kuna wanaojivunia uzuri wao mfano kina lulu na Masogange na wale wanaoonyesha mafanikio yao na jitihada zao mpaka wakafanikiwa mfano kina masanja mkandamizaji, ni jukumu lako kuamua umuige nani uwe kama yeye.

Insta hakuna umasikini kama Facebook, insta hakuna haja ya akili nyingi na maadili kama JamiiForums, kule ni utashati, uzuri, bata na utajiri.

Ningeambiwa nichague Dunia ya kuishi ningechagua insta. Nayapenda maisha ya insta hata misiba inahuzunikiwa with class and style, kuumwa watu wanaumwa kwa style and class wanalazwa Agha khan.

Nayapenda maisha ya Insta, ndoto ya kila kijana, vipi we mwenzangu?
 
Maisha ya JF kwa upande wangu ni mazuri mno kwa maana tunatumia akili na fikra pevu kuchambua hoja na mijadala mbalimbali

Maisha ya kupost picha kila saa na kuigiza siyawezi bora hapa JF naweza nikapata idea nzuri ya maisha kuliko uuzaji sura kule instagram
 
serikali ya china imewafanya wananchi yake wawe wachapakazi kwa kufungia website zote za kuuza sura..

ukiwa china huwez ingia instagram, facebook, youtube wa website yoyote ya ngono...

kule mawasiliano ni email na watsup tu kwa ajili ya kufanikisha business tu....

bongo muda wa kazi watu wanauza sura instagram tu... mtu anajiita king au queen huku hana hata buku mfukoni
 
serikali ya china imewafanya wananchi yake wawe wachapakazi kwa kufungia website zote za kuuza sura..

ukiwa china huwez ingia instagram, facebook, youtube wa website yoyote ya ngono...

kule mawasiliano ni email na watsup tu kwa ajili ya kufanikisha business tu....

bongo muda wa kazi watu wanauza sura instagram tu... mtu anajiita king au queen huku hana hata buku mfukoni
Hawa kina Jux ambao hua wanapost picha insta wakiwa China hua wanakua China ya gongo la mboto?

Naomba ufafanuzi kidogo…
 
serikali ya china imewafanya wananchi yake wawe wachapakazi kwa kufungia website zote za kuuza sura..

ukiwa china huwez ingia instagram, facebook, youtube wa website yoyote ya ngono...

kule mawasiliano ni email na watsup tu kwa ajili ya kufanikisha business tu....

bongo muda wa kazi watu wanauza sura instagram tu... mtu anajiita king au queen huku hana hata buku mfukoni
Jux yupo china, na amepost picha za graduation yake kwenye instagram... Hapo unasemaje??
Vipi kuhusu wakina Customer care(mdananda)... Deile wanapost mapicha ndani ya ghuangzhou
 
Maisha ya JF kwa upande wangu ni mazuri mno kwa maana tunatumia akili na fikra pevu kuchambua hoja na mijadala mbalimbali

Maisha ya kupost picha kila saa na kuigiza siyawezi bora hapa JF naweza nikapata idea nzuri ya maisha kuliko uuzaji sura kule instagram
Exactly Broo ndiyo maana na kulove....

Kwavile tumetoka tumbo mojaaaa[emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji8]
 
Maisha ya JF kwa upande wangu ni mazuri mno kwa maana tunatumia akili na fikra pevu kuchambua hoja na mijadala mbalimbali

Maisha ya kupost picha kila saa na kuigiza siyawezi bora hapa JF naweza nikapata idea nzuri ya maisha kuliko uuzaji sura kule instagram
Exactly Broo ndiyo maana na kulove....

Kwavile tumetoka tumbo mojaaaa[emoji7] [emoji7] [emoji7] [emoji8]
 
Back
Top Bottom