NBC imenipotezea malengo yangu

NBC imenipotezea malengo yangu

ngulyabhule

JF-Expert Member
Joined
Apr 5, 2020
Posts
226
Reaction score
377
Salaam moja kwa moja kwenye mada! Wiki mbili zilizopita nilipata bahati ya mzigo kwa bei rahisi! Basi nikawa na pesa nusu ya kuulipia na nusu iliyobaki nikaona nikope hii NBC! Na kumuahidi muuzaji ndani ya siku tano tu nitamalizia nikiwa na uhakika na hii bank hasa baada ya kuamini matangazo yao lakini mpaka leo ni siku ya 11 baada ya kukamilisha taratibu zoote! Jamaa karudisha pesa na kauza kwa mtu mwingine! Na nimeenda kusitisha mkopo wanadai process zote tayari kwenye mfumo ilihali pesa yao sijaingiziwa kiniumacho nia na lengo langu lishapotezwa ni hii BANK sasa hata hiyo pesa ikija dah!
 
NBC sikuizi sijui wana shida gani,.. Nina mwezi wa pili sasa tangu nimeandika barua kwa meneja ili nitoe hela kwenye MALENGO ACCOUNT,. Na hapo mda wa kutoa hela ushafika na kupitiliza,. Hadi jana kila nikienda wanasema mtandao unasumbua kutoa malengo,. Ni suala linalofikirisha mtandao kusumbua zaidi ya mwezi
 
NBC sikuizi sijui wana shida gani,.. Nina mwezi wa pili sasa tangu nimeandika barua kwa meneja ili itoe hela kwenye MALENGO ACCOUNT,. Hadi jana kila nikienda wanasema mtandao unasumbua kutoa malengo,. Ni suala linalofikirisha mtandao kusumbua zaidi ya mwezi
Na shida hawatoi taarifa kama wanajua mifumo yao shida wangetoa taarifa watu wafahamu. Pole sana muhanga mwenzangu
 
Salaam moja kwa moja kwenye mada! Wiki mbili zilizopita nilipata bahati ya mzigo kwa bei rahisi! Basi nikawa na pesa nusu ya kuulipia na nusu iliyobaki nikaona nikope hii NBC! Na kumuahidi muuzaji ndani ya siku tano tu nitamalizia nikiwa na uhakika na hii bank hasa baada ya kuamini matangazo yao lakini mpaka leo ni siku ya 11 baada ya kukamilisha taratibu zoote! Jamaa karudisha pesa na kauza kwa mtu mwingine! Na nimeenda kusitisha mkopo wanadai process zote tayari kwenye mfumo ilihali pesa yao sijaingiziwa kiniumacho nia na lengo langu lishapotezwa ni hii BANK sasa hata hiyo pesa ikija dah!
Hata sijui mnaipendea nini hiyo bank. Kamwone Branch Manager, atasitisha mkopo. Next time kwenye hizo bank uwe unaongea na wanaoweza kufanya maamuzi.

Ova
 
Na shida hawatoi taarifa kama wanajua mifumo yao shida wangetoa taarifa watu wafahamu. Pole sana muhanga mwenzangu
Wanakera sana aisee,. Bora hata wangekua wanatoa taarifa lakini walivyo wapuuzi kila siku wanakwambia njoo kesho uonane na mtu fulani,. Mara kesho hayupo njoo wiki ijayo,.
Yaani hiyo ni malengo Account tu,. Asa sijui wenye Fixed accounts wanapataje shida
 
Nijuavyo, kwenye bank njia rahisi ya kudeal na jambo kama hili ni kupitia kwa Branch Manager. Kusitisha mkopo ambao umechelewa ni haki yake.

Ova
Kwenye hilo suala la mkopo sifahamu kwasabu sijawahi kukopa,.

Lakini na kutoa hela nako kwenye Malengo accounts naona kama utaratibu wao uko complicated sana kuliko bank nyingine kama NMB ukienda unajaza tu ile fomu unasign wanagonga muhuri na kitambulisho unatoa,. Tena wanakufanyia palepale tu wale watu wa Customer services haina hata haja ya kuandika barua kwa meneja sijui nini

Wanakoelekea NBC watapoteza wateja,
 
Local banks zina mambo ya kijinga sana, mi toka kadi ya NMB iishe muda wake, alafu wao wakatengeneza kimya kimya wakaituma Mbeya niliwaona wapuuzi sana.
Nawaambia naitaka wailete dsm, wao wanadai nilipie 20k! Nilitoa hela yote dirishani na mpaka leo sijarudi tena!
 
Kwenye hilo suala la mkopo sifahamu kwasabu sijawahi kukopa,.

Lakini na kutoa hela nako kwenye Malengo accounts naona kama utaratibu wao uko complicated sana kuliko bank nyingine kama NMB ukienda unajaza tu ile fomu unasign wanagonga muhuri na kitambulisho unatoa,. Tena wanakufanyia palepale tu wale watu wa Customer services haina hata haja ya kuandika barua kwa meneja sijui nini

Wanakoelekea watapoteza NBC watapoteza wateja,
NBC wenye nayo hawako hapo Tanzania.

Ova
 
NBC sikuizi sijui wana shida gani,.. Nina mwezi wa pili sasa tangu nimeandika barua kwa meneja ili nitoe hela kwenye MALENGO ACCOUNT,. Na hapo mda wa kutoa hela ushafika na kupitiliza,. Hadi jana kila nikienda wanasema mtandao unasumbua kutoa malengo,. Ni suala linalofikirisha mtandao kusumbua zaidi ya mwezi
Mmh labda unataka kufunga account..malengo mbona unachukua ndani ya dakika kumi tu kama unabakisha hata 10k tu?
 
Mmh labda unataka kufunga account..malengo mbona unachukua ndani ya dakika kumi tu kama unabakisha hata 10k tu?
Ndio hicho kitu hata mimi nawashangaa,. Kwanini wananizungusha au mtandao wao iweje unasumbua zaidi ya mwezi kutoa malengo na shughuli nyingine zinafanyika kupitia system hiyohiyo,. Like how??🤔
 
Salaam moja kwa moja kwenye mada! Wiki mbili zilizopita nilipata bahati ya mzigo kwa bei rahisi! Basi nikawa na pesa nusu ya kuulipia na nusu iliyobaki nikaona nikope hii NBC! Na kumuahidi muuzaji ndani ya siku tano tu nitamalizia nikiwa na uhakika na hii bank hasa baada ya kuamini matangazo yao lakini mpaka leo ni siku ya 11 baada ya kukamilisha taratibu zoote! Jamaa karudisha pesa na kauza kwa mtu mwingine! Na nimeenda kusitisha mkopo wanadai process zote tayari kwenye mfumo ilihali pesa yao sijaingiziwa kiniumacho nia na lengo langu lishapotezwa ni hii BANK sasa hata hiyo pesa ikija dah!
Mkuu,Kwanza unapaswa kuelewa kwamba Benki haijaharibu Malengo yako bali ni wewe ulikuwa ujajipanga.Kama wewe ni Mfanya biashara unatakiwa uhakikisha kwamba Umeshakamilisha michakato ya kibenki kabla ya kupanga matumizi ya Pesa zao.Cha Muhimu sasa kama huo mkopo wa Casha huhitaji na umekamilisha taratibu zote waambie waugeuze uwe Standby Credit Facility Ila isiwe Overdraft usije itumie kunywea Bia.
 
Back
Top Bottom