Pre GE2025 NCCR Mageuzi wasema hawapo tayari kuunganisha nguvu na chama chochote cha upinzani

Pre GE2025 NCCR Mageuzi wasema hawapo tayari kuunganisha nguvu na chama chochote cha upinzani

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

the guardian 17

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2024
Posts
395
Reaction score
570
Wakuu NCCR nao nao wanadai hawapo kuunganisha nguvu na chama chochote cha upinzani, wanasahau kidole kimoja hakivunji chawa

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
=====

Chama cha NCCR-Mageuzi kimesema hakitajiunga na chama chochote cha upinzani kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Mwenyekiti wa chama hicho, Ambar Khamis, ametoa kauli hiyo leo, Februari 18, 2025, katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo Ilala, jijini Dar es Salaam.

"Sisi NCCR tutakuwa peke yetu, hatutakuwa na muungano na vyama vingine kutokana na madhara tuliyoyapata mwaka 2015 baada ya kujiunga na UKAWA. Tulipata wabunge wanne katika majimbo mbalimbali, lakini tukabaki na mbunge mmoja pekee, hali iliyotufanya kupoteza majimbo yetu," alisema Khamis.

Ameongeza kuwa kulikuwepo na makubaliano ndani ya muungano huo, lakini baadhi ya vyama wenza vilishindwa kuyatekeleza.

Aidha, Khamis amesema kuwa NCCR-Mageuzi tayari imeanza vikao vya Kamati Kuu kwa ajili ya maandalizi ya chaguzi za ndani ya chama.

"Vyama vingine kama ACT-Wazalendo, CAF, na CHADEMA vimeshafanya chaguzi zao, sasa ni zamu yetu," alisema.

Amebainisha kuwa chama hicho kinatarajia kufanya mkutano mkuu wa ngazi za kitaifa, mikoa, na wilaya mwezi Aprili mwaka huu, ndani ya kipindi cha mwezi mmoja.
 
Waunganishe nguvu zao wenyewe kwa wenyewe kwanza wapate chama, sasa hivi hawana hata chama cha maana
 
Wakuu NCCR nao nao wanadai hawapo kuunganisha nguvu na chama chochote cha upinzani, wanasahau kidole kimoja hakivunji chawa

=====

Chama cha NCCR-Mageuzi kimesema hakitajiunga na chama chochote cha upinzani kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Mwenyekiti wa chama hicho, Ambar Khamis, ametoa kauli hiyo leo, Februari 18, 2025, katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo Ilala, jijini Dar es Salaam.

"Sisi NCCR tutakuwa peke yetu, hatutakuwa na muungano na vyama vingine kutokana na madhara tuliyoyapata mwaka 2015 baada ya kujiunga na UKAWA. Tulipata wabunge wanne katika majimbo mbalimbali, lakini tukabaki na mbunge mmoja pekee, hali iliyotufanya kupoteza majimbo yetu," alisema Khamis.

Ameongeza kuwa kulikuwepo na makubaliano ndani ya muungano huo, lakini baadhi ya vyama wenza vilishindwa kuyatekeleza.

Aidha, Khamis amesema kuwa NCCR-Mageuzi tayari imeanza vikao vya Kamati Kuu kwa ajili ya maandalizi ya chaguzi za ndani ya chama.

"Vyama vingine kama ACT-Wazalendo, CAF, na CHADEMA vimeshafanya chaguzi zao, sasa ni zamu yetu," alisema.

Amebainisha kuwa chama hicho kinatarajia kufanya mkutano mkuu wa ngazi za kitaifa, mikoa, na wilaya mwezi Aprili mwaka huu, ndani ya kipindi cha mwezi mmoja.
View attachment 3240835
kibaka na tapeli wa siasa chadema ataku anajiskia vibaya sana akiona hii dah :pedroP:
 
Wakuu NCCR nao nao wanadai hawapo kuunganisha nguvu na chama chochote cha upinzani, wanasahau kidole kimoja hakivunji chawa

=====

Chama cha NCCR-Mageuzi kimesema hakitajiunga na chama chochote cha upinzani kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Mwenyekiti wa chama hicho, Ambar Khamis, ametoa kauli hiyo leo, Februari 18, 2025, katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo Ilala, jijini Dar es Salaam.

"Sisi NCCR tutakuwa peke yetu, hatutakuwa na muungano na vyama vingine kutokana na madhara tuliyoyapata mwaka 2015 baada ya kujiunga na UKAWA. Tulipata wabunge wanne katika majimbo mbalimbali, lakini tukabaki na mbunge mmoja pekee, hali iliyotufanya kupoteza majimbo yetu," alisema Khamis.

Ameongeza kuwa kulikuwepo na makubaliano ndani ya muungano huo, lakini baadhi ya vyama wenza vilishindwa kuyatekeleza.

Aidha, Khamis amesema kuwa NCCR-Mageuzi tayari imeanza vikao vya Kamati Kuu kwa ajili ya maandalizi ya chaguzi za ndani ya chama.

"Vyama vingine kama ACT-Wazalendo, CAF, na CHADEMA vimeshafanya chaguzi zao, sasa ni zamu yetu," alisema.

Amebainisha kuwa chama hicho kinatarajia kufanya mkutano mkuu wa ngazi za kitaifa, mikoa, na wilaya mwezi Aprili mwaka huu, ndani ya kipindi cha mwezi mmoja.
View attachment 3240835
unaunganishaje nguvu wakati huna
 
Chama cha NCCR Mageuzi kimesema hakitashirikiana na chama chochote cha siasa katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu kutokana na maumivu walioyapata uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 walipojiunga na ukawa.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa chama hicho Ambari Haji Hamisi wakati akizungumza na waandishi wa habari, kuelekea chaguzi za ndani za chama hicho na mkutano mkuu unaotarajiwa kufanyika Aprili mwaka huu.

Amesema kuwa, majereha walioyapata katika uchaguzi wa mwaka 2015 bado hayajapona, hivyo hawapotayari kushirikiana na chama chochote kutokana na kupoteza majimbo yao.

Amesema kuwa, mwaka 2015 walipounda umoja wa katiba ya wananchi UKAWA, kuna makubaliano ambayo walikaa kwa pamoja lakini kilichotokea ni maumivu kwa Chama cha NCCR Mageuzi.

"Tulikubaliana Kuna baadhi ya majimbo tutaachiana lakini kilichotokea kwetu ni maumivu, tulipojiunga tulikua na majimbo manne lakini tuliporidi tumerudi na Jimbo mmoja tu"amesema Ambari.

Amesema kuwa, katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu watasimama wao wenyewe bila kushirikiana na chama chochote.

"Hatuko kwenye vyama 14 wala sita wala vyama vitatu, sisi tuko peke yetu na tutaendelea kuwa peke yetu mpaka vikao halali vya chama vitakapoona vinginevyo...kwasasa umoja tulishauvunja Dodoma kwenye mkutano mkuu.

"Hatutaki umoja kwa sababu madhara yaliyotukuta 2015 ni makubwa mpaka leo hatujapona. Tuliingia kwenye uchaguzi tukiwa na wabunge wanne tukatoka na mbunge mmoja mengine tukapoteza...sisi hatukufaidika chochote kwenye Ukawa," amesema Khamis.

Mwenyekiti huyo amesema yako maadhimio ambayo walikubaliana na kusaini lakini vyama vingine havikuyatekeleza hivyo hawawezi kurudia makosa.

Aidha amesema kupitia mkutano mkuu utakaofanyika Aprili mwaka huu pia watatangaza jina la mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mgombea urais kwa upande wa Zanzibar pamoja na kupitisha mabadiliko ya katiba ya chama hicho.

Chama hicho kimesema kimejifunza kilipokosea na sasa kimejipanga kuhakikisha kinashiriki vizuri Uchaguzi Mkuu na kushinda kwa kishindo.
 
Chama chenyewe kiko hoi bin taabani halafu hakitaki kuunganisha nguvu. Bora CHADEMA wakatae kuliko NCCR Mageuzi iliyojichokea kama CUF
 
Wakuu NCCR nao nao wanadai hawapo kuunganisha nguvu na chama chochote cha upinzani, wanasahau kidole kimoja hakivunji chawa

=====

Chama cha NCCR-Mageuzi kimesema hakitajiunga na chama chochote cha upinzani kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Mwenyekiti wa chama hicho, Ambar Khamis, ametoa kauli hiyo leo, Februari 18, 2025, katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo Ilala, jijini Dar es Salaam.

"Sisi NCCR tutakuwa peke yetu, hatutakuwa na muungano na vyama vingine kutokana na madhara tuliyoyapata mwaka 2015 baada ya kujiunga na UKAWA. Tulipata wabunge wanne katika majimbo mbalimbali, lakini tukabaki na mbunge mmoja pekee, hali iliyotufanya kupoteza majimbo yetu," alisema Khamis.

Ameongeza kuwa kulikuwepo na makubaliano ndani ya muungano huo, lakini baadhi ya vyama wenza vilishindwa kuyatekeleza.

Aidha, Khamis amesema kuwa NCCR-Mageuzi tayari imeanza vikao vya Kamati Kuu kwa ajili ya maandalizi ya chaguzi za ndani ya chama.

"Vyama vingine kama ACT-Wazalendo, CAF, na CHADEMA vimeshafanya chaguzi zao, sasa ni zamu yetu," alisema.

Amebainisha kuwa chama hicho kinatarajia kufanya mkutano mkuu wa ngazi za kitaifa, mikoa, na wilaya mwezi Aprili mwaka huu, ndani ya kipindi cha mwezi mmoja.
View attachment 3240835
Nchi hii inavituko sana , sasa ichi nacho kipo na shida gani , yani vikiitwa vyama nacho ati kinatoka
 
Uongozi uliopo ni mamluki kwani waliwekwa kinyemela na Msajili wa vyama
 
Back
Top Bottom