Eleza ni kipi kimefanyika ambacho ni katika mipango ya kuifanya ccm wakae? Kipi kilichobadilika katika yale mambo yenye kutumika na ccm kuendelea kubaki madarakani?Mwaka 2020 upo kivingine CCM lazima wakae
Ni kweli kuwa CCM walifanya makosa sana kwa kutompeleka Magufuli kanda ya kusini; Jakaya, Majaliwa na Samia tu hawakuwa kete ya kutosha. Hiyo inaweza kuwa inawahakikishia CCM kukosa mikoa mitatu hasa kwa vile Nape ni mwana CCM ambaye yuko upande wa pili na haijulikani yeye anapiga kampeini za namna gani. Kwa hivyo Lindi, Mtwara na Ruvuma inaweza kuwa ni bye bye kwa CCM!!Mbaya zaidi ni huko kanda ya kusini. Serikali ya magufuli walipoona magufuli ameshindwa kufanya kampeni mikoa ya LINDI na Mtwara wakaamua Jana kumzuia Lissu kufanya mikutano kama nane kwenye mikoa hiyo. Kilichonishangaza ni kuwa wananchi wameapa kwa Jina la Allah kuwa vyovyote vile watampigia kura Tundu Antiphas Lissu na watazilinda kura zao hapo wiki ijayo.
Kweli wakati wa Mungu alishafika, hakuna wa kuuzuia!!
Angefanya kazi yake pasipo kututeka, kutupoteza, kututungia sheria kandamizi,... . ......... ingekuwa vyema. Lakini sasa....Magufuli anafanya kazi kubwa wewe umekaa tu. Muda wote upo unabonyeza simu.
Hapa jf mnaonekana kushupaza shingo Sana,Ila huko mtaani ni CCM tupu.Kafanye utafiti mtaani,sio hapa jf.
Huree! Freedom in offing.Chagua Kiongozi atakayetupatia
HAKI
UHURU
Na
MAENDELEO YA WATU
Siyo Mwingine zaidi ya Tundu Lissu
Endelea kujifurahisha na kuwadanganya wabeba mabox wa Ulaya na USA!Zikiwa zimebaki siku 3 kabla hatujaingia tarehe 28.10.2020 siku ya kufanyika kwa uchaguzi Mkuu Tanzania, nadiriki kusema kuwa nchi naona inamtaka Lisu. Nimezunguka Mikoa 25 ya Bara na 3 ya Zanzibar, nimepita kila pembe ya nchi. Nimezunguka vijijini sana na kila kona ya nchi hii kwa shughuli za kikazi katika NGO aiseeee sijui nini kitokee ila nimeshuhudia kwa macho yangu na kuona namna Lisu anavyokubalika sana sana.
Ambacho sikuamini ni mwamko walionao vijijini ni mkubwa kuliko hata wa majiji. Vijijini wanasema kwa hii njaa ya miaka 5 hawawezi tena kuipa serikali hii kura. Jana nilivyokuwa narudi Dar es Salaam, nilipita takriban mikoa 7 kutoka kanda ya ziwa nimeshuhudia namna Mawakala wa upinzani walivyojipanga na kupeana semina wenyewe kwa wenyewe.
Bahati mbaya zikwenda kukusanya data za kisaisa ila kwa haya nilioyaona katika hiyo Mikoa 28 sioni namna Tundu Lisu akashindwa huu uchaguzi. Watu wamechoka, watu wana njaa, watu hawana fedha, watu wamekosa matumaini. Tena ukiwauliza maswali wanakujibu waziwazi kuwa kwa mbunge huyo sawa tutampa wa CCM ila suala la Urais Hapana tunampa "Mbeba Maono"
Lazima utakuwa nje ya TZ!JPM ameshashindwa uchaguzi hadi hapa tulipofika. Polisi wamesaidia sana kusambaza habari za Tundu Lissu.
Huo wimbo ushachuja mitano tena kwa jpmKazi kubwa ipi? Kazi kubwa ni kuwabambikia kesi kesi za uonevu unyanyasaji wafanyabiashara wakubwa kwa kutumia TRA? Kazi kubwa ni kuwabambikia kesi kuwapiga risasi wapinzani?
Zikiwa zimebaki siku 3 kabla hatujaingia tarehe 28.10.2020 siku ya kufanyika kwa uchaguzi Mkuu Tanzania, nadiriki kusema kuwa nchi naona inamtaka Lisu. Nimezunguka Mikoa 25 ya Bara na 3 ya Zanzibar, nimepita kila pembe ya nchi. Nimezunguka vijijini sana na kila kona ya nchi hii kwa shughuli za kikazi katika NGO aiseeee sijui nini kitokee ila nimeshuhudia kwa macho yangu na kuona namna Lisu anavyokubalika sana sana.
Ambacho sikuamini ni mwamko walionao vijijini ni mkubwa kuliko hata wa majiji. Vijijini wanasema kwa hii njaa ya miaka 5 hawawezi tena kuipa serikali hii kura. Jana nilivyokuwa narudi Dar es Salaam, nilipita takriban mikoa 7 kutoka kanda ya ziwa nimeshuhudia namna Mawakala wa upinzani walivyojipanga na kupeana semina wenyewe kwa wenyewe.
Bahati mbaya zikwenda kukusanya data za kisaisa ila kwa haya nilioyaona katika hiyo Mikoa 28 sioni namna Tundu Lisu akashindwa huu uchaguzi. Watu wamechoka, watu wana njaa, watu hawana fedha, watu wamekosa matumaini. Tena ukiwauliza maswali wanakujibu waziwazi kuwa kwa mbunge huyo sawa tutampa wa CCM ila suala la Urais Hapana tunampa "Mbeba Maono"
Kweli kabisa usemalo.2015 watu walikuwa huru, hata hapa watu tunaandika kwa taadhali sana