Nchi ya kwanza duniani iliyozikwa ikingali Hai

Nchi ya kwanza duniani iliyozikwa ikingali Hai

Gellangi

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2016
Posts
2,782
Reaction score
3,018
Umekuwa ni msiba mkubwa ambao ulilikumba Taifa hili lililobarikiwa utajiri wa kupigiwa mfano na unaotamaniwa na wapenda vinono duniani kote, Sasa yapata takriban miaka 58 imezikwa na hadi Leo inasadikika kuwa bado inapumua kwa shida shimoni(Kaburini).

Hii nchi ya kipekee duniani, hakukuwa na maombolezo rasmi na hadi leo matanga yanaendelea, mirathi yake ni migogogro mitupu. Wanaojaribu kudai Haki za nchi hii huandamwa na mauzauza ya walioiangamiza na wanaweza kupatwa na mabaya yasiyomithilika au kupotelea Kule ilikoenda nchi yao.

Watoto na wajukuu Wa nchi hii iliyofishwa wanagombana wenyewe kwa wenyewe hata kwenye kuandika muhtasari wa mustakabali wa Taifa lao na Sasa wanatawaliwa toka ng'ambo(Bahari kuu) na hawana mbinu za kujiasua.

Jambo hili linahitaji nguvu na akili ya ziada ili kuliweka sawa. Tufukue kaburi maana taarifa za kitaalam zinaonyesha kwa uhakika hajafariki maana tunaona mtikisiko chini ya Ardhi anavyopumua kwa taabu, tusipofanya hima atafariki rasmi muda si mrefu ujao.

Tujadili.
 
Sifahamu kwa nini watoto Wa nchi hii nzuri ya Mababu zetu wamekosa ujasiri Wa kumpigania mzazi wao kwa miaka yote hii? Hawataki wajukuu, vitukuu au vilembwe vya akina Mkwawa wasijadili au hata kulitaja jina zuri la nchi yao!
Kulikoni? Tujadili tafadhali ili kuiokoa nchi yetu.
 
Hatuna jema...waswahili wanasema tuna gubu..
 
Hatuna jema...waswahili wanasema tuna gubu..
Hatuna jema...waswahili wanasema tuna gubu..
Waswahili wanahusikaje kwenye suala nyeti linalohusu nchi yetu ya Urithi iliyozikwa ikiwa Hai?Unatuondoa kwenye mjadala Wa familia yetu kuunganisha nguvu kuifufua/kuifukua nchi ya Mababu zetu kina Kinjekitile?
 
Hakuna wa ngambo anayetawala..yupo kama kivuli rimoti zipo Tanganyika tokea gamso.

Hata usiwe na wasi wasi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Yeye anaweza akawa kivuli tu maamuzi yote yanatoka kwa mstaafu
 
Nchi ambayo watu wake wanaweza anzisha jambo la mabilioni ya pesa na bajeti ikatengwa, watu wakaanza mchakato wa kulifanya, ikafika tu pahala wakatofautiana, na jambo hilo likaishia njiani, na pesa zikatafunwa bila kufanikiwa kwa jambo hilo....! Na watu wa nchi ile wakakaa kiiimyaa bila kudai upotevu wa mabilion hayo!

Baada ya muda tena, watu wale wale waliosababisha hasara ya msbilion hayo, wanaanzisha kelele tena za jambo lilelile eti wanahitaji liwekwe mezani tena kwa Mara nyingine!

Shikamo taifa hilo lisilohesabu hasara!

Hili la katiba, napingana vikali na waliosababisha hasara hii kusema mchakato wa katiba uanze bila kutwambia mabilioni yaliyotumika nyakati zile yanarudije, ningependa kutoa rai kwa waliohusika kuleta hasara hii, bajeti yake waichangie wao na vyama vyao vyote vilivyohusika

Tusikubali itolewe pesa ya walipa kodi kwa jambo lilelile! Huu ni wizi na ufisadi wa kiwango cha rami!
 
Yeye anaweza akawa kivuli tu maamuzi yote yanatoka kwa mstaafu
Hivyo vivuli vya kufikirika ndivyo vimeifanya nchi ya urithi ya Mababu zetu akina Isike,Mirambo na Mareale iendelee kuumia kaburini kwa miaka 58 ingali hai.Hauelewi nini?
 
Nchi ambayo watu wake wanaweza anzisha jambo la mabilioni ya pesa na bajeti ikatengwa, watu wakaanza mchakato wa kulifanya, ikafika tu pahala wakatofautiana, na jambo hilo likaishia njiani, na pesa zikatafunwa bila kufanikiwa kwa jambo hilo....! Na watu wa nchi ile wakakaa kiiimyaa bila kudai upotevu wa mabilion hayo!

Baada ya muda tena, watu wale wale waliosababisha hasara ya msbilion hayo, wanaanzisha kelele tena za jambo lilelile eti wanahitaji liwekwe mezani tena kwa Mara nyingine!

Shikamo taifa hilo lisilohesabu hasara!

Hili la katiba, napingana vikali na waliosababisha hasara hii, ikibidi, hili la katiba, bajeti yake, kwa kuwa waliohusika kuleta hasara hii ni wanasiasa na vyama vyao, basi bajeti yake vyama vichangie,

Tunapenda kuendelea, si kwa upuuzi unaofanywa na wanasiasa kila uchwao
Sema wanasiasa Wa CCM ndiyo wanaopotezea mijadala ya Katiba Mpya wakiungwa mkono na vyama pendwa vyake.Ukija upande Wa watetezi wa kweli Wa Haki,Uhuru,Katiba mpya ni agenda ya kudumu since 1991/92.Hivyo siyo wanasiasa wote,wapo wanaofanya Kazi yao ipasavyo.
CCM imeizika Tanganyika yetu ikiwa Hai watashindwa kuua kitu gani?
Tujadili.
 
Nauliza kiungwana;Nani aliyeidhinisha Tanganyika izikwe ingali haijafa hadi Sasa?Alipewa mamlaka na nani?
 
Kosa la Tanganyika ambalo linaifanya ikose utetezi Wa watoto,wajukuu au vitukuu ni nini?CCM tuambieni,Kosa la nchi iliyopiganiwa na Mababu zetu,wakaikomboa bila kumwaga damu nyingi ni lipi hadi isistahili kuwepo kwenye ramani za dunia?Nini faida tuliyopata kwa kujizika sisi na nchi yetu?
 
hiyo nchi imefutiwa lugha ya kiingereza ambapo vijana wake wenye vipaji vya wasanii hawavuki nje ya mipaka kujipanua kimasoko. Lugha yao ya kimataifa irudishiwe maana katika mashindano ya commonwealth game hawana mawasiliano mazuri na wenzi wao kutoka mataifa ya nje huishia kutoa sheeepish smiles tu na kucheka !
 
Back
Top Bottom