Nchi ya kwanza duniani iliyozikwa ikingali Hai

Nchi ya kwanza duniani iliyozikwa ikingali Hai

Kulikuwa na wale G55 walijaribu kufufua nchi yao iliyozikwa, lakini walitawanywa kama vifaranga
 
Kosa kubwa linalofanyika hivi sasa hapa nchini ni kurithi makosa ya kuitawala yaliyofanyika hapo kabla, na hatimaye sasa kuyachukilia kama ndiyo miiko sahihi inayopaswa kufuatwa. Makosa hayo yamepelekea watu wengi kufungwa katika nira ya kutoweza kufikiria nje ya kasha.

Kuna kosa la kwanza litokanalo na kubinafsisha historia ya mapambano ya uhuru na kuyahusisha na watu wawili tu. Ijapkuwa kuna watu wengi sana ambao nyuma yao ipo sehemu muhimu ya historia kupitia michango yao ya kujitoa kwa hali na mali, bado ushiriki wao wala hautambuliwi, na pengine unafichwa kwa makusudi ili historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika na Zanzibar ubaki kuwa alama ya watu wawili, na kwa faida ya vyama vya TANU na ASP ambavyo ni wazazi wa CCM.

Wakati historia ikimpamba Nyerere kuwa ndiye mwamba pekee dhidi ya utawala wa kikoloni na kupeleka kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika. Kwa upande wa Zanzibar, historia inampamba Karume kuwa ndiye alama kuu ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Kosa la pili ni hili la muundo wa JMT. Mchakato mzima ulioileta serikali ya JMT ulitawaliwa na kasoro nyingi sana. Ni ukweli usiotia shaka kuwa muundo huu ulikuwa ni kama ule wa mchezo wa utotoni;
"Sanda kalawe, Amina! Mwenye kupata, Apate! Mwenye kukosa, Akose!"

Na kwa hakika ndivyo ilivyokuwa, Nyerere akaambulia urais wa serikali kuu ya JMT, na ili kumpooza wenzake akampasa kubakia na urais wake wa serikali ya Zanzibar, na hapo ndipo mwili wa iliyokuwa serikali ya Tanganyika ulopizikwa rasmi.

Badala ya kutambua uwepo wa serikali mbili zinazounda muungano na ziongozwe na mawaziri wakuu, na kisha itafutwe serikali kuu ambayo ingeongozwa na Rais wa JMT. Ubinafsi wa kutaka kuvitambua vya TANU na ASP kama sehemu pekee ya historia ya uhuru, na tamaa ya kugawana vyeo ndiyo ikapelekea kifo cha mpendwa wetu Tanganyika.
 
Katiba Mpya hasa ile rasimu ya Warioba itakuja kurahisisha upatikanaji wa vitu vingi na kimojawapo ni hicho mleta mada unacholilia.

Hivyo ni vyema tuelekeze nguvu zetu kwenye kuipigania Katiba Mpya kuliko kudai vitu kimoja kimoja, kwasababu naona kama tukianza kudai vitu kimoja kimoja tutazidi kujichelewesha kwenye kulifikia lengo letu bila kujua.
 
Kosa kubwa linalofanyika hivi sasa hapa nchini ni kurithi makosa ya kuitawala yaliyofanyika hapo kabla, na hatimaye sasa kuyachukilia kama ndiyo miiko sahihi inayopaswa kufuatwa. Makosa hayo yamepelekea watu wengi kufungwa katika nira ya kutoweza kufikiria nje ya kasha.

Kuna kosa la kwanza litokanalo na kubinafsisha historia ya mapambano ya uhuru na kuyahusisha na watu wawili tu. Ijapkuwa kuna watu wengi sana ambao nyuma yao ipo sehemu muhimu ya historia kupitia michango yao ya kujitoa kwa hali na mali, bado ushiriki wao wala hautambuliwi, na pengine unafichwa kwa makusudi ili historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika na Zanzibar ubaki kuwa alama ya watu wawili, na kwa faida ya vyama vya TANU na ASP ambavyo ni wazazi wa CCM.

Wakati historia ikimpamba Nyerere kuwa ndiye mwamba pekee dhidi ya utawala wa kikoloni na kupeleka kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika. Kwa upande wa Zanzibar, historia inampamba Karume kuwa ndiye alama kuu ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Kosa la pili ni hili la muundo wa JMT. Mchakato mzima ulioileta serikali ya JMT ulitawaliwa na kasoro nyingi sana. Ni ukweli usiotia shaka kuwa muundo huu ulikuwa ni kama ule wa mchezo wa utotoni;
"Sanda kalawe, Amina! Mwenye kupata, Apate! Mwenye kukosa, Akose!"

Na kwa hakika ndivyo ilivyokuwa, Nyerere akaambulia urais wa serikali kuu ya JMT, na ili kumpooza wenzake akampasa kubakia na urais wake wa serikali ya Zanzibar, na hapo ndipo mwili wa iliyokuwa serikali ya Tanganyika ulopizikwa rasmi.

Badala ya kutambua uwepo wa serikali mbili zinazounda muungano na ziongozwe na mawaziri wakuu, na kisha itafutwe serikali kuu ambayo ingeongozwa na Rais wa JMT. Ubinafsi wa kutaka kuvitambua vya TANU na ASP kama sehemu pekee ya historia ya uhuru, na tamaa ya kugawana vyeo ndiyo ikapelekea kifo cha mpendwa wetu Tanganyika.
Historia ya kupikwa ikafunzwa katika skuli zetu,Tanganyika ikazikwa bila maombolezo na jina lake likafanywa kuwa chukizo masikioni mwa watu.
 
Tuipiganie na kuinusuru Tanganyika kupitia Katiba mpya itakayoweka mizani sawa kuhusu Muungano na kuzitambua Tanganyika & Zanzibar kama washirika wa Muungano.
Lengo la mada ya kuitambulisha nchi ya kwanza duniani kujizika ikiwa na miaka 2 na hadi Leo inapumulia kifichoni.
Tunapojadili Katiba mpya tunamaanisha kuzifuta ziitwazo kero za Muungano zitokanazo na Tanganyika kupelekwa msukule/kaburini na hivyo kuiacha Zanzibar ikiwa mpweke.
Tujadili.
 
Back
Top Bottom