Nchi ya Rwanda inaadhimisha miaka 30 tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari dhidi ya watutsi mwaka 1994

Nchi ya Rwanda inaadhimisha miaka 30 tangu kutokea kwa mauaji ya kimbari dhidi ya watutsi mwaka 1994

dubu

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2011
Posts
3,502
Reaction score
3,483

kumbukumbu inayofanyika Jijini Kigali na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoka barani Afrika, Ulaya, Amerika na Asia wakiongozwa na Rais Paul Kagame.

Ishara ya kuanza kwa kumbukumbu ya mauaji ya kimbari ni pamoja na kuwashwa kwa mishumaa katika eneo la Gisozi mahala ambapo mabaki ya miili ya watu zaidi ya 250,000 imezikwa katika kaburi la pamoja.

Mauaji hayo ya kimbari yalianza April 7, 1994 siku moja baada ya Ndege iliyombeba Rais wa wakati huo Juvenali Habyarimana na aliyekuwa Rais wa Burundi Cyprian Ntaryamira kudunguliwa wakati ikijiandaa kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kigali.

Baada ya tukio hilo majeshi ya serikali ya wakati huo na makundi yenye silaha ya Impunzamugambi na Intarahamwe yaliyokuwa na unasaba na chama tawala MRND yalianza kuwaua watu wa Jamii ya watutsi na wahutu wenye msimamo wa wastani.

✍🏿 @fredricknwaka
🎤 @e_j1official
 
Kwanini wanakumbuka siku hii Mbaya...!?
 
Mauaji ya kimbari ya watutsi utadhani wahutu nk hawakufa, huu upandaji chuki wa ajabu, ni aina nyingine ya kutengeneza uadui na fukuto kwenye mioyo ya watu (wahutu) hasa wanaoujua ukweli wa kipindi hicho, masimulizi na hadithi hurithiwa vizazi Hadi vizazi
 
Jamaa amefanikiwa kuilaghai dunia wakati yeye na kikundi chake ndiyo wauaji.
Hajalaghai yoyote. Dunia tunaenda naye kidiplomasia kwa kuangalia maslahi mapana. Siku akijichanganya anawekwa sawa.
 
Unaweza kuwafanya watu wajinga kwa muda lakini hauwezi kuwafanya watu wajinga milele.
 
Back
Top Bottom