Ndani ya Daladala!......

Enzi zile stendi ipo mwenge,Konda kamkoromea jamaa fulani yupo simple tuu.jamaa kila akiuchuna konda anachonga tuu,nikaona jamaa kashika simu kwa muda halafu kaweka mfukoni tunakaribia kituo cha jeshi pale mbele lugalo nikaona wala wenye kofia nyekundu wapo wa3 wanaelekeza gari ielekeee kule ndani.........Itaendelea.
 
Reactions: Lee
Unakuta gari liko moja na lishajaa ila konda anazidi kusema sogea nyuma" Abiria unaanza kuhamasisha tushuke wote tuu"konda anakuchora tuu,ile unashuka tu anagonga gari iondoke.....
 
Siku moja nilishuhudia konda kagoma kumpakia abiria fulani maeneo fulani baada ya gari aliyopanda kuishia njiani kisa eti Yule abiria aliringa kupanda gari yake kule kituoni sasa kamkuta tena mbele anamwambia we si una haraka!
 
napenda sana daladala siku moja moja hua napanda hasa mwendokasi nikiwa dar. ila mwendo wa huku zanzibar ni tofauti
 
Hakuna kinacho niuzi kama mishuzi!
 
[emoji23] [emoji23] gari lenyewe la mkopo hii hua naitamka sana hii
 
Juzi kati nimepanda UDART. Bas kulikuwa mshua mmoja anakanyaga popote pale iwe ni juu ya mtu au juu ya mguu wa mtu, kwake sawa tu. Ikabidi nisimamie mguu mmoja halafu mguu mwingine unashuka kwa machale pale napopata upenyo.
Watu kama hao inabidi umkanyage yeye makusudi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…