Ndani ya Daladala!......

Ukitaka kusafiri bure we kila asubuhi toa noti ya 10,000! Siku 5 kati ya 7 konda atakuachia!
 
Raha kusimama nyuma ya msambwanda, tatizo daladala inawahi kufika kituoni!
Nyie ndo madunga dunga yenyewe, unang'ang'ana mbele husogei nyuma husogei utazania umekanyaga supaglu iliyomwagika
 
Tupo mkuu tumejaa
Naona kila mtu anajidai mpanda daladala. Wewe unapanda la wapi? Daladala kiboko za m'nyamala ikifika pale A abiria mnabaki wawili wanaingia mateja 10 akili kichwani hapo
 
Naona kila mtu anajidai mpanda daladala. Wewe unapanda la wapi? Daladala kiboko za m'nyamala ikifika pale A abiria mnabaki wawili wanaingia mateja 10 akili kichwani hapo
Sio kujidai rrondo huo ndio ukweli mm nap and a mwendokasi naelekea mbezi
 
Reactions: Lee
Daladala za mwananyamala kuna dereva mmoja teja halafu mlevi yaani maarufu kishenzi huyo jamaa,siku nimepanda gari lake amelewa chakari halafu haogopi hata trafiki yaani kupita pale vijana club wakapanda wenzake kama kumi hizo story humo ndani nilijua tumetekwa!
 
Kuna siku nimepanda daladala mzee mmoja kalewa ananiuliza kwanini simuoi binti wake amesoma ana masters ila yuko home tu anaangalia tv!
Hahaha ukamjibu vipi sasa
 
Hivi mwendokasi kuna drama kama hizi zetu kawe-mbagala rangi tatu?
Unanikumbusha mbaali sana, enzi flani nikiwa Mgulani j... Jioni wakati wa kurudi, magari ya mbagala yalikuwa ya shida sana, yaani wakati wa kupanda mnagombania na unaweza kuingizwa ndani kwa kubebwa juu juu, mtajikuta midume mitupu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…