Ndani ya katiba mpya, Rais aondolewe kwa kura na sio kwa mihula miwili

Ndani ya katiba mpya, Rais aondolewe kwa kura na sio kwa mihula miwili

Nadhani mmoja ya kazi za Tume ya Uchaguzi na vyama vya siasa ni kuwapa wananchi elimu ya upigaji kura. Ni bahati mbaya kwamba vyama vya siasa vinajikita kwenye kulumbana badala ya kuwaonesha wananchi / wapiga kura ni kwa nini wao wanafikiri wakiwa madarakani watakidhi matarajio ya wananchi ili kwayo wananchi waamue ni nani wampe kura.
Aidha baadhi ya viongozi kuhama vyama vyao kunaashiria kwamba hata wao ama hawajui wafanyacho au wanajua walifanya makosa kuingia huko wanakotoka.
Kimsingi tukubaliane kwamba: "Katiba nzuri inatoa Tume ya Uchaguzi nzuri na Tume ya Uchaguzi nzuri inatoa viongozi wazuri (baada ya wananchi kuelemishwa vizuri juu ya namna nzuri ya kuchagua viongozi wao) na viongozi wazuri (kutokana na vyama kuwa makini juu ya kuteua wapigiwa kura) watatoa matokeo mazuri ambayo yataipeleka mbele nchi yetu kwa uzuri"
Bado nasimamia hoja yangu kwamba "raisi aendelee kuchaguliwa kwa kura, na sio kwa mihula"!
Kinadharia upo sahihi uyasemayo ila kiuhalisia ni tofauti sana.

Elimu ya upigaji kura ya miezi isiyozidi 6 au tuseme mwaka 1 haiwezi kuwa mbadala wa elimu ya sekondari na ya elimu ya juu.

Elimu ya upigaji kura haifundishi kuongeza uwezo wa kufikiri namaanisha haiongezi reasoning capacity ya mtu kwa kiwango kama cha elimu ya sekondari na kuendelea elimu ya juu.

Katika hali yetu ya umasikini bado rushwa ktk uchaguzi ni kikwazo hata mbele ya elimu ya upigaji kura.
 
We ndo kilaza kabisa, kuna nin cha kuiga kwa chandimu, kama hujui sasa hata kwa katiba ya sasa hilo lipo ila limewekwa kwa wabunge kithungu wanasema (VOTE OF NO CONFIDENCE) lakin sijaona kibaya cha mpaka kufikia huko zaidi utakuwa unatafuta machafuko na nchi haitatawalika, maana leo akiamka huyu anataka kura kumuondoa huyu madarakan hali hiyo itaendelea,
Fikiri kwanza kabla ya kupost
 
Sanduku LA kura haliamui mshindi labda kwa nchi zilizoendelea
 
Nani akupe katiba mpya??....unafikiri ni mafala kiasi hicho?!!
 
Kama katiba itatokea kufanyiwa marekebisho, nashauri raisi aondolewe na kura na sio kwa ukomo wa mihulai. Hii itamuwezesha raisi aliyepo madarakani kukamilisha dhima yake au kama ameshindwa, kumuondoa madarakani. Hali hii inaweza kumfanya kiongozi anayefaa kuendelea kuiongoza nchi na yule ambaye hafai kuishia atakakoishia. Kura iamue na sio mihula!
Tuige mfano wa CHADEMA, Urusi, Ujerumani, Uchina, n.k

Utapata tabu sana
 
Back
Top Bottom