Ndege ya ATCL iliyokamatwa uholanzi mbona hatuambiwi chochote; au ndiyo basi tena?

Ndege ya ATCL iliyokamatwa uholanzi mbona hatuambiwi chochote; au ndiyo basi tena?

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,892
Reaction score
7,780
Huku nyuma awamu ya 5 kila jaribio la wale nawaita wahuni kushika ndege za ATCL ili kulipwa madeni ya mchongo na Tanzania yamekua yanashindwa na ndege zimekua zinaachiwa baada ya muda mfupi. Wakati wa awamu ya 5 tuliona pale jaribio la kushika ndege ya ATCL kule afrika ya kusini liliposhindwa.

Wengi tunaamini hakuna mikataba na wawekezaji inafutwa kinyume na sheria za Tanzania ila wawekezaji hawaridhiki bila kuikomoa nchi kwa madai ya kutaka kuchuma utajiri bila ya kua wamewekeza kitu.
Pia wananchi wanaamini vigogo wenye nia ya kupiga hela ya umma hushirikiana na hao wanaodai ili kupewa fungu.

Tangu ndege ya ATCL ikamatwe uholanzi kwa kile kinasemekana ni serikali kudaiwa kimepita kipindi kirefu zaidi ya kama miezi sita. Kuna uvumi kwamba wapo vigogo wanakula njama na wageni hata kutaka kuuza ndege hiyo. Ingefaa kutolewa taarifa ya wazi nini kinaendelea kwenye hili sakata la kuzuiliwa ndege mali ya umma.
 
Huku nyuma awamu ya 5 kila jaribio la wale nawaita wahuni kushika ndege za ATCL ili kulipwa madeni ya mchongo na Tanzania yamekua yanashindwa na ndege zimekua zinaachiwa baada ya muda mfupi...
Inawezekana haikukamatwa ila kuna wajanja wanataka kuiiba.
 
Huku nyuma awamu ya 5 kila jaribio la wale nawaita wahuni kushika ndege za ATCL ili kulipwa madeni ya mchongo na Tanzania yamekua yanashindwa na ndege zimekua zinaachiwa baada ya muda mfupi...
Nani alikudanganya yameshindwa? Si ingefanywa sherehe ya kitaifa.

Ndege zote zilizokamatwa madeni yalilipwa ndiyo zikaachiwa.

Kujimwambafai ni hapa tu kwa wajinga ndiyo waliwao. Huko duniani hakutaki kujimwambafai, utaumbuka.
 
Mkiambiwa jiwe aliinajisi nchi muwe mnaelewa. Na bado ndege nyingine inatafutwa. Ikamatwe.
 
Nani alikudanganya yameshindw? Si ingefanywa sherehe ya kitaifa.

Ndege zote zilizokamatwa madeni yalilipwa ndiyo zikaachiwa.

Kujimwabafai ni hapa tu kwa wajinga ndiyo waliwao. Huko duniani hakutaki kujimwambafai utaumbuka.
Sasa na sasahivi si walipe!
 
Makosa yote yaliyo pelekea kukamatwa ndege yalifanywa na serikali ya Mwendakuzimu.
Afadhali waje waikate ile boti Mv Bagamoyo MaguMashi .
 
Nani alikudanganya yameshindwa? Si ingefanywa sherehe ya kitaifa.

Ndege zote zilizokamatwa madeni yalilipwa ndiyo zikaachiwa.

Kujimwambafai ni hapa tu kwa wajinga ndiyo waliwao. Huko duniani hakutaki kujimwambafai, utaumbuka.
Ujinga mtupu
 
Makosa yote yaliyo pelekea kukamatwa ndege yalifanywa na serikali ya Mwendakuzimu.
Afadhali waje waikate ile boti Mv Bagamoyo MaguMashi .
Kuna madeni lukuki na makubwa ya enzi ya Kikwete ya kukodisha Airbus kwa Lebanese bado hazina inalipa kama deni la nje!

Ndege za ATCL hazikanyagi huko Pretoria kwa kuogopa zitakamatwa sababu ya madeni ya enzi ya Kikwete!

Halafu kuna mbwiga humu wanamsifia eti alikuwa Rais bora kuliko waliomtangulia!
Kaingia amekuta lundo la foreign reserve Mkapa alizomuachia akazikomba zote kwa mambo yasiyo na maana!
 
Back
Top Bottom