Ndege ya ATCL number TC 106 Bomberdier, tairi moja ni kipara mpaka nyuzi zinaonekana kabisa

Maelezo ya ATCL hayakutokana na jinsi wasio na utaalam wa ndege wanavyoendelea kutaka iwe bali ushahidi wa miongozo ya watengeneza ndege. Bado nakubaliana nao kuwa wanakazi ngumu ya kuelimisha umma ambao unataka eti waachane na misingi iliyowekwa na wataalam na kuchukua mawazo ya mitandaoni kutoka kwa watu wasio na uekewa bali hisia. Kibaya zaidi hisia za wengi ni siasa tu bila msingi wowote wa ufahamu au hata uelewa. Nitafurahi kama JF itajiongeza na kupata ukweli wa watengenezaji wa ndege kupinga ushahidi wa ATCL. Tairi ya ndege ina matabaka manne sio ya fuso hiyo.
 
Umejibu kwa jeuri sana mkuu bahati mbaya hukuwa unajua chochote juu ya unachokitetea!!

Uliwahi kuona wapi tairi isiyojazwa upepo ikaisha Kwa staili hiyo?

hata tairi ya wheel barrow haijawahi kutoa nyuzi nyuzi kwenye kuisha kwake..
Soma mwongozo wa watengeneza ndege na uwe na uekewa wa sayansi ya ndege ndio utoe mlinganisho wa bajaji au land cruiser. Tatizo hatusomi na kuanza kutoa ufafanuzi usio na kichwa. Mwongozo wa mtengeneza ndege unazungumzia hizo nyuzi. Ndege inatua toka juu na ndio inatembea. Inapotua speed yake ni karibu 250km kwa saa na inapokimbia kuruka speed pia iko hivyo. Uzito wake ni mkubwa. Break zake sio za bajaji au benz!
 
Unajua nilitegemea wewe na wataalam wenzio hapo shirikani, mngetumia utaalamu wenu kuiponya nchi na siyo kuiangamiza!

Nimeshangaa kwa ujasiri mkubwa kabisa mnasema ile tairi ndiyo kwanza ina mruko mmoja..

mruko mmoja iishe vile? Mbona ya pembeni yake haijaisha hivyo? Hata kama tairi ya ndani na ya nje uishaji wake si sawa, ndiyo kuwe na tofauti kubwa hivyo?

Inawezekana being a common /layman ndiyo inanifanya nisielewe maelezo yako yenye utaalamu wa hali ya juu sana..

By the way, umeniquote wakati nilikuwa namuuliza huyo aliyedanganya eti tairi zenu hazijazwi upepo!

Kama utetezi wako utaendelea kuwa wa namna hiyo naomba usiniquote mkuu!

Nakuheshimu sana..
Ahsante!!!
 
@NOD hoja kama hizi unaziruka, tolea ufafanuzi mambo kama haya..

Uwe na mda mwema!!
 
@NOD hoja kama hizi unaziruka, tolea ufafanuzi mambo kama haya..

Uwe na mda mwema!!
Mkuu hizi ndio hoja. Kuhusu rangi, Emirates ana hoja ya msingi maana repainting ni gharama, ingawa sijui kama argument yao kama ni hiyo tu, na siwezi kukubali uniingize gharama kwa kuniletea ndege mpya na tayari ina defect. Huu mfano hauna mahusiano na suala la ATCL.

Hoja ingine yenye mashiko ni maelezo ya Goodyear ambao ni watengeneza matairi ya ndege maarufu. Nime copy na ku paste maagizo ya Goodyear aliyotuma mleta hoja.
Aircraft tires should be removed when the tread is worn to the base of any groove at any spot, or to the minimum depth stated by the aircraft manufacturer." Kama kizungu kiko sawa " or to the minimum depth stated by the aircraft manufacturer " .
De Havilland ndio aircraft manufacturer na ushahidi wa ATCL ni maagizo ya huyo aircraft manufacturer. Case closed. Kwa hiyo hao wachumia tumbo kama alivyowaita wako sahihi. Mwambie mleta hoja awe anasoma mpaka mwisho. Tatizo kubwa hata hiyo document ya maagizo ya muunda ndege ambayo ndio mwongozo wa ATCL na lazima ithibitishwe na TCAA na pia ukaguzi wa IATA (IOSA) haisomwi na kuja na reference za tairi ya gari. Bado nina imani na ATCL.
 
Mkuu hebu concentrate hapa,

"An aircraft tyre should be removed when the tread is worn to the base.."

Kama manufacturer ndiyo amerecommend hivyo kwanini utetezi wako upingane nae kwamba ile tairi bado ni salama?

Yaani unaona kabisa unachokitetea wewe ni sawa?

Usinikwaze mkuu!!
Ahsante!
 
Umewahi kupanda ndege? Kama jibu lako ndio basi usingeuliza swali hili!
Na jibu lake kama ni 'ndio', anatakiwa aulizwe swali la pili. 'Je ulipanda ndege ya aina gani?'. Sababu kuna ndege ambazo ukiwa ndani dirisha lolote, huwezi ona tairi lolote.
 
Mkuu, Naomba usome De Havilland procedure ya kufuatilia matumizi ya tairi na maagizo yao katika ubadilishaji kama ilivyorejewa na ATCL kama document inayowaonggoza. Ukaguzi wa TCAA na IATA (IOSA) unaangalia hayo maagizo na utekelezaji wake sio vinginevyo. Siwezi kutetea uzembe ila tujue maana ya msemo wa kuwa huwezi kuwa mtakatifu kuliko Papa. Mimi swali langu kwa ATCL litakuwa watupe evidence ya jinsi wanavyotimiza maagizo ya De Havilland kama walivyorejea na kutoa hisia za mtandaoni au observation ya abiria. Kitu kingine muhimu, reference ya mtoa hoja ni tairi ya Goodyear wakati maagizo ya De Havilland yanaagiza zitumike tairi za Dunlop retreadable. Governing document ni manufacturer wa ndege na ndio maana hata Goodyear anakwambia kama manufacturer atavyoagiza. Likitokea lakutokea liability ni manufacturer siyo muuza tairi maana maagizo yake ndio mwongozo uliopitishwa na mamlaka za usimamizi. Sitarajii kuwa mtengeneza ndege mahili kama De Havilland akatoa maagizo ambayo ana mashaka nayo maana itakula kwake. Kujiona huku mitandaoni tunajua kuliko manufacturer sidhani kama ni kweli unless ATCL wameweka document fake. Tusihukumu kwa hisia bali ushaidi wa kitalaam na kisheria kama walivyotoa ATCL.
 
walitoa ufafanuzi kwamba kwa mujibu wa expire dates za matairi yao hilo bado lina miruko 7 hivi kwahiyo sio case, Nchi ina mazombie hii sijapata kuona yani mtu anaandaa taarifa kwa umma kabisa kuongelea utumbo wa picha ambayo iko obvious . SHAME.
 
walitoa ufafanuzi kwamba kwa mujibu wa expire dates za matairi yao hilo bado lina miruko 7 hivi kwahiyo sio case, Nchi ina mazombie hii sijapata kuona yani mtu anaandaa taarifa kwa umma kabisa kuongelea utumbo wa picha ambayo iko obvious . SHAME.
Picha iko obvious machoni kwako sio kwa wataalam na watengenezaji waliotoa maagizo hayo. Tusichanganye ukipara wa tairi ya Toyo au Vits au hata Range Rover na tairi ya ndege. Fuata maagizo na siyo hisia na obvious ya macho yako. Bado nasimama na ATCL kuwa wako sahihi. Kwanza ukiangalia miruko ya ndege hiyo sio zaidi ya siku mbili tu maana Dar kwenda Mwanza then Bukoba na kurudi ni miruko minne tayari. Kama atakwenda Mbeya na kurudi ni miruko miwil zaidi. jumla miruko sita! Hisia zako na reality ya wataalam vinaweza visiendane. ATCl fuata utaalam mambo ya mitandao tuachie😀
 
Kwa haya maelezo sina tatizo kabisa na wewe mkuu na moyo wangu ni mweupe!

Sasa turudi kwenye uhalisia, wewe kama mtaalam na mtu mwenye uzoefu wa kutosha kwenye haya maswala,

Unakubaliana na ATCL kwamba ile tairi ina mruko mmoja? Kama mruko mmoja tu ndiyo imeburuzwa kiasi hicho, baada ya miruko minne itakuwa na hali gani?

Kama manufacturer kasema ibadilishwe baada ya miruko 8, na mruko mmoja ndiyo inafanana hivyo , unafikiri itamaliza miruko iliyobakia?
 
Bro nakupongeza hata atcl watakupongeza , kumkumbusha mtu wajibu wa kazi sio kosa wala uadui bali ni nia Njema , Naweza kusema Mtazamo wako na wangu unafanana .
Kuna tukio huko UK abiria alikuwa dirishani Akaona Injini inatema moto lakini hakutoa taarifa rubani Hakuona kwasababu isioeleweka akaizima Injini nzima yenye power akaacha isiyokuwa na power inayotema moto ,
Mwisho wa yote ndege ilipokosa power ya Kukaa angani rubani akaishusha kwa mtindo wa belly landing , Ikatua kwa tumbo Kwenye eneo lenye miti
Yule abiria akajuta Kwanini hakumjulisha mhudumu wa ndege

Inajulikana kuwa tunatakiwa tutoe taarifa tukiona miundombinu inaharibika iwe ni reli , umeme , ndege nk
 
Mkuu tuanze na huo mburuzo na ndio kuna issues nyingi. Miburuzo ya tairi ya ndege inasababishwa na tear and wear ya kawaida ya kuruka na kutua pia kuna mambo ya break za nguvu (harsh breaking) na hali ya njia ya kurukia ndege (runway surface condition). Mchubuko kwa mujibu wa document ya De Havilland ni ile hali ya kufikia nyuzi za tairi (reinforcement cord) siyo kipara cha kuisha michoro kama ilivyo kwa magari. Tuisome tena document ya De Havilland ili tujue wana maana gani unless english iwe imenipita pembeni. Mchubuko wa kwanza ukionekana anatakiwa asizidi miruko minane ndio maelekezo ya De Havilland. ukiangalia miruko ya ndege hiyo, miruko minane inaweza ikaisha kwa siku moja au mbili tu maana Dar kwenda Mwanza then Bukoba na kurudi ni miruko minne tayari na kama ataongeza kutoka Dar kwenda Mbeya na kurudi ni miruko miwil zaidi, na jumla itakuwa miruko sita kwa siku. Kwa kuangalia hiyo michubuko sio kuisha michoro ndege hiyo ina uwezo wa kutua tena mara saba bila matatizo. Nasema hivi kwa sababu kuna matabaka manne kabla ya kufikia sehemu ya upepo. Kwa maana hiyo, tairi ina usalama bado kutokana na muundo wake. ATCL, nikiangalia maelekezo ya De Havilland, huwa hawachongi (retreading) tairi zao zikiisha bali wanatupa. Kama wangekuwa wanachonga tairi zao wangepewa muongozo tofauti. Niseme tu tena kuwa huwezi ukahukumu kwa macho bila utalaam na uelewa wa maagizo ya watengenezaji. Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) hufuatia uelewa na utekelezaji wa hiyo miongo. Ukaguzi wa IATA (IATA Operational Safety Audit - IOSA) pia unajukumu la kuhakikisha ATCL wanakidhi matakwa haya na kinyume cha hapo wananyimwa cheti.
 

Na barabarani mnaendesha magari yenye vipara zaidi ya hilo tairi la ndege lenye kutumika kutua na kupaa tu. Na trafik hata hawawakagui , na mnapiga speed ya 160 km/ hr
 
Hii ni Atari kuliko wanavyodhani. Hapo Engineer aliekagua na kujaza log book ahojiwe. Rubani pia anatakiwa kuhojiwa kwanini aruhusu kuruka na tairi kama Hilo.
Nafikiri Matindi na Tim yake wajichunguze

Hujui utaratibu wa kurusha ndege
 
Na barabarani mnaendesha magari yenye vipara zaidi ya hilo tairi la ndege lenye kutumika kutua na kupaa tu. Na trafik hata hawawakagui , na mnapiga speed ya 160 km/ hr
kwanza toa huo uongo wako wa kuonabwatu wanaendesha magari kwa speed hiyo, hizo barabara mnazo?

Na uliniona nikiendesha hilo lorry?

Tweneke Ng'wanamangilingili

Ulinyoo bebe???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…