Ndege ya ATCL number TC 106 Bomberdier, tairi moja ni kipara mpaka nyuzi zinaonekana kabisa

Ndege ya ATCL number TC 106 Bomberdier, tairi moja ni kipara mpaka nyuzi zinaonekana kabisa

Mkuu tuanze na huo mburuzo na ndio kuna issues nyingi. Miburuzo ya tairi ya ndege inasababishwa na tear and wear ya kawaida ya kuruka na kutua pia kuna mambo ya break za nguvu (harsh breaking) na hali ya njia ya kurukia ndege (runway surface condition). Mchubuko kwa mujibu wa document ya De Havilland ni ile hali ya kufikia nyuzi za tairi (reinforcement cord) siyo kipara cha kuisha michoro kama ilivyo kwa magari. Tuisome tena document ya De Havilland ili tujue wana maana gani unless english iwe imenipita pembeni. Mchubuko wa kwanza ukionekana anatakiwa asizidi miruko minane ndio maelekezo ya De Havilland. ukiangalia miruko ya ndege hiyo, miruko minane inaweza ikaisha kwa siku moja au mbili tu maana Dar kwenda Mwanza then Bukoba na kurudi ni miruko minne tayari na kama ataongeza kutoka Dar kwenda Mbeya na kurudi ni miruko miwil zaidi, na jumla itakuwa miruko sita kwa siku. Kwa kuangalia hiyo michubuko sio kuisha michoro ndege hiyo ina uwezo wa kutua tena mara saba bila matatizo. Nasema hivi kwa sababu kuna matabaka manne kabla ya kufikia sehemu ya upepo. Kwa maana hiyo, tairi ina usalama bado kutokana na muundo wake. ATCL, nikiangalia maelekezo ya De Havilland, huwa hawachongi (retreading) tairi zao zikiisha bali wanatupa. Kama wangekuwa wanachonga tairi zao wangepewa muongozo tofauti. Niseme tu tena kuwa huwezi ukahukumu kwa macho bila utalaam na uelewa wa maagizo ya watengenezaji. Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) hufuatia uelewa na utekelezaji wa hiyo miongo. Ukaguzi wa IATA (IATA Operational Safety Audit - IOSA) pia unajukumu la kuhakikisha ATCL wanakidhi matakwa haya na kinyume cha hapo wananyimwa cheti.
Asante kwa ufafanuzi mzuri mkuu!

Nilianza mjadala kwa gadhabu lakini hukunipuuza wala kunichoka..

Umejibu kwa hekima sana na nimejifunza kitu kikubwa sana kutoka kwako!

Barikiwa!!
 
Hii ni hatari kuliko wanavyodhani. Hapo Engineer aliekagua na kujaza log book ahojiwe. Rubani pia anatakiwa kuhojiwa kwanini aruhusu kuruka na tairi kama Hilo.

Nafikiri Matindi na Timu yake wajichunguze
Hii yote ni sahihi lakini kama kungekuwa na mfumo mzuri wa check and balance .ndege zilinunuliwa kisiasa na ni za serikali hakuna mtu angeweza kupinga au kuhoji ufanisi bila ya yeye kutikiswa .

Hakuna mechanism ya kuiwajibisha serikali ,mfano magari mengi ya serikali hayana bima na yana overspeed , lakini hutakuta yamekamatwa na kuwajibishwa, serikali inaweza ikaanzisha shule na kusiwe na vyoo au maabara , maktaba nk na itakuwa salama hutasikia taasisis yoyote ikenda kukagua shule za serikali na kuziwajibisha , ila kwa mtu binafsi hawezi kuwa na shule yenye mapungufu bila taasisis za serikali kumsumbua na faini.
Moja ya risk za serikali kufanya biashara ndo mambo kama hizi , haiwajibishwi!
 
Mkuu tuanze na huo mburuzo na ndio kuna issues nyingi. Miburuzo ya tairi ya ndege inasababishwa na tear and wear ya kawaida ya kuruka na kutua pia kuna mambo ya break za nguvu (harsh breaking) na hali ya njia ya kurukia ndege (runway surface condition). Mchubuko kwa mujibu wa document ya De Havilland ni ile hali ya kufikia nyuzi za tairi (reinforcement cord) siyo kipara cha kuisha michoro kama ilivyo kwa magari. Tuisome tena document ya De Havilland ili tujue wana maana gani unless english iwe imenipita pembeni. Mchubuko wa kwanza ukionekana anatakiwa asizidi miruko minane ndio maelekezo ya De Havilland. ukiangalia miruko ya ndege hiyo, miruko minane inaweza ikaisha kwa siku moja au mbili tu maana Dar kwenda Mwanza then Bukoba na kurudi ni miruko minne tayari na kama ataongeza kutoka Dar kwenda Mbeya na kurudi ni miruko miwil zaidi, na jumla itakuwa miruko sita kwa siku. Kwa kuangalia hiyo michubuko sio kuisha michoro ndege hiyo ina uwezo wa kutua tena mara saba bila matatizo. Nasema hivi kwa sababu kuna matabaka manne kabla ya kufikia sehemu ya upepo. Kwa maana hiyo, tairi ina usalama bado kutokana na muundo wake. ATCL, nikiangalia maelekezo ya De Havilland, huwa hawachongi (retreading) tairi zao zikiisha bali wanatupa. Kama wangekuwa wanachonga tairi zao wangepewa muongozo tofauti. Niseme tu tena kuwa huwezi ukahukumu kwa macho bila utalaam na uelewa wa maagizo ya watengenezaji. Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA) hufuatia uelewa na utekelezaji wa hiyo miongo. Ukaguzi wa IATA (IATA Operational Safety Audit - IOSA) pia unajukumu la kuhakikisha ATCL wanakidhi matakwa haya na kinyume cha hapo wananyimwa cheti.
Mkuu Atcl wamejibu kisisasa , cha kushukuru ni kuwa wameonyesha kulikubali tatizo na kuondoa taharuki kitu ambacho naona wamefanya sahihi kabisa

De havilland , hatengenezi tairi!! Hoja ya ubora au uimara au red line ya matairi ilitakiwa ijibiwe na trye manufactures , de havilland hapo ametumiaka kutoa uzoefu wake kwa tairi kwa ndege yake ya bombadier lakini wenye tairi zao wanaeza kuja na hoja tofauti kabisa kwa hali ike ya tairi , so far to date , watengenezaji mashuhuri wa tairi za ndege ni goodyear , dunlop na kwa sasa michellin anasogeasoge on top,
Cha kushukutu mungu ni inaonekana halitajirudia tena hilo swala
 
Back
Top Bottom