mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,897
- 18,477
Rais tumemchagua sisi wenyewe kwa mujibu wa katiba. Anaongoza serikali na nchi kwa jumla kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi kwa ujumla wake. Kutokumtii Rais ni kuwadharau wananchi na kutokuitii katiba ambayo imemweka madarakani. Huo ni upande mmoja wa shilingi. Upande wa pili ni kwamba Rais kuongoza nchi kinyume na sheria au kutoa maagizo yaliyo tofauti na sheria zilizopo ni kutokuitii katiba na wananchi waliomweka madarakani. Rais ni mtumishi wa watu na ana haki kwa mujibu wa katiba kuongoza nchi kwa manufaa ya wananchi. Kama akafika mahali akaona kwamba anataka kutoa maagizo yatakayokuwa na manufaa kwa wananchi wake, lakini kwa sasa maagizo hayo yanaonekana kukinzana na sheria zilizopo, basi ufanyike utaratibu wa kikatiba wa kufanyia marekebisho sheria hizo ili zitoe uhalali wa maagizo ya Rais kutekelezwa bila kuvunja sheria.
Kwa hiyo kama Rais ameona ni kero na haina tija kwa wananchi kudaiwa malimbikizo ya kodi, tukubali kuwa kupanga ni kuchagua!! Basi yaandikwe mapendekezo ya marekebisho ya sheria ihusuyo ukusanyaji wa kodi unaofanywa na TRA. Hawa TRA wapigwe marufuku kwa mujibu wa sheria KUDAI MALIMBIKIZO YA KODI kwa wafanyabiashara wote, na siyo wa kariakoo tu (sheria ni msumeno), halafu tusikilizie utamu wake!! Vinginevyo itakuwa akidaiwa malimbikizo ya kodi mfanyabiashara aitwaye MUHOGO MCHUNGU halitatoka tamko la kusema TRA wasimdai malimbikizo ya kodi, lakini akidaiwa malimbikizo ya kodi mfanyabiashara aitwaye MUHOGO MTAMU, fasta litatoka tamko la kusema TRA wasimdai malimbikizo ya kodi.
Lingine (AMBALO NDIYO KIINI CHA MAWAZO YANGU), naomba tusiwe tunapotosha au tunatafsiri vibaya kauli na matamko ya Rais wetu mpendwa. Siamini kabisa kuwa Rais ametoa tamko la kuzuia TRA wasidai malimbikizon ya kodi, kama ni hivyo atawezaje kutekeleza mipango ya serikali?. Ila ninaamini kuwa hakubaliani na namna inayotumiwa na TRA kukusanya hayo malimbikizo ya kodi. Hakubaliani na TRA kufunga biashara za watu kwa kisingizio cha malimbikizo ya kodi. Rais anataka TRA na Wafanyabiashara wakae pamoja wazungumze namna rafiki ya kulipa hayo malimbikizo na si kwa kutumia mabavu ya kufunga biashara zao. Biashara zikifungwa serikali itapata wapi mapato yake? Hiyo pesa ya kulipa MISHAHARA MINONO YA TRA ITATOKA WAPI?
Maana haiingii akilini, ninyi TRA mlikuwa wapi hadi mfanyabiashara huyu MUHOGO MTAMU/MUHOGO MCHUNGU akalimbikiza kodi kwa miaka kadhaa? Picha ninayoipata ni kuwa baadhi ya watumishi hawa wa TRA waliridhia mfanyabiashara huyu alimbikize kodi kwa kuwa alikuwa anawapa kitu kidogo (japo inasemekana TRA hupokea kitu kikubwa, ila Polisi ndio hupokea kitu kidogo-sina uhakika na hilo).
Kwa hiyo kama Rais ameona ni kero na haina tija kwa wananchi kudaiwa malimbikizo ya kodi, tukubali kuwa kupanga ni kuchagua!! Basi yaandikwe mapendekezo ya marekebisho ya sheria ihusuyo ukusanyaji wa kodi unaofanywa na TRA. Hawa TRA wapigwe marufuku kwa mujibu wa sheria KUDAI MALIMBIKIZO YA KODI kwa wafanyabiashara wote, na siyo wa kariakoo tu (sheria ni msumeno), halafu tusikilizie utamu wake!! Vinginevyo itakuwa akidaiwa malimbikizo ya kodi mfanyabiashara aitwaye MUHOGO MCHUNGU halitatoka tamko la kusema TRA wasimdai malimbikizo ya kodi, lakini akidaiwa malimbikizo ya kodi mfanyabiashara aitwaye MUHOGO MTAMU, fasta litatoka tamko la kusema TRA wasimdai malimbikizo ya kodi.
Lingine (AMBALO NDIYO KIINI CHA MAWAZO YANGU), naomba tusiwe tunapotosha au tunatafsiri vibaya kauli na matamko ya Rais wetu mpendwa. Siamini kabisa kuwa Rais ametoa tamko la kuzuia TRA wasidai malimbikizon ya kodi, kama ni hivyo atawezaje kutekeleza mipango ya serikali?. Ila ninaamini kuwa hakubaliani na namna inayotumiwa na TRA kukusanya hayo malimbikizo ya kodi. Hakubaliani na TRA kufunga biashara za watu kwa kisingizio cha malimbikizo ya kodi. Rais anataka TRA na Wafanyabiashara wakae pamoja wazungumze namna rafiki ya kulipa hayo malimbikizo na si kwa kutumia mabavu ya kufunga biashara zao. Biashara zikifungwa serikali itapata wapi mapato yake? Hiyo pesa ya kulipa MISHAHARA MINONO YA TRA ITATOKA WAPI?
Maana haiingii akilini, ninyi TRA mlikuwa wapi hadi mfanyabiashara huyu MUHOGO MTAMU/MUHOGO MCHUNGU akalimbikiza kodi kwa miaka kadhaa? Picha ninayoipata ni kuwa baadhi ya watumishi hawa wa TRA waliridhia mfanyabiashara huyu alimbikize kodi kwa kuwa alikuwa anawapa kitu kidogo (japo inasemekana TRA hupokea kitu kikubwa, ila Polisi ndio hupokea kitu kidogo-sina uhakika na hilo).