Ndizi dawa ya Ukimwi!!

Ndizi dawa ya Ukimwi!!

Kimey

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2009
Posts
4,117
Reaction score
833
VIPIMO vya kimaabara vya wanasayansi nchini Marekani vimebaini kuwa ndizi zina virutubisho maalumu viitwavyo BanLec ambavyo viko sawa na aina mbili za dawa zinazotumika katika kuzuia kuenea kwa virusi vya ukimwi.

Wanasayansi hao wamesema wanaamini virutubisho hivyo vya BanLec ni muhimu na vinaweza kuokoa maisha ya mamilioni ya watu.

Kwa mujibu wa matokeo ya utafiti huo ambayo yameripotiwa katika jarida la Biological Chemistry la Michigan, virutubisho hivyo vinatokana na kemikali ambayo inazalishwa kiasili katika mimea ijulikanayo kama ‘lectin’ ambayo inapambana na magonjwa yanayoikumba mimea.

Watafiti hao wamegundua kuwa lectin iliyo ndani ya ndizi inaweza kukabiliana na madhara ya HIV kwa kuzuia virusi kuingia katika mwili wa binadamu.

BanLec hutumika kama bahasha maalumu ya kuhifadhia protini ambayo hudhibiti kubadilika kwa vinasaba vya vijidudu vya HIV.
Msimamizi mkuu wa jarida la kisayansi kutoka Chuo Kikuu cha Michigan, Michael Swanson alisema: “Tatizo la baadhi ya dawa za kudhibiti HIV ni kuwa zinaweza kuzidiwa nguvu, lakini inakuwa vigumu zaidi zinapokuwa na lectin.
“Lectin hujiunga na sukari inayopatikana katika nukta tofauti za bahasha za HIV-1, na inadhaniwa kuwa inaweza kuwa na nguvu zaidi ya kuzuia virusi kuikaribia.”
Source: Mwananchi
 
VIPIMO vya kimaabara vya wanasayansi nchini Marekani vimebaini kuwa ndizi zina virutubisho maalumu viitwavyo BanLec ambavyo viko sawa na aina mbili za dawa zinazotumika katika kuzuia kuenea kwa virusi vya ukimwi.

Wanasayansi hao wamesema wanaamini virutubisho hivyo vya BanLec ni muhimu na vinaweza kuokoa maisha ya mamilioni ya watu.

Kwa mujibu wa matokeo ya utafiti huo ambayo yameripotiwa katika jarida la Biological Chemistry la Michigan, virutubisho hivyo vinatokana na kemikali ambayo inazalishwa kiasili katika mimea ijulikanayo kama ‘lectin’ ambayo inapambana na magonjwa yanayoikumba mimea.

Watafiti hao wamegundua kuwa lectin iliyo ndani ya ndizi inaweza kukabiliana na madhara ya HIV kwa kuzuia virusi kuingia katika mwili wa binadamu.

BanLec hutumika kama bahasha maalumu ya kuhifadhia protini ambayo hudhibiti kubadilika kwa vinasaba vya vijidudu vya HIV.
Msimamizi mkuu wa jarida la kisayansi kutoka Chuo Kikuu cha Michigan, Michael Swanson alisema: “Tatizo la baadhi ya dawa za kudhibiti HIV ni kuwa zinaweza kuzidiwa nguvu, lakini inakuwa vigumu zaidi zinapokuwa na lectin.
“Lectin hujiunga na sukari inayopatikana katika nukta tofauti za bahasha za HIV-1, na inadhaniwa kuwa inaweza kuwa na nguvu zaidi ya kuzuia virusi kuikaribia.”
Source: Mwananchi
Ajabu hapa Tanzania sehemu ambazo ndizi ndio chakula kikuu ndiko Ukimwi unaongoza,nenda mkoa wa Mbeya na Kagera,huko ndizi ndio menu kubwa lakini gonjwa kwa saaana,hizi tafiti zingine bana ni uchuro mtupu
 
Ajabu hapa Tanzania sehemu ambazo ndizi ndio chakula kikuu ndiko Ukimwi unaongoza,nenda mkoa wa Mbeya na Kagera,huko ndizi ndio menu kubwa lakini gonjwa kwa saaana,hizi tafiti zingine bana ni uchuro mtupu

Hata mimi nashangaa, labda watuelimishe namna ya kuzitumia. pengine inatakiwa ziliwe zikiwa mbichi.
 
Ajabu hapa Tanzania sehemu ambazo ndizi ndio chakula kikuu ndiko Ukimwi unaongoza,nenda mkoa wa Mbeya na Kagera,huko ndizi ndio menu kubwa lakini gonjwa kwa saaana,hizi tafiti zingine bana ni uchuro mtupu
Labda kwa ngozi nyeusi ni Vise-versa!!
 
Ajabu hapa Tanzania sehemu ambazo ndizi ndio chakula kikuu ndiko Ukimwi unaongoza,nenda mkoa wa Mbeya na Kagera,huko ndizi ndio menu kubwa lakini gonjwa kwa saaana,hizi tafiti zingine bana ni uchuro mtupu

Kutokana na utafiti huu kinachozuiwa ni HIV-1, Afrika na hasa Tanzania kuna HIV-1 na HIV-2 na anayeshambulia sana na kumaliza wengi ni HIV-2. Huenda huko Mbeya na Kagera kuna HIV-2 ambaye hazuiliki kwa ndizi
 
Hawa watafiti wasipokua makini kututangazia majaribio yao katika vyakula, watazidisha maambukizi mapya kwani watu watadhani kula ndizi ndio umemaliza ukimwi kumbe unamaliza watu.
Siku zijazo watatwambia mchele, mahindi, ulezi yaani vyakula vinavyoliwa na wengi ndio dawa kumbe siyo dawa. Hatari sana!!!! tafiti hizi.
 
Sishangai matunda mengine wanaiogopa ndizi.
 

Attachments

  • Ndizi.jpg
    Ndizi.jpg
    25.1 KB · Views: 190
ndizi mbivu sio ndizi mbichi au ndizi mbichi zilizopikwa.
sio Plantin, ni banana
 
Ajabu hapa Tanzania sehemu ambazo ndizi ndio chakula kikuu ndiko Ukimwi unaongoza,nenda mkoa wa Mbeya na Kagera,huko ndizi ndio menu kubwa lakini gonjwa kwa saaana,hizi tafiti zingine bana ni uchuro mtupu

na mie nashanga sana, ingekuwa ni kweli basi huko kagera na mbeya wasingeyumbishwa na virus, au ni mpaka zifanyiwe 'modification' kabla ya kuwa kinga/dawa ya ukimwi???
 
Sasa mbona kilimanjaro na kagera ndiko kunapoongoza kwa maambukizi?
 
Back
Top Bottom