Ndoa Hii Inaweza Kuvunjwa??

swali la kizushi hapo..
Umesha test bidhaa ngapi mpaka sasa???????lol

mh...! Hata sikumbuki idadi, mwe! ngoja nianze kukumbuka hisabu yake vizuri, ntarudi kukujibu kwa ufasaha badae.
 
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
atakuwa mnafiki huyo binamu yako, kwani hakumbuki kama alimwambia atakuwa nae kwenye shida na raha? Sasa inakuaje atake kutumia taratibu za kuvunja ndoa? Aache ufala, amvumilie tu mume wake.
Shida nyingine ni ngumu kuzivumilia..
 
...Katavi mi nilitegemea huyo binadamu yako badala ya kukimbilia kutafuta ushauri kwa watu kutaka kuvunja ndoa ningemuona muelewa kama angetafuta ushauri wa jinsi ya kumsaidia huyo mumewe. Kwani ninachofahamu mimi suala la jogoo kutopanda mtungi linatokana na mambo mengi kama vile maradhi (kisukari), stress, uoga kama mtu hajawahi kukutana nae kimwili na huyo mkewe hapo kabla au kweli ni hitilafu aliyozaliwa nayo. So huyo bibie alitakiwa kujua hasa nini kilichosababisha huyo jamaa kushindwa kusimamisha mashine. Sidhani kama kuomba ushauri wa kuvunja ndoa kuwa eti anaogopa kumdhalilisha mumewe wala haina maaana ameshamdhalilisha tayari.
 
inaweza kuvunjwa kama wote wawili mkiafikiana na kanisa likiamuru
 

Mkuu haya ni yale mambo watu wanaoana bila kujua misimamo ya ndoa. Mambo haya yalitakiwa yasuluhishwe ndani kwa ndani wajue chanzo cha tatizo ni nini na msaada gani wanaweza kupeana katika kuhakikisha wanalitibu tatizo kabla ya kurukia kuwaambia watu wa nje. Hizi ni siri za ndani ya chumba ambazo zinatakiwa kubakia kwa muda ndani ya mle kabla ya kuzitoa nje. Kitendo chake cha kukuambia wewe ni kwamba kashamdhalilisha bwana mwenyewe
Maswali ya kujiuliza kabla
Je ni tatizo la kuzaliwa
Je ni wasiwasi wa jamaa
Je ni mara ya kwanz aamefanya hilo jambo
Je ana ugonjwa wowote kama kisukari au magonjwa ya moyo
Je ni periodic au ni paremanent

Je washakaa na huyo mwenza wake wakaongea akamueleza tatizo ni nini
 
Inawezekana kuvunjwa hasa ikijulikana kwamba mwanamme alidanganya makusudi akijua mapungufu yake.Itavunjwa kwa kutumia sheria na hata dini.Ingawa dini proces yake itachukua muda kidogo.
 

Mia kwa mia.
Nimehudhuria semina ya ndoa ya dhehebu hilo hilo lililotajwa na mojawapo ya mambo yanayosababisha ndoa kuwa batili ni kisa hicho. Yaani ikithibitika tu hakuna mjadala. Sio kwamba ndoa inavunjwa bali hiyo ndoa ni batili au kwa maneno mazuri ni kuwa hiyo si ndoa kwa sababu imeshindwa kukidhi takwa kubwa zaidi na la kwanza la kuitwa ndoa.
Yaani ikipelekwa kanisani hiyo kesi haichukui hata wiki, kila mtu kwao!
Yawezekana kabisa jamaa hakuhudhuria semina ya ndoa au kama alihudhuria alikuwa hasikilizi maudhui.

Note:
Lazima ithibitike kuwa hilo tatizo jamaa alikuwa nalo kabla ya kufungwa kwa hiyo ndoa, vinginevyo huyo ndugu yako avumilie tu.
 
Hiyo inavunjwa bila tatizo lolote. Na jamaa si wa kumhurumia ni mbinafsi sana. Kama anajua ana tatizo kubwa kama hilo inakuwaje anaoa kumtia nuksi mwenzie?? Anaoa ili iweje?? Anataka kumtumia mke kuficha kasoro alonayo?? Mimi simhurumii hata kidogo naoan ni the most selfish man kwani binti ndo keshatiwa dosari tena; from now on tayari dada atakuwa na title ya divorcee.
 

N.K punguza ukali...mhurumie jamaa kwani hakupenda iwe hivyo.
Ingekuwa wewe ungefanyaje..!
 
Huyo jamaa alikuwa na tatizo hilo hata kabla ya ndoa, alidanganya!
 
Huyo jamaa alikuwa na tatizo hilo hata kabla ya ndoa, alidanganya!

Basi kesho aende akamwone Padri....kabla ya wiki ijayo haijesha itakuwa tayari yuko huru...unless kama bado anapenda kukaa kwa jamaa.
 
Kwa sheria za kanisa katoliki, INAWEZA kuvunjwa (kubatilishwa). Mojawapo ya mambo yanayoweza kubatilisha ndoa ni kwa mmoja wao kuwa na tatizo la kibayologia, lililothibitishwa kuwa linazuia uwezekano wa kufanyika tendo la ndoa. Pia kama mmoja wao hana uwezo wa kuzaa, na alijua kuwa hana uwezo wa kuzaa, lakini hakumwambia mwenzake kabla ya ndoa, then ndoa hiyo ni batili.

Tatizo linalojitokeza hapo ni sociological impact ya kubatilishwa kwa hiyo ndoa. Inabidi dada awe na busara sana namna ya ku-handle hiyo hali, otherwise anaweza kusababisha matatizo makubwa au hata suicide committing..
 
Kanisa katoliki linao utaratibu wa kutengua ndoa zenye utata mkubwa, na consummation kutokuwapo angalau mara moja mwanzoni ni utata mkubwa.

Amwone Paroko wake kuanzisha huo utaratibu wa kuwa huru.
 

Naunga mkono hoja 100%
 
Hapo hakuna mjadala zaidi ya ndoa kuvunjwa.

Huyo mshikaji alioa ili afanyaje mtoto wa watu? kumpikia ugali?
 
first thing... ana uhakika gani jamaa hawezi kupanda mtungi kabisa? inawezekana jamaa ni mwoga na alikua hajawahi kufanya hayo mambo

kujamiiana kwa mara ya kwanza ni very tricky thing inawezekana jamaa ni mwoga kiasi kwamba jogoo haliwiki

i mean inawezekana ushirikiano kati ya downstairs kwa mshkaji na upstairs haupo when in bed,.... anahitaji usaidizi na sio kuachwa!!!
 
Mi siafiki kitu kama hicho kwani haya mambo yanazungumzika then kama wameshafunga ndo ni ishu ya mazungumzo kati ya mke na mume kwanini nasema ivo ni kwamba mume ili asizalilike na mke asililike mwanamke inabidi awe anatoka nje ya ndoa kukata kiu yake wakati ndoa inaendelea.ila angalizo mwanamke anapokuwa anatoka nje ya ndoa asimweleze uyo mwanaume weaknes za mume wake ili kuweza kujenga heshima ya mume wake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…