Ndoa na Mirathi: Nafasi ya Mahakama ya Kadhi kwa Wanawake

Status
Not open for further replies.
Black Rose, Faiza Foxy,Topical,

..je asiye Muislamu anaruhusiwa kuwa hakimu ktk mahakama ya Kadhi?

..je wanawake wanaruhusiwa kuwa mahakimu ktk mahakama ya Kadhi?
 
Black Rose, Faiza Foxy,Topical,

..je asiye Muislamu anaruhusiwa kuwa hakimu ktk mahakama ya Kadhi?

..je wanawake wanaruhusiwa kuwa mahakimu ktk mahakama ya Kadhi?


Sifa za Kadhi -ni wazi kuwa lazima awe muumini wa imani ya kiislam na awe na ujuzi na uelewa wa kutosha wa SHARIA.

Fikiria kama "kafir" atasimamia masuala ya ibada ya muislam, patatosha?

kuhusu wanawake, nilishalielezea vya kutosha hapo mwanzoni ( sikumbuki post namba ngapi, unaweza kupitia tena previous posts) kwamba Qu'ran iko kimya.Ina maana hakuna katazo.Atakayebisha atuwekee ushahidi hapa.
 
so mahakama za kadhi hazifai?
nini mbadala wake?
 
Black Rose,

..asante kwa majibu yako.

..je, according to QURAN, kuna nafasi yoyote ile ya uongozi ambayo mwanamke hapaswi kushika??
 

Hayo maneno yako tu yanazidi kukuweka mbali na uislam..hahahaha, katonta bana, haya endelea kumwagwa uharo wako! Wewe ndiyo muislamu mwenyewe hakuna kama wewe humu JF

Wewe ni umejiunga juzi JF umeishajua kama Invisible ni Mod..hahahahahah!!!
 
Hayo maneno yako tu yanazidi kukuweka mbali na uislam..hahahaha, katonta bana, haya endelea kumwagwa uharo wako! Wewe ndiyo muislamu mwenyewe hakuna kama wewe humu JF

Wewe ni umejiunga juzi JF umeishajua kama Invisible ni Mod..hahahahahah!!!

Hewala! Mimi maneno yangu yenye staha, yanazidi kuniweka mbali na usilam,ila yako ya matusi ndio yanakuvuta karibu!
Huu ndio upeo wa akili yako nakusamehe.
 
Hewala! Mimi maneno yangu yenye staha, yanazidi kuniweka mbali na usilam,ila yako ya matusi ndio yanakuvuta karibu!
Huu ndio upeo wa akili yako nakusamehe.

BR achana nae huyo mafuriko yanamsumbua...UKWELI UNAUMA.,tupe dawa siye.
 


Bibie, umeeleza vizuri sana niseme nimeona point mbili kwenye hii habari niliyo quote:

1. Kwamba waislamu wahangaike sana na kuwa waadilifu kwanza na wapatikane wengi nafikiri unakosea kusubiri hali hiyo kutokea kwasababu waislamu kama watu wengine wengi wanaweza kupenda dunia kuliko ahera sasa sisi tunaotaka ibada zetu hatuwezi kuwasubiri maana hilo kwa mazingira yaliyopo lina changamoto nyingi..na ujue kuwa mchaMungu ni choice..kwa hoja hiyo ni dhaifu hata kama tuko wachache tupewe haki yetu ya mahakama ya kadhi

2. Umeonyeonyesha uzoefu wa kenya, well sitegemei kwamba mahamaka ya kadhi isiwe na changamoto kokote duniani, zinaweza kuwepo changamoto za weledi, fedha nk. lakini bila kuanza jambo utakaogopa changamoto hadi lini??

Nafikiri hoja ya kuogopa ni mbaya zaidi ni afadhali kuanza na kujifunza na kurekebisha changamoto kila siku kama ilivyo taasisi yeyote ile
 
[/LIST]Duh.. unajua siku hizi mbili umenifanya nifikirie kweli. Maana muda wote ambao tumekuwa tunazungumzia "kadhi" miye mawazoni namuona mbaba fulani akiwa hivyo. Swali ni je, wanawake Waislamu wa Tanzania wanajua wanayo haki ya kuwa kadhi?

Mkuu vipi tena sentesi za namna hii? wewe unadhani wake zetu, dada zetu hawafahamu haki zao kwanini? waislamu wanawake wanajua haki zao kwakuwa haki hizo hazitoki kwa kadhi ila kwenye kitabu kitakatifu (qura'n na sunna)..

Kwahiyo naomba usijidai unawajali sana wake zetu, dada zetu wakati wewe tunafahamu uko upande gani kwenye dini??
 
Black Rose,

..asante kwa majibu yako.

..je, according to QURAN, kuna nafasi yoyote ile ya uongozi ambayo mwanamke hapaswi kushika??

Hili somo ni sensitive.Kuna madhehebu yenye misimamo tofauti kuhusu nafasi zinazoweza kushikwa na wanawake.Pia nchi mbalimbali zimeonyesha mifano kwenye hili.Zipo nchi kama Morocco wao wanatoa mafunzo ya Uimam kwa wanawake, Marekani ina imam wanawake Turkey etc. Kuna nchi nyingine wanawake wanaongoza swala kwa wanawake tu, nyingine wanawake wanaruhusiwa tarawih tu.
Tusubiri wengine akina Topical etc waje kutujuza zaidi.
 

Asante kwa mawazo yako mazuri. Ni kweli unavyosema kuwa wale wachache waadilifu wanajiskia kuhitaji chombo chao waweze kujiskia kamili kwenye masuala ya imani.
Tuendelee kuchambua na kuelimishana.Nadhani hadi sasa kuna wenzetu wanajifunza moja au mawili kutoka kwetu.


Nimependa has point yako niliyoikoleza wino (BOLD) kwamba changamoto zisiogopwe bali zitafutiwe jinsi ya kukabiliana nazo. Kuna wenzetu wao wanadhani hakuna changamoto. Na hata wakajaribu kutoa mfano wa Kenya.Na ndio maana nikaweka mfano huo na changamoto zake.
 

tatizo lako unafikiri Waislamu wako kwenye familia yako au yenu peke yako. Hauwezi kabisa kufikiria labda watu kama miye tuna wadogo zetu walioingia Uislamu au wameolewa na Waislamu! Na tunapozungumzia "Waislamu" tunazungumzia ndugu zetu wenyewe!
 
Mimi si mwelewa sana wa mambo ya Sharia Dada Black Rose lakini nasikia kuwa katika dini hii wanawake wanawekwa nafasi ya chini sana, yaani wanaume wanakuwa favored kuliko wanawake (sijui kama ni kweli) lakini kama ni kweli je haiwezekani kuwa mahkama hii itakuwa ni hatari kwa wanawake hawa?

Natanguliza samahani zangu kwanza pale nitakapokuwa nimewakosea)
 


Hapana mpendwa.Dini yetu ya Islam ni dini ya amani na haki.
Mwanamke katika Uislam, ana haki zake na siyo kama watu wanavyoamini.Hayo mengine ni utamaduni, ustaarabu na hata utashi wa wale wanaomzunguka.Yatosha tu kusema kuwa "uonevu" unaoonekana kutendewa wanawake siyo maagizo au maamrisho ya Kuraan! Ukiisoma hii mada na michango iliyomo utaona tatizo siyo Uislam bali ni watu ndani ya Uislam.
Hawa watu ndio watakuwa kikwazo kwa haki za wanawake kuanzia majumbani hadi watakapofikishana huko kwa Kadhi.
 

Aksante sana dada yangu. Hakika umenielimisha.
 
BR.. inakuwaje

a. Ambapo mwanamke ni Mkristu na mke ni Muislamu na yule Mke anataka kutafuta haki kwa kutumia Kadhi na mume Mkristu hatambui mamlaka ya kadhi?

b. Mwanamme ni Muislamu na mwanamke ni Mkristu na mume anataka mahakama ya kadhi ndio iamue mambo ya ndoa wakati mwanamke anataka Mahakama ya Kanisa iamue (chukulia kesi ya kwanza ndoa ilifungwa Kikristu, na pili ndoa ilifungwa Kiislamu). Huyu mwanamke atalindwa vipi?

c. Watoto ni Wakristu na wazazi Waislamu na hoja ni mirathi. Inakuwa vipi hapo?

Asante.
 
tatizo lako unafikiri Waislamu wako kwenye familia yako au yenu peke yako. Hauwezi kabisa kufikiria labda watu kama miye tuna wadogo zetu walioingia Uislamu au wameolewa na Waislamu! Na tunapozungumzia "Waislamu" tunazungumzia ndugu zetu wenyewe!

Nafikia kwenye hiyo conclusion kwasababu unauliza maswali very "unethical" unaweka shaka kuhusu wake zetu na dada zetu kama vile sisi wanaume ndio tunawalazimisha kuvaa, kuishi kiislam? which is quite wrong..kama unataka kuelewa na sikushinda na kuweka tricks kama kawaida yako tuko pamoja..otherwise sikuamini mkuu ..
 

Mkuu japo hujaniuliza na wengine wanaweza kunisaidia kama wana ufahamu

a +b: Jibu lake ni kuwa ndoa kati ya mke mkiristo na mume muislam kuna school of thought mbili; kuna wale wanaoamini kuwa ndoa hiyo ni halali kwakuwa wanawake wa kikristo na kiyahudi ni halali kwa waislamu kwakuwa wanamuamini Mungu moja; kuna wale wanaosema wanawake wa kikristo si halali kwakuwa wanaamini mungu watatu lakini wakiyahudi ni halali. wanazuoni wanaoendesha mahakama ya kadhi inabidi wakaubaliane kwanza wafuate which school of though in rule accordingly;

C. Naomba nitafute jibu lake
 

Well,

Ndio maana nasema uadilifu wa waislam kama watu (dunia hii ina watu wabaya waislamu na wakristo pia) hautasubiriwa ndipo sisi tunaotaka mahakama ya kadhi tupewe hilo nikutunyima haki yetu mbele ya katiba ya nchi

Pili nimewapa mfano naweza kurudia mfano wangu binafsi; mimi nina wake wawili moja ni mwalimu (graduate) anaendesha miradi ya shule nursery ana pesa zake na mwingine ni officer katika ofisi ya umma anaendesha maisha nami nashughulikia biashara zangu kila moja anaishi kwake nawalisha vizuri tunataka kupata pepo na swala la mirathi ni muhimu..

Nina uhakika wanawake hawa wangependa mali zangu nikifa zigawanywe kwa mujibu wa dini yetu lakini hiyo facility haipo?? wao wenyewe hawawezi kufikia muafaka wa mgawanyo wa mali zangu nikifa hata iweje?? (na katika mazungumzo yetu wanadiriki kusema hatutaki huu mtihani afadhali angekuwepo kadhi mwenye mamlaka (you see what mean)

Ok kuna watu wanasema tumtumie imam lakini hatoshi kwasababu inakuwa kama advice tu kwakuwa hana mamlaka na imam atakubalikaje na wake zangu wote?? ni ngumu sana ku-compromise ili kuondoa zana ya kudhulumiwa???

OK kuna watu watasema wao si wacha mungu kwanini wanahangaika na mali za marehemu guys?? kuna mtu anapenda kudhulumiwa?? dini yetu imekataza kudhulumu na kudhulumiwa hence kwangu mahakama ya kadhi ni muhimu sana..sijui wengine..

Anyway iko siku tutapata
 

wewe uko upande gani? Je ni halali au siyo halali kumuoa au kuolewa na Mkristu?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…