Ndolezo Petro: Kuendelea kuwakamata Viongozi wa NETO ni kuvunja Katiba ya Uhuru wa Kujieleza

Ndolezo Petro: Kuendelea kuwakamata Viongozi wa NETO ni kuvunja Katiba ya Uhuru wa Kujieleza

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Waziri Kivuli wa Sera, Bunge, Vijana, Kazi na Ajira, Ndolezo Petro wa ACT Wazalendo ametoa tamko kuhusu taarifa za kukamatwa kwa kiongozi mwingine wa NETO.

Pia soma ~ Baada ya Mwenyekiti, Katibu wa Jumuiya wa Walimu Wasio Na Ajira (NETO) naye adaiwa kukamatwa na Jeshi La Polisi usiku huu

=========================​

TUJIKUMBUSHE TAARIFA YENYEWE
Umoja wa Walimu Wasio na Ajira Tanzania (NETO) umesema Katibu wa NETO Daniel Edger Mkinga amekamatwa Kibaha Miembe Saba nyumbani kwake majira ya usiku wa saa tatu kasoro kwa tuhuma za kuwepo kwenye Jumuiya ya NETO ambapo waliofika nyumbani kwake kumkamata ni Balozi, Mjumbe na Askari watatu kutoka kituo cha Polisi Maili Moja Kibaha, Pwani.

Taarifa iliyotolewa na Makamu Mwenyekiti wa NETO, Agnesss Mpundi imesema “Tunaomba Wanasheria wenye mapenzi mema na Shirika la Utetezi wa Haki za Binadamu watusaidie kupata uhuru wake, tunaeendelea kuwakumbusha kuwa NETO sio Chama cha kisiasa, genge la Wahalifu wala halina nia yoyote ovu dhidi ya amani ya Nchi yetu, adhima kuu ya NETO ni kuomba ajira za Walimu wa Serikali na kusisitiza kufanyia kazi makala tuliyoiandikia Serikali”

“Kwa Wakazi wa Dar es salam na Pwani kwa ujumla,(Walimu tusiokuwa na ajira) tukutane leo katika kituo cha polisi Kibaha Mail moja kumwona katibu wetu Daniel, aliyekamatwa hapo jana usiku, sisi sio Wahaini, tunataka ajira, ajira ni haki yetu”

Itakumbuka juzi Mwenyekiti wa NETO Joseph Paulo Kaheza alikamatwa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Geita (RCO) kisha akaachiwa kwa dhamana jana ambapo Polisi walisema walimkamata kwa mahojiano kwa kuongoza umoja huo ambao haujasajiliwa.

Chanzo: Millard Ayo
 
Waziri Kivuli wa Sera, Bunge, Vijana, Kazi na Ajira, Ndolezo Petro wa ACT Wazalendo ametoa tamko kuhusu taarifa za kukamatwa kwa kiongozi mwingine wa NETO.

Pia soma ~ Baada ya Mwenyekiti, Katibu wa Jumuiya wa Walimu Wasio Na Ajira (NETO) naye adaiwa kukamatwa na Jeshi La Polisi usiku huu

=========================​

TUJIKUMBUSHE TAARIFA YENYEWE
Umoja wa Walimu Wasio na Ajira Tanzania (NETO) umesema Katibu wa NETO Daniel Edger Mkinga amekamatwa Kibaha Miembe Saba nyumbani kwake majira ya usiku wa saa tatu kasoro kwa tuhuma za kuwepo kwenye Jumuiya ya NETO ambapo waliofika nyumbani kwake kumkamata ni Balozi, Mjumbe na Askari watatu kutoka kituo cha Polisi Maili Moja Kibaha, Pwani.

Taarifa iliyotolewa na Makamu Mwenyekiti wa NETO, Agnesss Mpundi imesema “Tunaomba Wanasheria wenye mapenzi mema na Shirika la Utetezi wa Haki za Binadamu watusaidie kupata uhuru wake, tunaeendelea kuwakumbusha kuwa NETO sio Chama cha kisiasa, genge la Wahalifu wala halina nia yoyote ovu dhidi ya amani ya Nchi yetu, adhima kuu ya NETO ni kuomba ajira za Walimu wa Serikali na kusisitiza kufanyia kazi makala tuliyoiandikia Serikali”

“Kwa Wakazi wa Dar es salam na Pwani kwa ujumla,(Walimu tusiokuwa na ajira) tukutane leo katika kituo cha polisi Kibaha Mail moja kumwona katibu wetu Daniel, aliyekamatwa hapo jana usiku, sisi sio Wahaini, tunataka ajira, ajira ni haki yetu”

Itakumbuka juzi Mwenyekiti wa NETO Joseph Paulo Kaheza alikamatwa na Mkuu wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Mkoa wa Geita (RCO) kisha akaachiwa kwa dhamana jana ambapo Polisi walisema walimkamata kwa mahojiano kwa kuongoza umoja huo ambao haujasajiliwa.

Chanzo: Millard Ayo
Samia yuko madarakani kwa mujibu wa katiba. Cha ajabu ni kwamba serikali anayoiongoza ndiyo inaongoza kuvunja katiba. Inafaa ajiulize kama katiba isingefatwa baada ya kifo cha magufuli leo hii yeye angekuwa raisi? Cdf alisema kuna watu walikuwa hawataki apewe madaraka ila cdf akasema lazima tufate katiba sasa mbona serikali ya sasa inavunja katiba kwa kuminya uhuru wa kujieleza. Waacheni walimu wasio na ajira wajieleze na sio kuwakamata kama wahalifu. Ni vema kuwasikiliza na kuyafanyia kazi madai yao.
 
Um
Samia yuko madarakani kwa mujibu wa katiba. Cha ajabu ni kwamba serikali anayoiongoza ndiyo inaongoza kuvunja katiba. Inafaa ajiulize kama katiba isingefatwa baada ya kifo cha magufuli leo hii yeye angekuwa raisi? Cdf alisema kuna watu walikuwa hawataki apewe madaraka ila cdf akasema lazima tufate katiba sasa mbona serikali ya sasa inavunja katiba kwa kuminya uhuru wa kujieleza. Waacheni walimu wasio na ajira wajieleze na sio kuwakamata kama wahalifu. Ni vema kuwasikiliza na kuyafanyia kazi madai yao.
Umeeleweka
 
Huyo Ndolezi Petro pia sio Raia wa Tanzania kama huyo Mwenyekiti wa NETO

Wote wawili sio raia wa Tanzania
 
Hoja izingatiwe
Taasisi yoyote Tanzania ili ipate uhalali wa kufanya kazi nchini LAZIMA iwe imesajiliwa. Hawa NETO hawajasajiliwa na wanadai wanaongelea Walimu wa Kitanzania. Sio sahihi kisheria.

John Mnyika aliwahi kuanzisha Umoja wa Vijana Tanzania enzi za Mzee Che Nkapa. Ulikuwa ni Umoja ambao ulikuwa haujasajiliwa. Muulize kashkash alozozipata.
 
Kuna wakati mtu anaweza kushindwa kutofautisha kati ya polisi na uvccm!!
 
Back
Top Bottom