NDONDI: Deontay WILDER vs Luis ORTIZ kumaliza ubishi kesho..

screpa

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2015
Posts
10,857
Reaction score
15,866
Kesho alfajiri tutashuhudia pambano kubwa la uzito wa juu kati ya Deontay Wilder 'The Bronze Bomber' na Luis Ortiz 'KingKong', hili ni pambano la marudiano baada ya lile la awali liliyofanyika mapema mwaka jana, ambapo Wilder alishinda kwa KO (kwa tabu sana). Endapo Wilder atashinda ataungana na magwiji wengine kama Muhammad Ali kwakuwa atakuwa ameutetea mkanda wake wa WCB kwa mara ya 10 mfululizo, rekodi za hawa wawili ni kama zinavyoonekana hapo pichani...
 
The baddest man on the Planet [emoji3581], all the best...
 
Ortiz alijitaidi sana pambano la kwanza lakini alikalishwa.namkubali sana Wilder na atanikalishia Tena ortiz
 
Huyu Wilder ana mangumi kombora ambayo huwa yanamfikilisha sana Antony Joshua kuingia nae kwenye pambano.
AJ mtu mwingine mzee hayo maneno na vijembe wanavyotupiana ni mapromoter wanataka watengeneze pesa katika pambano lao liwelamvuto na ndio maana wanakwepana kwepana tu.
 
Kama uliangalia pambano la kwanza. Kuna round wilder alichoka kabisa pona pona yake ilikuwa mwisho wa round
Jana alikua anahojiwa Sky Sports akasema kwenye lile pambano alikua anaumwa yuko hoi kabla hajapanda ulingoni
 
Ortiz anamkalisha aj..huyu Wilder anamuua aj tunabeba maiti tu.ila Ortiz atakalishwa
 
Mzigo [emoji383] wangu naweka kwa Ortiz [emoji123]
Si ajabu Ortiz akashinda, jamaa naye ni mnyama, pambano la kwanza nusura amkalishe Wilder kwa KO, refa ikabidi ambebe amuongezee muda wa kurecover baada ya kengele. Sema Wilder anajua kuusoma mchezo, rematch anaweza kummaliza within three rounds
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…