Ndoto ya kurudi tena masomoni, huwa inamaanisha nini?

Ndoto ya kurudi tena masomoni, huwa inamaanisha nini?

Ukiota mazingira ya shule, upo na ma classmates wa siku nyingi zilizopita, mfano unaota upo katika mazingira ya shule yako ya msingi na upo na wanafunzi mliosoma nao wakati ule pengine imepita miaka mingi inamaanisha kwamba kuna kitu cha kiroho kinachoendelea katika maisha yako kinachohusiana na mambo ya siku zilizopita.

Chunguza maisha yako vizuri unakuta kuna mambo haya yafuatayo:
  • umekuwa ukikwama katika mambo yako kila wakati
  • unaishi nyuma ya wakati wako; yaani ulipaswa kuwa mbali zaidi ya hapo ulipo
  • huridhiki na maendeleo yako pamoja na kuwa na elimu kubwa na ujunzi mzuri
  • ulikuwa unafanya vizuri darasani lakini maendeleo yako sasa hayalingani na kipaji chako
  • umekuwa na ambitions za kitaaluma lakini hujaweza kuzifikia
Kuota ndoto za shuleni mara kwa mara kwaweza kumaanisha kwamba bado hujatenganishwa na wakati uliopita, na umekwamishwa kiroho kuvuka na kwenda kwenye nafasi yako ya ukubwa au mafanikio.

Hivyo basi unapaswa kuchunguza maisha yako. Angalia historia ya familia yako, baba, mama, kaka na dada zako, je nao wapo kwenye hali ya kuchelewa maishani?

Unahitaji kuondolewa hapo ulipokwama kiroho kabla hujachelewa mno. Inategemea imani yako ilivyo lakini haijalishi pia, kwani Mungu huongea kila wakati na kila mtu kwa namna yake ikiwa ni pamoja na kupitia ndoto. Ila tatizo ni kwamba wengi wetu hatutambui kabisa kwamba Mungu amezungumza licha ya kutambua amezungumza nini!

Unahitaji kutoka hapo ulipo kiroho, umekwama au umekwamishwa kiroho. Ulimwengu wa kiroho upo na unafanya kazi kwa ufanisi na usahihi usioelezeka. Tafuta watu ambao kweli ni watumishi wa Mungu Mwenyezi na uwaeleze shida yako nao watakuombea na kukusaidia '"Kutoka" hapo ulipo. Nawe kuanzia sasa anza kuzungumza na Mungu kama unavyozungumza na yule unayemheshimu sana, mwambie kila kitu, kila shida yako na mwombe specifically unachotaka akufanyie ukitaja tatizo lako barabara na kumwambia unataka afanye nini hasa. Fanya hivyo bila kuchoka ama kuona aibu kila wakati. Fuatilia matokeo yake na pia andika uombacho na tarehe, fuatilia maombi yako kwa imani, Mungu si mwanadamu ili asahau au ashindwe kukujibu, atakujibu tu, kuwa mwangalifu akizungumza umsikie kwani ndipo tatizo kubwa la mwanadamu; wengi hawasikii Mungu anapozungumza! Atazungumza na kukujibu kila kitu, fuatilia kwa uangalifu mkubwa, Mungu ni mwaminifu mno na hujibu kila ombi!

Kama una maswali zaidi nitakusaidia zaidi, tuwasiliane. Nimekuwa katika hali kama hii naifahamu vizuri na ninaendelea kutoka kwa kasi kubwa kila siku.
Spiritual world controls the physical world
 
Hata mimi iliwahi nitokea ndoto kama hiyo, eti niko napambana kumaliza pepa na dakika zinakaribia kuisha, halafu maswali ndio kwanza nimejibu mawili kati ya 50, hafu wenzangu washamaliza wanakusanya, yaani huwa inatesa ndoto ya namna hiyo, acheni tu.
 
Nimekua na teswa mara kwa mara na ndoto kama yako mkuu.. Na mara nyingine nipo kabisa kwenye chumba cha mtian ila sijasoma chochote.. Mwenye ujuzi wa maswala ya ndoto atusaidie
Hyo ndoto ata mim niliota hvyo ila nilikuja kuambiwa na nabii flni kuwaa kuna maswala yangu hayako poa kuna watu wanakurudisha nyuma awataki wew uende mbelee kemee sanaaa
 
Kama umeota uko shule ya msingi Jaribu kukumbuka ni somo gani Au mtihani gani Au ni suala Au mazingira gani Au watu gani ulikua nao kwenye ndoto . LAZIMA ktk hiyo ndoto kimoja wapo kitakuwepo. Hayo mazingira ndio yanajawabu kwa kile unachokipitia sasa ktk maisha Iwe ndoa, biashara Au kazi etc. MAANA YAKE KUNA MATATIZO YA FIKRA AU MTIZAMO AU UMEKOSA MSINGI MZURI WA KUFANYA HILO JAMBO.
 
Hii ndoto wengi inatusumbua, wakati mwingine napata hofu kwamba nasubiri mtihani, kumbe nishamaliza
 
Mimi niliishia form four sikuwah kusoma A level ila naota Mara Kwa mara nipo darasani ila form five au nipo kwenye chumba cha mtihani wa kumaliza kidato cha sita na katika shule ile ile niliyokuwa nasoma.
 
Mimi niliishia form four sikuwah kusoma A level ila naota Mara Kwa mara nipo darasani ila form five au nipo kwenye chumba cha mtihani wa kumaliza kidato cha sita na katika shule ile ile niliyokuwa nasoma.
Nyota yako imeibwa inatumika mahala angalia maisha yako hayaeleweki
 
Ukiota mazingira ya shule, upo na ma classmates wa siku nyingi zilizopita, mfano unaota upo katika mazingira ya shule yako ya msingi na upo na wanafunzi mliosoma nao wakati ule pengine imepita miaka mingi inamaanisha kwamba kuna kitu cha kiroho kinachoendelea katika maisha yako kinachohusiana na mambo ya siku zilizopita.

Chunguza maisha yako vizuri unakuta kuna mambo haya yafuatayo:
  • umekuwa ukikwama katika mambo yako kila wakati
  • unaishi nyuma ya wakati wako; yaani ulipaswa kuwa mbali zaidi ya hapo ulipo
  • huridhiki na maendeleo yako pamoja na kuwa na elimu kubwa na ujunzi mzuri
  • ulikuwa unafanya vizuri darasani lakini maendeleo yako sasa hayalingani na kipaji chako
  • umekuwa na ambitions za kitaaluma lakini hujaweza kuzifikia
Kuota ndoto za shuleni mara kwa mara kwaweza kumaanisha kwamba bado hujatenganishwa na wakati uliopita, na umekwamishwa kiroho kuvuka na kwenda kwenye nafasi yako ya ukubwa au mafanikio.

Hivyo basi unapaswa kuchunguza maisha yako. Angalia historia ya familia yako, baba, mama, kaka na dada zako, je nao wapo kwenye hali ya kuchelewa maishani?

Unahitaji kuondolewa hapo ulipokwama kiroho kabla hujachelewa mno. Inategemea imani yako ilivyo lakini haijalishi pia, kwani Mungu huongea kila wakati na kila mtu kwa namna yake ikiwa ni pamoja na kupitia ndoto. Ila tatizo ni kwamba wengi wetu hatutambui kabisa kwamba Mungu amezungumza licha ya kutambua amezungumza nini!

Unahitaji kutoka hapo ulipo kiroho, umekwama au umekwamishwa kiroho. Ulimwengu wa kiroho upo na unafanya kazi kwa ufanisi na usahihi usioelezeka. Tafuta watu ambao kweli ni watumishi wa Mungu Mwenyezi na uwaeleze shida yako nao watakuombea na kukusaidia '"Kutoka" hapo ulipo. Nawe kuanzia sasa anza kuzungumza na Mungu kama unavyozungumza na yule unayemheshimu sana, mwambie kila kitu, kila shida yako na mwombe specifically unachotaka akufanyie ukitaja tatizo lako barabara na kumwambia unataka afanye nini hasa. Fanya hivyo bila kuchoka ama kuona aibu kila wakati. Fuatilia matokeo yake na pia andika uombacho na tarehe, fuatilia maombi yako kwa imani, Mungu si mwanadamu ili asahau au ashindwe kukujibu, atakujibu tu, kuwa mwangalifu akizungumza umsikie kwani ndipo tatizo kubwa la mwanadamu; wengi hawasikii Mungu anapozungumza! Atazungumza na kukujibu kila kitu, fuatilia kwa uangalifu mkubwa, Mungu ni mwaminifu mno na hujibu kila ombi!

Kama una maswali zaidi nitakusaidia zaidi, tuwasiliane. Nimekuwa katika hali kama hii naifahamu vizuri na ninaendelea kutoka kwa kasi kubwa kila siku.
Ubarikiwe kwa andiko zuri
 
Hebu chukulia imepita miaka takribani 15 au 20 kabisa toka uhitimu masomo ya ngazi flani mfano: elimu ya sekondari au chuo

Lakini ghafla siku za karibuni unaota ndoto umerudi tena masomoni tena sio kwa kuanza upya ni katikati ya muhula wanafunzi wenzako wakiwa tayari wamesoma topiki nyingi kuliko wewe na mmebakiza mwezi mmoja kwa ajili ya kufanya mtihani wa mwisho

Nielewesheni ndoto kama hii huwa ina maana gani katika maisha yako halisi

Kuota unafanya Mtihani.

Hii ni moja ya ndoto ambayo inaotwa na watu wengi sana, na hii huwa inachukua maumbile tofauti tofauti, wengine utakuta wanaota wanafanya mitihani na hawajajiandaa, wanachoshtukia tu ni wakati wa mtihani umefika, hakuna chochote walichofanya wanajiuliza siku zote alikuwa wapi…wengine wanaota wanafanya mtihani mgumu sana lakini wenzake wanaonekana wanafahamu cha kujaza yeye hajui, wengine wanaota kama walikatisha masomo wakaondoka, baadaye aliporudi muda umeshapita mitihani ya mwisho imekaribia, wengine wanaota wamerudi madarasa ya nyuma ambayo tayari wameshayavuka siku nyingi na ni lazima wayavuke ili waendelee na madarasa ya mbele, wengine wanaota wapo wanafundishwa, wengine wanapewa adhabu n.k.…


Na ndoto hizi huwa zinatesa sana, zinaweza kujirudia hata kila baada ya wiki au mwezi, au miezi kadhaa, inategemea na mtu na mtu, lakini ni ndoto ambazo haziachi kuja.


Biblia inasema..Ayubu 33:14 “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;”

Mungu sikuzote huwa anapenda kutumia vitu vinavyotuzunguka kutufukishia sisi ujumbe fulani au kutufundisha, na ndio maana utaona Bwana Yesu alipokuwa anafundisha mifano yake yote alikuwa anatumia mambo ya kawaida tu yanatozunguka sikuzote ili kutufikishia sisi ujumbe na tuulewe utaona wakati mwingine alitumia mifano ya ndege, wanafanyabiashara, wafalme, harusi n.k…Hivyo na Mungu ili kukufikisha ujumbe wako wa wokovu huwa anapenda kutumia mfano wa kitu ambacho kimetukuka sana mbele yako, kitu chenye maana sana kwako ambacho ukikisoma anajua kabisa umekosa maisha na hicho si kingine zaidi ya ELIMU.


Kufunua kuwa Ipo elimu iliyokuu ambayo inafungua ufunguo sio tu wa maisha ya hapa bali pia wa maisha ya ulimwengu unaokuja, na hiyo si nyingine zaidi ya Elimu ya Ufalme wa Mbinguni..Mungu anakuonyesha hali yako ya kiroho ilivyo kupitia maisha yako ya shuleni, kama unavyojiona upo shuleni hujajiandaa, au mtihani ni mgumu basi katika roho ndivyo hivyo ulivyo.. kuwa upo nyuma, na unapaswa ushinde, yapo madarasa haujayavuka bado, upo pale pale kiroho umekwama, unatamani uendelee mbele unashindwa au unaona ni ngumu kwasababu bado hujayamaliza madarasa ya nyuma Mungu aliyokupa.


Hivyo unapaswa uongeze bidii yako kwa Mungu, ili ufike pale Mungu anapotaka kufika, ongeza kiwango chako cha maombi, jifunze Neno la Mungu sana, ishi maisha yanayompendeza Mungu, punguza muda wa kuihangaikia dunia, na ongeza muda wako wa kumtafuta Mungu, kwasababu yeye ndio ufunguo wa kweli wa maisha yako ndugu. Ukimpata Mungu umepata vyote.


Mathayo 6:33 “Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.”

Hivyo ukiwa na bidii na Mungu akaridhika na wewe basi atakuvusha na kukupeleka katika kiwango kingine cha kiroho na kiufahamu. Kumbuka Mungu anakupenda na ndio maana anakuonyesha ndoto kama hizo, Hivyo usipuuzie ungeza bidii yako kwake.


Ubarikiwe.

 
Inamaanisha ulipo sio pazuri kimaisha. Yaani ni kama bado upo kipindi unasoma
Bado hujafikia ulivyotakuwa kuwa kwenye level inayotakiwa kuwa. Pambana bado haujachelewa kuwa katika level unayotakiwa kuwepo.
 
Inamaanisha ulipo sio pazuri kimaisha. Yaani ni kama bado upo kipindi unasoma
Bado hujafikia ulivyotakuwa kuwa kwenye level inayotakiwa kuwa. Pambana bado haujachelewa kuwa katika level unayotakiwa kuwepo.
hivi huwa mnajuaje hizi tafsiri
 
Unafanya kazi kwa juhudi zaidi kuliko maarifa....jitahidi kusoma kuongeza weredi katika kazi zako ili upate mafanikio.
 
Hebu chukulia imepita miaka takribani 15 au 20 kabisa toka uhitimu masomo ya ngazi flani mfano: elimu ya sekondari au chuo

Lakini ghafla siku za karibuni unaota ndoto umerudi tena masomoni tena sio kwa kuanza upya ni katikati ya muhula wanafunzi wenzako wakiwa tayari wamesoma topiki nyingi kuliko wewe na mmebakiza mwezi mmoja kwa ajili ya kufanya mtihani wa mwisho

Nielewesheni ndoto kama hii huwa ina maana gani katika maisha yako halisi
Mm nshawai sikia huwa ina maana kua Kuna mahali uliachwa na wenzio wa Rika lako hasa maendeleo yaan Kuna sehem ulkwama inatakiw ufanyie kaz
 
Hebu chukulia imepita miaka takribani 15 au 20 kabisa toka uhitimu masomo ya ngazi flani mfano: elimu ya sekondari au chuo

Lakini ghafla siku za karibuni unaota ndoto umerudi tena masomoni tena sio kwa kuanza upya ni katikati ya muhula wanafunzi wenzako wakiwa tayari wamesoma topiki nyingi kuliko wewe na mmebakiza mwezi mmoja kwa ajili ya kufanya mtihani wa mwisho

Nielewesheni ndoto kama hii huwa ina maana gani katika maisha yako halisi
Wenzio tuna miaka 40 na usheee na bado tunaota tunaenda darasani bila viatu, tunaenda choo kimejaa vinyesi, tunaota hakuna wa kutuonglesha. Hii inanitokea kila mara mpaka nimezoea. Si shwari inauma ila nimempata mwenzangu anayeteseka kama mimi. nilimaliza 0 level 1976 lakini mpaka leo naandamwa. Kuna somo nilidhani nilipta sana nikalifail lakini kwenye ndoto naonyeshwa mwalimu wangu alivyolibadili kumpa mtu. Nina maisha mazuri sana ila siwezi sahau na ndoto huwa inanirudia kunionesha kilichotokea.
 
Ukiota mazingira ya shule, upo na ma classmates wa siku nyingi zilizopita, mfano unaota upo katika mazingira ya shule yako ya msingi na upo na wanafunzi mliosoma nao wakati ule pengine imepita miaka mingi inamaanisha kwamba kuna kitu cha kiroho kinachoendelea katika maisha yako kinachohusiana na mambo ya siku zilizopita.

Chunguza maisha yako vizuri unakuta kuna mambo haya yafuatayo:
  • umekuwa ukikwama katika mambo yako kila wakati
  • unaishi nyuma ya wakati wako; yaani ulipaswa kuwa mbali zaidi ya hapo ulipo
  • huridhiki na maendeleo yako pamoja na kuwa na elimu kubwa na ujunzi mzuri
  • ulikuwa unafanya vizuri darasani lakini maendeleo yako sasa hayalingani na kipaji chako
  • umekuwa na ambitions za kitaaluma lakini hujaweza kuzifikia
Kuota ndoto za shuleni mara kwa mara kwaweza kumaanisha kwamba bado hujatenganishwa na wakati uliopita, na umekwamishwa kiroho kuvuka na kwenda kwenye nafasi yako ya ukubwa au mafanikio.

Hivyo basi unapaswa kuchunguza maisha yako. Angalia historia ya familia yako, baba, mama, kaka na dada zako, je nao wapo kwenye hali ya kuchelewa maishani?

Unahitaji kuondolewa hapo ulipokwama kiroho kabla hujachelewa mno. Inategemea imani yako ilivyo lakini haijalishi pia, kwani Mungu huongea kila wakati na kila mtu kwa namna yake ikiwa ni pamoja na kupitia ndoto. Ila tatizo ni kwamba wengi wetu hatutambui kabisa kwamba Mungu amezungumza licha ya kutambua amezungumza nini!

Unahitaji kutoka hapo ulipo kiroho, umekwama au umekwamishwa kiroho. Ulimwengu wa kiroho upo na unafanya kazi kwa ufanisi na usahihi usioelezeka. Tafuta watu ambao kweli ni watumishi wa Mungu Mwenyezi na uwaeleze shida yako nao watakuombea na kukusaidia '"Kutoka" hapo ulipo. Nawe kuanzia sasa anza kuzungumza na Mungu kama unavyozungumza na yule unayemheshimu sana, mwambie kila kitu, kila shida yako na mwombe specifically unachotaka akufanyie ukitaja tatizo lako barabara na kumwambia unataka afanye nini hasa. Fanya hivyo bila kuchoka ama kuona aibu kila wakati. Fuatilia matokeo yake na pia andika uombacho na tarehe, fuatilia maombi yako kwa imani, Mungu si mwanadamu ili asahau au ashindwe kukujibu, atakujibu tu, kuwa mwangalifu akizungumza umsikie kwani ndipo tatizo kubwa la mwanadamu; wengi hawasikii Mungu anapozungumza! Atazungumza na kukujibu kila kitu, fuatilia kwa uangalifu mkubwa, Mungu ni mwaminifu mno na hujibu kila ombi!

Kama una maswali zaidi nitakusaidia zaidi, tuwasiliane. Nimekuwa katika hali kama hii naifahamu vizuri na ninaendelea kutoka kwa kasi kubwa kila siku.
acha ushirikina mkuu ,ndoto ni mindset tu wengi humu kipindi kirefu cha maisha yetu tangu utotoni tumetumia shuleni hivyo hizo moments mara nyingi hujirudia hasa kile kipindi cha mateso cha mitihani .walokole na waganga wanadanganya sana watu ili wapige pesa
 
Umetekwa kwa namna fulani fanya haraka sana kutoka hapo, watu wanafaidika na wewe, msukule sio lazima atoweke wengi wanaishi na ni watu wa kawaida sana ila hawajui kinachoendelea nyuma ya pazia, wahi ndugu!
sijui imani za kujinga kama hizi zitaishi lini kwenye jamii zetu
 
ndoto ni memory tu kwenye ubongo hakuna lolote,wengi wanaoota hivyo ni wale ambao muda wao mwingi waliutumia shuleni na moments za mitihani na masomo zilikua zinaumiza sana akili ,hiyo memory sio rahisi kutoka akili ni sawa na kumuota mtu aliyefariki kitambo na ulikua unampenda kumuona amerudi upo nae.walokole na waganga hutumia hii fursa kudanganya watu ila kiukweli hakuna lolote
 
Back
Top Bottom