Ndubu ni samaki wa ajabu anayepatikana Ziwa Tanganyika

Kigoma Region Tanzania

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2021
Posts
230
Reaction score
611
Samaki huyo mwenye mpomo au Komwe jina lake anaitwa NDUBU, ni samaki mwenye kuvutia kwa macho anapendeza mno akiwa kwenye maji. Samaki huyu ni moja ya kivutio cha watalii katika ziwa letu Tanganyika.

Hutumika kama samaki wa kuliwa ni mtamu sana na mwenye ladha nzuri na pia hutumika kama samaki wa mapambo (aquarium) akiwa kwenye maji humeremeta.

NDUBU hupatikana ziwa Tanganyika wilaya ya Uvinza maeneo ya Kalya, Sibwesa na Buhingu ndiko hupatikana kwa wingi samaki wa mapambo.

Kama ilipendekezwa watoto wa Shule ya msingi wavae Socks za pundamilia Ilikuwa ni kwasababu ya kiashirio cha wanyama hao wafahamike, hivyo basi hakuna budi tuseme socks za pundamilia pia ni Kiwakilishi kizuri cha samaki wetu huyu mtamu. MR NDUBU

Kitaalamu anafahamika kama ''Cyphotilapia frontosa'' kigoma f1 (First Filial), Wapo Jinsia ya kiume na jinsia ya kike.

Utajiri wa ziwa Tanganyika.
Ndubu ni huyu samaki mwenye mistari na komwe


MR NDUBU


MR NDUBU
 
Anafanana na wanachama wa cha chama fulani cha siasa
 
Masudi Kipanya Mungu anakuona.

Kwa waCuba tu wataelewa🤣
 
Nilifanya sport fishing Buhingu hadi Kalilani samaki ni wengi mono Jamii ya Sangara
 
Nilifanya sport fishing Buhingu hadi Kalilani samaki ni wengi mono Jamii ya Sangara

Ziwa Tanganyika ndiko walitolewa sangara wakaenda kupandikizwa ziwa victoria, sema sangara kule haeleweki sana kama mgebuka, kitoga na ningu, lakini kuna sangara wengi na wakubwa lile ziwa haijapata kutokea
 
Safi sana unaitangaza kigoma

Mtu kwao bwana

Ova
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…