Ndugai: Lishe duni ya wachezaji wetu imechangia Taifa Stars kufungwa

Ndugai: Lishe duni ya wachezaji wetu imechangia Taifa Stars kufungwa

Amegundua Hili baada ya kufungwa?
Salam zimefika. Nadhani Ndgu mwakyembe ajiangalie. Ule ushauri wa kutaka kupunguza wachezaji wa kigeni kwenye vilabu kwa kutegemea hawa waketu! Hata zile nafasi 4 za uwakilishi caf tutapoteza hivi karibunitu.
 
Alifanya Press hapo airport au!?
 
Mbona walikuwa wanashindwa kuwanyanganya mpira wachezaji wa Senegal kitaalam wanasema one to one battle Wachezaji wetu wialionekana dhahiri kushindwa

..I did not see it that way.

..Nitaangalia mchezo tena ili kujiridhisha.

..Ila nimeona Tz tuli-commit fouls nyingi kuliko wapinzani wetu. Hiyo inaonyesha kuwa sisi ndiyo tulikuwa na mabavu/ maguvu kuliko Senegal.

..Nadhani tunahitaji KIUNGO MCHEZESHAJI mzuri zaidi. Wasenegali walituzidi kwenye upande wa ball possesion and shots attempted. Hiyo ina maana kuwa hatuna kiungo/viuongo wa kumiliki na kusambaza mpira kwa washambuliaji.
Cc ChoiceVariable , severinembena
 
Mambo ya udumavu unaosababishwa na lishe duni upo lakini pia ni species za kitanzania,waganda wana Vimo vya average ya John Boko lakini waliwamudu wakongo wenye miili dizaini ya Senegal urefu na unene
Ko sio sahihi moja kwa moja kusema hiyo ndio sababu,kwa mpira gani tuliocheza hadi hiyo iwe sababu? Species za West/Central and North Africa ni giants kuliko east Africa anbapo wengi ni moderate,wasukuma ni jamii ya west africa
Lishe tu hakuna u giants hapo
Mfano mNigeria chakula anachokula kwa mlo mmoja ni mlo wa siku nzima kwa mtz
 
Mwakyembe na Shonza hakuna mahali wamewahi cheza mpira au mchezo wowote leo hii ndio wamepewa wizara unategemea nini
Kama hao mawaziri ni wabovu ni wabovu tu haihusiani na kucheza mpira hata wangecheza ndiyo vilevile tu
 
Dar es Salaam. Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amesema miongoni mwa sababu iliyochangia Stars kupoteza mchezo wa kwanza jana dhidi ya Senegal ni lishe duni ya wachezaji wetu.

Spika Ndugai ameyasema hayo muda mfupi baada ya kuwasili Dar es Salaam akitokea Misri aliposhuhudia mchezo wa kwanza wa Kombe la Mataifa ya Afrika kati ya Senegal na Tanzania uliomalizika kwa Taifa Stars kuchapwa 2-0.

Ndugai alisema ukiangalia kwa umakini utaona wale wachezaji wa timu pinzani walikuwa na miili mizuri ambayo inatokana na lishe nzuri.

"Kuna umuhimu wa kuwapa wachezaji wetu lishe nzuri ya kutosha ili kushindana na wapinzani wa aina ya Senegal," alisema Ndugai.

Katika hatua nyingine Ndugai alisema viongozi wengi wa soka na michezo mingine hapa nchini siyo watu sahihi wa kuongoza.

Source : Mwananchi
Ahaaaa Ndugai kweli walifungwa kwa ajili ya lishe tu? Kocha Amunike hakuliona hilo la lishe?Watanzania kwa sababu utawajua tu.
 
Lishe tu hakuna u giants hapo
Mfano mNigeria chakula anachokula kwa mlo mmoja ni mlo wa siku nzima kwa mtz

Hivi mtu ukiwa tu CCM ndo akili zinakuwa boga kabisa...!?

Na mnakubaliana na kauli hiyo ya Speaker!??
 
Hivi mtu ukiwa tu CCM ndo akili zinakuwa boga kabisa...!?

Na mnakubaliana na kauli hiyo ya Speaker!??
Nilichikiandika hapa hakiusiani na ccm na wala sijawahi kuielewa ccm katika maisha yangu
 
East Africa Tanzania ndio kwenye udumavu mkuu, Kenya na Uganda asili yao ni miili mikubwa kwa maana ya vimo na maumbile..tuangalie aina lishe zetu tukiwa watoto na kipindi cha ujauzito wa wake zetu..

Special research inahitajika hapa ili kujenga generation ya watu wenye akili, nguvu, kujisimamia na kujielewa - tunakwama hapa.

Mkuu kama kimo ni kigezo basi Messi au Maradona wasingekuwa wachezaji nyota.
 
Mambo ya udumavu unaosababishwa na lishe duni upo lakini pia ni species za kitanzania,waganda wana Vimo vya average ya John Boko lakini waliwamudu wakongo wenye miili dizaini ya Senegal urefu na unene
Ko sio sahihi moja kwa moja kusema hiyo ndio sababu,kwa mpira gani tuliocheza hadi hiyo iwe sababu? Species za West/Central and North Africa ni giants kuliko east Africa anbapo wengi ni moderate,wasukuma ni jamii ya west africa
udumavu kwa watoto wa tz kwa sasa ni 40%...tatizo lipo kwenye mlo kamili tangu utotono,huko nyuma kula haikua shida,mtazame pondamali,tenga,ken mkapa na wa vizazi hivyo...ngasa hata umlishe vp hawezi kua,spika kaonesha namna gani lishe imempiga chenga
 
..I did not see it that way.

..Nitaangalia mchezo tena ili kujiridhisha.

..Ila nimeona Tz tuli-commit fouls nyingi kuliko wapinzani wetu. Hiyo inaonyesha kuwa sisi ndiyo tulikuwa na mabavu/ maguvu kuliko Senegal.

..Nadhani tunahitaji KIUNGO MCHEZESHAJI mzuri zaidi. Wasenegali walituzidi kwenye upande wa ball possesion and shots attempted. Hiyo ina maana kuwa hatuna kiungo/viuongo wa kumiliki na kusambaza mpira kwa washambuliaji.
Cc ChoiceVariable , severinembena
zilikua faulo za kukwatua visigino
 
Basi usisapoti hiyo kauli ya kijinga ya radio mbao...
Ndugai sio mtu anayefaa kuwa kiongozi lakini ukiwa mtu wa kupinga kila kitu wewe utakuwa mwendawazimu hauko sawa

Mbali na kuongea Ndugai Mimi mwenyewe nalifahamu hilo nime confirm tu kwamba yuko sahihi
 
Hivi Warundi wana miilli mikubwa? Mbona ni wadogo tu kama sisi lkn wanacheza mpira mzuri kuliko sisi?

Nachojua soka sio mieleka wala masumbwi, ndio maana hakuna kupimwa uzito, soka ni akili na ufundi, maguvu ni nyongeza tu.

Vv
 
udumavu kwa watoto wa tz kwa sasa ni 40%...tatizo lipo kwenye mlo kamili tangu utotono,huko nyuma kula haikua shida,mtazame pondamali,tenga,ken mkapa na wa vizazi hivyo...ngasa hata umlishe vp hawezi kua,spika kaonesha namna gani lishe imempiga chenga

Inaonekana kuna kujichanganya kati ya lishe na kimo. Wengi kwenye huu uzi huenda na spika wanaonyesha lishe ni urefu na unene. Kama hiyo ndio ndio mantiki ya wengi basi Messi asingecheza mpira kabisa. Ni vyema ikawekwa wazi, tatizo ni lishe au kimo cha mtu mmoja mmoja?
 
Inaonekana kuna kujichanganya kati ya lishe na kimo. Wengi kwenye huu uzi huenda na spika wanaonyesha lishe ni urefu na unene. Kama hiyo ndio ndio mantiki ya wengi basi Messi asingecheza mpira kabisa. Ni vyema ikawekwa wazi, tatizo ni lishe au kimo cha mtu mmoja mmoja?
havitengani hivyo vitu,vimo vya watanzania vimepungua sana kizazi hiki kisa mlo kamili ni tabu,nafasi anayocheza messi kimo si hitaji muhimu,plus messi si mchezaji wa kawaida
 
Ha ha ha kuna ukweli hapo ndugu
Upi huo? Tulizidiwa maarifa na uzoefu au afya? Hata kama hawajapenda matokeo kujiokoteza sababu ilmradi waiponde team yetu haikubaliki!

Hivi kabisa serious mtu amewaza akapata hii ndio sababu? Na wewe unaunga mkono?

Tuna safari ndefu sana. Na labda wajukuu watafika kwa mtindo huu!
 
Midfielder bora Roberto Carlos,Gatuso,Paul Scholes na mpaka sasa Kante anakimbiza Premier league, bila ya kuwasahau wataalamu wa wataalamu Maradona na Messi, mpira ni kipaji si umbile. Huyu jamaa anakipaji cha kuwanyanyasa wapinzani bungeni aendelee na kipaji chake mambo ya soka aachane nayo.
 
Angekuwa anatoa posho yake ili wakale vizuri
 
Back
Top Bottom