Ndugu hakopesheki

Mtetezi.com

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
3,134
Reaction score
3,584
Ndugu akikuazima hela kama unayo mpe tu but mwambie nimekukopesha ili asipokulipa next time ashindwe kukukopa tena.
Na kama hela unakazi nayo ndani ya mda mfupi ujao mwambie tu Dada/kaka hali ngumu sina japo hawaaminigi kuwa wengine wanakosa.

NB
Ili uendeleze mahusiano na ndg yako ni bora tu utoe kama msaada/support na si kama mkopo wa mwisho wa mwezi nitalipa mwisho wa siku mtakuwa hamwelewani.
 
Hii ni kweli. Kuna shangazi yangu namdai laki moja mpaka leo kulipa hataki.
 
Sio ndugu tu hata rafiki ukitaka kugombana nae mkopeshe

Mm nikishamkopesha rafiki najisemea tu anilipe sawa asinilipe sawa
We acha tu dada yangu yani hapa nikipiga mahesabu ya watu ninaowadai naweza hata jenga kakibanda mjini lakini sijui napataga waoi roho hiyo mana kuna wakati nasema
It's enough now sikopeshi tena but anakuja mtu analia shida unamhurumia unamkopesha unarushwa.
 
Unamkopesha mtu kwa roho moja tu mwisho wa siku anakununia ghafla tu anajishtukia tu sababu anadaiwa
 
Kama hela ipo mpe tu. Akirudisha poa asiporudisha poa tu. Maisha yanasonga ina siku huwezi kujua yeye atakusaidiaje.

Maana unaweza kumkazia leo alafu kesho na kesho kutwa ukapigika ukakosa pakukimbilia.
 
Kweli kabisa
Watu wengi huwa wanajisahaulisha hilo jambo. Ndio maana unaweza kuta mtu anataabika hana hata mia na hana msaada unajiuliza huyu hana hata ndugu?

Kumbe ndio wale wale walijaliwa wakawaona ndugu maboya, upepo umebadilika ndio wanaanza kuanya anya.
 
Watu wengi huwa wanajisahaulisha hilo jambo. Ndio maana unaweza kuta mtu anataabika hana hata mia na hana msaada unajiuliza huyu hana hata ndugu?

Kumbe ndio wale wale walijaliwa wakawaona ndugu maboya, upepo umebadilika ndio wanaanza kuanya anya.
Dizaini hii wapo wengi sana
 
Mtu yeyote akija na shida ya kutaka kukopa ukampa na hajarudisha basi unamwachia Mungu tu,shida hazinaga mwisho

Sasa kila anayekuja ukifanya hivyo si utafilisika mkuu ndg anakuja anasema nyumba yake bado mwez bank ipige mnada unamwonea huruma hasahasa watoto wake unamkombolea sasa wakija kama hao kumi si unarudi kijijini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…