Ndugu Mtanzania: Je unajua hili?

Ndugu Mtanzania: Je unajua hili?

Maamuzi ya mtu, vitu anavyofanya, vitu anavyotoa, mchango wake kwa jamii, mazuri na mabaya yake yote tunayoyaona... yote ni matokeo ya uwezo wake wa kufikiri.

Na pia, uwezo wa kufikiri wa mtu, maamuzi yake na vitu vingine vyote unavyoweza kuviita "maamuzi yake" vinategemeana na nini "ANACHOKIJUA" kichwani mwake.

Kujua ni kuelemika, na ndio msingi wa maamuzi yetu na mchango katika jamii yetu. Elimu ni uwezo wa kuona - na ndio kujua kwenyewe huko! Je, kwani hakuna tofauti kati ya mwenye macho na kipofu katika giza totoro?

Hata kama tupo katika giza nene lisilopenyeka, bado mwenye macho ni zaidi ya kipofu, ingawa sote hatuoni mbele!

Na ndivyo ilivyo katika kujua. Hata kama kujua hakutubadilishi, bado kujua ni bora kuliko kutojua kabisa!

Mimi nafurahia kujua .... waache watu wajue!
 
Re: Ndugu Mtanzania: Je unajua hili?
Nafikili sasa viongozi wa serikali yetu wanatupeleka kuzimu kwa tamaa zao.Hivi kweli waziri ambaye ni daktari kwa taaruma anataka kununua bajaji kwa ajili ya kubeba wagonjwa! Hao wagonjwa wamekuwa magunia ya mihogo?
 
Kweli Nyerere alifanya kazi kubwa, kwani lazima utumie neno NDUGU? Misingi ya Ujamaa inaonekana haiwezi kutoka kwa Watanzania.

Halafu bado watu wanamtukana Mwalimu Nyerere! Kaazi kweli kweli NDUGUZANGUNI!!
 
Mwanakijiji,wahenga walisema 'usilolijua ni usiku wa giza' na wazungu wakasema 'let sleeping dogs lie' maana wakiamka hujui watafanya nini!
 
Mi nadhani tumeshajua ila hatujajua wengi wa kutosha kuweza kufanya mabadiliko na ndio maana hawatishiki sana. Wanajua wanaojua wote ni wenye uwezo wa kupata internate. Je ni asilimia ngapi ya watanzania wana uwezo wa kupata hiyo huduma kama si chini ya 1%. Sasa umefika wakati tuwafikie na walio vijijini kwa njia nyingine bora na madhubuti zaidi kuliko kuishia kwenye internate. Ndio maana wamefika kipindi hawatishiki tena wanajua tunajua lakini hatuwatishi. Tunaojua ni idadi sawa na wao wanaotenda sasa sisi ni wanafiki na wenye wivu kama tulivyowahi kutuita kipindi fulani hapo nyuma.
Kinachotakiwa sasa ni kuanzisha vuguvugu la kitaifa kama kipindi kile tulipodai uhuru wetu kutoka kwa wakoloni weupe. Hawa ni sawa na wale wakoloni tuliowafukuza miaka ya 60 tofauti ni rangi tu. Hawataondoka kwenye huo ulaji wao mpaka tuwe na nia thabiti ya kuwaondoa ala sivyo tutaonekana mabwege kila kukicha.
Sasa hapa nataka tufanye hivi..... ripoti kama za meremeta hazipaswi
kuishia kwenye mitandao tu ya internate. Zichapishwe zigawanywe kwa wananchi kila mmoja ajue nini kinachofanyika. Hapa sisemi tunahitaji kufanya hivyo kwa kujificha hapana tuyafanye kwa dhahiri kabisa na wajue tuyafanyayo. Hizo nakala zinaweza kuuzwa kwa bei ambayo mtanzania wa kawaida kabisa anaweza kuinunua.
Jamani tukumbuke kwamba hatuhitaji watanzania milioni 40 kuanza hizi pirikapirika kwa pomoja. Tuanze sisi mia wenye nia baadae tukawawezesha na wenzetu. Ila tukitaka sisi mia tupambane na wao mia hatuwezi wenyewe wana na vya ziada tutaishia kujua then roho zitueme halafu tuzoee.
Ni wakati sasa wa mapambano ya dhati kabisa.
Naomba wenye nia hasa watoe mwelekeo nini kifanyeje tuweze kutenda kwa tunayoyajua na wala tusiwafiche tumechoka jamani.

salamu!!
Dawa nikuanza kuwaelimisha watoto wetu na wana familia zetu wote juu ya mwenendo mbaya wa nchi yetu ambao chanzo chake ni utawala mbovu wa serikali ya chama kimoja tokea uhuru tunatakiwa tubadilike kwenye kila kitu.
 
Baada ya kusoma post hii, nilikuwa naona, tungefungua Forum ya UFISADI. Hii ingewekwa kwa ajili ya kumbukumbu ya ufisadi mbalimbali uliokwisha fanyika na kwa waliohusika. Tatizo nililoliona, ni sisi wananchi tunakuwa busy sana katika kujihusisha na shughuli zetu binafsi, kiasi kwamba ufisadi unapoandikwa katika magazeti, ni rahisi kusoma na kusahau. Kama ingewekwa forum decicated to UFISADI, tungeweza kupitia kila siku na kujikumbusha ujinga unaondelea katika serikali yetu. Yani ingewekwa na ya quotation ovyo ovyo, ingekuwa fresh kabisa.

Nakumbuka MMKJ alikuwa anafanya reseach ya asili ya ufisadi, imeishia wapi mkulu! Tunangoja
 
Mzee Mwanakijiji naona umeanza kukata tamaaaa!!!! wapiganaji hatasiku moja hawakati tamaa bali hurudisha nyuma majeshi na kupanga mbinu mpya za kumkabili adui..
Ni kweli habari nyeti siku hizi zimekuwa nje nje tu!!!!! Wanaozitoa ni wapiganaji wanaotaka tadanganyika wengine wazipate hizo nyeti ili adui ajue kwamba yupo uchi....Pia tutarajie watu nao watazinduka......

mathalani wamegoma kubadilisha kanuni za uchaguzi, mwezi ujao kuna uchaguzi kwa kanuni zile zile za kijamaaa!!!! Tatizo nchi ipo kwa old BOYS TO MEN!!!! wanakenua tu, na mdudu wa watanziania kuamini kila kitu atakacho sema mkuru basi ni shida.....

ALUTA CONTINUA
 
hamna lolote, upuuzi mtupu, tena unaofaa kupuuzwa, huna jipya!
 
Asante sana kwa tafakari yako yenye kina na hekima. Kujua hilo ulilosema si bure, kwani huenda ikawa ni hatua ya kwanza kwawajulishwa kuelekea kufanya kitu fulani juu ya mambo ya muhimu tujulishwayo...Ikingali bado kunapingamizi zinazozuia safari ya binadamu kuelekea utu kamilifu, sikumoja yatatokea mapinduzi kama njia pekee ya kulazimisha hali hiyo, kama yalivyotokea huko nyuma....Ni bahati mbaya tu kuwa mapinduzi hayo yanaweza kughalimu damu...maana waliopewa majukumu ya kubalisha hali hawafanyi hivyo kiustaarabu.......

Watanzania wenzangu tukumbuke busara ya yule mwanamapinduzi mtanzania, Kinjeketile...aliamini kuwa "Neno linanguvu ya kubadili risasi kuwa maji...."

Mwanakijiji naomba uendelee kutushirikisha tafakari yako juu ya neno, ufahamu na maana zake.
 
00:00:00: Meremeta..Extra
Mbona hiyo mada ilifungwa? na vipi kuuziana zile nyaraka 100 kwa dola 30? au mlipishana kimakubaliano na mod....?
ila all in all harakati zako zimeanza zamani sana japo siku hizi umepunguza kufukunyua yale yanayo itwa siri.
 
............but,at least corruption is taken care!...or minimised!


............NOT UNTIL WE ELIMINATE CCM INTO POWER!kani and according to me,sisiemu haiondolewi madarakani DIPLOMATICALLY!angalia namna wanavyotumia mabavu kushinda chaguzi ndogo!NO WAY BWANA


mwanakijiji i would like to have clarifications on this idea,please!naona kama umeniacha njia panda


practically WE CANNOT!as long as ccm will remain into power

You mean.!:thumbup:
 
Na. M. M. Mwanakijiji




Lakini swali linalonisumbua zaidi ni kuwa hivi tunajua ili kiwe nini? Ujuzi wetu wa mambo yanayohusu hali ya nchi yetu, siasa zetu, viongozi wetu unatusaidia vipi? Tunajua mambo haya yote na kupeana taarifa kila baada ya sekunde halafu nini kinafuata?

Je tunajua ili kuridhisha udadisi wetu ili na sisi tuwe miongoni mwa wajuao? Tunajua ili na sisi tuoneshe kuwa tunajua na si mbumbumbu? Tunajua haya yote na mengine mengi tunayoyapata kijiweni halafu yanatubadilisha sisi tuweje? Kama katika kujua kwako hujabadilika kwa namna yoyote sasa si bora kuishi bila ya kujua?


Je ni lazima watu wote wajue kila kitu au wakati mwingine ni bora wachache wajue kwa niaba ya wengi? Unajua hilo?



Kwanini tusome historia kwa mfano Wazungu kugawana Afrika kama keki enzi hizo za 1884 kama kujua jambo hakuna faida?
Mpaka leo hii bado unadhani kujua hakukuwa na Faida?
 
Mimi nataka kujua undani wa Meremeta.... tuwasiliane kwa PM ndugu yangu!
ukishajua utafanya nini na ganzi yako. MLETA MADA KASHUSHA NONDO kwa great thinker. GANZI isipopatiwa suruhisho hamtapata siri za mafisadi .a ndio kwishne.MA.A mkipewa vitu nondo yule fisadi; kwa ganzi zenu na flana ya bure mnampigia makofi arudi tena mjengoni akackote
 
Re: Ndugu Mtanzania: Je unajua hili?
Nafikili sasa viongozi wa serikali yetu wanatupeleka kuzimu kwa tamaa zao.Hivi kweli waziri ambaye ni daktari kwa taaruma anataka kununua bajaji kwa ajili ya kubeba wagonjwa! Hao wagonjwa wamekuwa magunia ya mihogo?

wakati wao wanatembelea shangingi la milioni 200. kwa nini asijitolee kutembelea gari ya milion hata 50 hizo zingine zikanunua gari la wagonjwa. Anaona abaki na shangingi mil 200 na mgonjwa apande bajaji ya mil 4. JE AKIUMWA YEYE ATAPANDA BAJAJI?
MWANANCHI FUNGUKA NA NCHI YAKO USIKANDAMIZWE; USINYONYWE nchi yetu tajiri zaidi ya Afrika Kusini. kama unabisha angalia gesi ya mtwara. angalia chuma cha mchuchuma.
 
Back
Top Bottom