Ndugu wakulima na wafugaji sema changamoto yako kuhusu mazao yako na kila aina ya mifugo Ili wataalamu wakusaidie kutatua changamoto hiyo

Asante mkuu. Ila huu mchanganyiko mbona kama kuku wa kisasa
 
Shubiri Mwitu (Aloe vera):
Chukua majani 3-5 makubwa, katakata na loweka ndani ya
maji lita 10 kwa masaa 12 hadi 16. Wape kuku kwa siku 5 - 7.
Isiyotumika mwaga na tengeneza nyingine baada ya masaa 12.

Mchanganyiko huu unaweza kutibu:

Kideri/Mdondo (Mdonde/Chikwemba/Kitoga/Chinoya/Sotoka)
- inyweshwe kabla kwa kinga.
Homa ya matumbo (Typhoid).
Mafua (Coryza).
Kipindupindu cha kuku (Fowl Cholera).


Mwembe:

Majani magao mawili, ponda na chemsha ndani ya lita 6 za maji hadi ibaki lita 1. Wape kwa siku
moja.

Mwembe hutibu:
Homa ya matumbo.
Mafua.
Kinga ya Kideri/Mdondo
 
Nimbolea gani nzuri yakupiga kwenye tangawizi
MBOLEA
Wiki 1-2 kabla ya kupanda weka mbolea ya samadi au mboji kiasi cha tani 10 - 12 Kwa ekari na kwa kukuzia weka kiasi cha NPK. N 40 – 48 kg, P2O5 31.2 – 32 kg, na K2O 40 – 48 kg. Mwanzoni tumia nusu ya Nitrogen na kiasi chote cha P na K, kiasi kilichobaki cha Nitrogeni kitumike siku ya 45 na 90 baada ya kupanda. Tandaza nyasi shambani kuhifadhi unyevunyevu hasa pale kivuli kinapokosekana. Palizi hufanywa mara magugu yanapoota, dawa ya kuua magugu, Kama simazine hutumika.


Nimeitoa sehemu sijawahi lima tangawizi mkuu sina uziefu huo. Tusuburi wengine waje ama ingia hapo

Kilimo cha Tangawizi - Masoko, Mbinu na Ushauri Toka kwa Wadau
 
Mimi kuna kuku amechomwa na mwiba ama msumari (sina uhakika) hapa pa kukanyagia..leo ndo nimemuona jioni wakati wanaingia ndani ya banda Amevimba na nimejaribu kupashika analalamika. Nampatia nini ? Antibiotics? Nilichokifanya nimemsafisha hapo palipoumia kwa maji then nikampaka alovera.
 
Pole saana! Tafuta dawa ya vidonda ile ya kupuliza
 
Nitajie jina la viazi vya kulisha nguruwe tunavyo kaangiwa hapa dar es salaam kama chips...kisha niambie kwanini viazi vizuri vya chips vimepotea nchini ...kwanini serikali pumbavu ya samia inashindwa kuweka viwango na ubora na aina za mazao yaliyo chaguliwa kwa ubora kulimwa nchini na kupiga marufuku mbegu zote na kilimo cha mazao mabovu kama hivi viazi vya kulishia nguruwe ambavyo huyu msomali.mpuuzi kafanya vifulike nchini ...sifa ya hivyo viazi ni kama utapikia pilau basi vyenyewe vina anza kuchacha kabla ya pilau na kuozesha pilau lililo lala....kama unajua jina la hivyo viazi mviringo ni vyema ukatuambia jina lake?
 
Samahani sana mkuu sikuona notification yako asee. Ulichofanya ni sahihi zaidi ya yote chukua maji ya mkonge (katani) unakuwa unaweka hapo kwenye jeraha kila umalizapo ku,safisha na maji ya vuguvugu yaliyotiwa chumvi kidogo.
 
Samahani sana mkuu sikuona notification yako asee. Ulichofanya ni sahihi zaidi ya yote chukua maji ya mkonge (katani) unakuwa unaweka hapo kwenye jeraha kila umalizapo ku,safisha na maji ya vuguvugu yaliyotiwa chumvi kidogo.
Sawasawa. Ila nilitumia alovera tuu..asubuhi namnywesha na kumpaka, jioni nampaka tuu..siku tatu tuu akawa sawa.

Asante sana Mkuu. Hiyo ya katani sijui nitapata wapi niipande hapa kwangu...?
 
Sawasawa. Ila nilitumia alovera tuu..asubuhi namnywesha na kumpaka, jioni nampaka tuu..siku tatu tuu akawa sawa.

Asante sana Mkuu. Hiyo ya katani sijui nitapata wapi niipande hapa kwangu...?
EE UKIPANDA NI NZURI ZAIDI
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…