Ndugu wamuua dada yao wakigombea ardhi

Ndugu wamuua dada yao wakigombea ardhi

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Wanaume wanne wamekamatwa kwa madai ya kumuua dada yao waliompiga hadi kumsababishia umauti kwa kile kinachodaiwa kuwa ni mgogoro wa ardhi waliokuwa nao kwa muda mrefu.

Tukio hilo limetokea siku ya Jumamosi usiku, wilayani Rukiga nchini Uganda, tovuti ya Monitor ya Uganda imeripoti.

Watuhumiwa hao ambao ni kaka wa marehemu wote ni wakazi wa Ibumba katika kata ndogo ya Rwamucucu, wanadaiwa kumshambulia kwa kipigo dada yao aitwaye Christine Kiconco mwenye miaka 41.

Msemaji wa polisi mkoani Kigezi, Elly Maate aliwataja washukiwa ni Innocent Tumwekwase, Samuel Atuhirwe, Christopher Bikorwomuhangi na Justus Mayumba.

"Inadaiwa kuwa familia ya marehemu imekuwa na mgogoro wa ardhi tangu baba yao aitwaye Selestino Byaruhanga alipoamua kuwagaia urithi watoto wake hao ndipo matatizo yalipoanza,” alisema Maate.

Inasemekana watoto wa kiume waliamua kuuza ardhi yao mara moja baada ya kurithishwa na kuanza kudai sehemu ambayo walipewa watoto wakike na tangu wakati huo, wamekuwa wakimtishia marehemu.

Kulingana na polisi, wamesema marehemu alirudi nyumbani akiwa amelewa majira ya saa nane usiku wa kuamkia Jumamosi ndipo umauti ukamkuta.

Polisi walifika eneo la tukio wakiwa na mbwa wa kunusa ambapo aliwaongoza maafisa wa uchunguzi hadi kwenye nyumba za washukiwa na hivyo kukamatwa.

Kesi hiyo ya mauaji ya kushambulia imefunguliwa katika Kituo cha Polisi cha Rukiga Kusini Magharibi mwa Uganda.

MWANANCHI
 
Umasikini ni tatizo. Hao wanaume wanashindwa kununua ardhi mpk wagombanie ardhi ya urithi?
Bora hata wangekuwa vijana chini ya miaka 18 ningesema utoto lkn watu wazima. Ni upumbav sana
 
Siwangeenda ata vikindu kule nasikia Kuna adi vya laki 6
 
Umasikini ni tatizo. Hao wanaume wanashindwa kununua ardhi mpk wagombanie ardhi ya urithi?
Bora hata wangekuwa vijana chini ya miaka 18 ningesema utoto lkn watu wazima. Ni upumbav sana
Wanagombe urithi wa ardhi wakati kimira mtoto wakike hatakiwi kuridhi aridhi ya ukoo,wanamke hatakiwi kugombea ardhi ya ukoo, waAfrika tumeacha tamaduni zetu na kuzifuata tamaduni za magharibi, Mtoto wakike hawezi kurithi ardhi ya ukoo, yeye ana rithi mali za mume wake tu, Watoto wakike wanatakiwa waambiwe ukweli kwamba wakishaolewa hawa tena chao ila wana haki ya kurithi kwa mume wake.
 
Wanagombe urithi wa ardhi wakati kimira mtoto wakike hatakiwi kuridhi aridhi ya ukoo,wanamke hatakiwi kugombea ardhi ya ukoo, waAfrika tumeacha tamaduni zetu na kuzifuata tamaduni za magharibi, Mtoto wakike hawezi kurithi ardhi ya ukoo, yeye ana rithi mali za mume wake tu, Watoto wakike wanatakiwa waambiwe ukweli kwamba wakishaolewa hawa tena chao ila wana haki ya kurithi kwa mume wake.
Dah Aisee...zama hizi kweli bado mawazo haya yapo bado?vipi kwa aliyepata watoto wa kike pekee?mali hizo atarithi nan ss?
 
Wanaume wanne wamekamatwa kwa madai ya kumuua dada yao waliompiga hadi kumsababishia umauti kwa kile kinachodaiwa kuwa ni mgogoro wa ardhi waliokuwa nao kwa muda mrefu.

Tukio hilo limetokea siku ya Jumamosi usiku, wilayani Rukiga nchini Uganda, tovuti ya Monitor ya Uganda imeripoti.

Watuhumiwa hao ambao ni kaka wa marehemu wote ni wakazi wa Ibumba katika kata ndogo ya Rwamucucu, wanadaiwa kumshambulia kwa kipigo dada yao aitwaye Christine Kiconco mwenye miaka 41.

Msemaji wa polisi mkoani Kigezi, Elly Maate aliwataja washukiwa ni Innocent Tumwekwase, Samuel Atuhirwe, Christopher Bikorwomuhangi na Justus Mayumba.

"Inadaiwa kuwa familia ya marehemu imekuwa na mgogoro wa ardhi tangu baba yao aitwaye Selestino Byaruhanga alipoamua kuwagaia urithi watoto wake hao ndipo matatizo yalipoanza,” alisema Maate.

Inasemekana watoto wa kiume waliamua kuuza ardhi yao mara moja baada ya kurithishwa na kuanza kudai sehemu ambayo walipewa watoto wakike na tangu wakati huo, wamekuwa wakimtishia marehemu.

Kulingana na polisi, wamesema marehemu alirudi nyumbani akiwa amelewa majira ya saa nane usiku wa kuamkia Jumamosi ndipo umauti ukamkuta.

Polisi walifika eneo la tukio wakiwa na mbwa wa kunusa ambapo aliwaongoza maafisa wa uchunguzi hadi kwenye nyumba za washukiwa na hivyo kukamatwa.

Kesi hiyo ya mauaji ya kushambulia imefunguliwa katika Kituo cha Polisi cha Rukiga Kusini Magharibi mwa Uganda.

MWANANCHI
wanyongwe
 
Wanagombe urithi wa ardhi wakati kimira mtoto wakike hatakiwi kuridhi aridhi ya ukoo,wanamke hatakiwi kugombea ardhi ya ukoo, waAfrika tumeacha tamaduni zetu na kuzifuata tamaduni za magharibi, Mtoto wakike hawezi kurithi ardhi ya ukoo, yeye ana rithi mali za mume wake tu, Watoto wakike wanatakiwa waambiwe ukweli kwamba wakishaolewa hawa tena chao ila wana haki ya kurithi kwa mume wake.
Wewe na ukubwa wote huo unashindwa kununua ardhi mpk ugombee ardhi ya urithi?
Ardhi wangekuwa wanarithi wanawake maana hawajui kutafuta na sisi wanawaume tutafute hela zetu tukanunue ardhi zetu kwa pesa zetu.
Haya sasa, unamuua ndugu yako kwa sababu ya ardhi ya urithi si ukichaa huu.
Haina tofauti na waarabu, wanauana wenyewe wanawasingizia wamerekani. Hapo sijui hao jamaa watamsingizia shetani au ardhi?
 
Wewe na ukubwa wote huo unashindwa kununua ardhi mpk ugombee ardhi ya urithi?
Ardhi wangekuwa wanarithi wanawake maana hawajui kutafuta na sisi wanawaume tutafute hela zetu tukanunue ardhi zetu kwa pesa zetu.
Haya sasa, unamuua ndugu yako kwa sababu ya ardhi ya urithi si ukichaa huu.
Haina tofauti na waarabu, wanauana wenyewe wanawasingizia wamerekani. Hapo sijui hao jamaa watamsingizia shetani au ardhi?
Kwanza ardhi yenyewe babayao alishaigawa wao wakaiuza yote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanagombe urithi wa ardhi wakati kimira mtoto wakike hatakiwi kuridhi aridhi ya ukoo,wanamke hatakiwi kugombea ardhi ya ukoo, waAfrika tumeacha tamaduni zetu na kuzifuata tamaduni za magharibi, Mtoto wakike hawezi kurithi ardhi ya ukoo, yeye ana rithi mali za mume wake tu, Watoto wakike wanatakiwa waambiwe ukweli kwamba wakishaolewa hawa tena chao ila wana haki ya kurithi kwa mume wake.

Lakini kutokana na maelezo ,baba yao ndio aliowarithisha Ardhi hao mabinti zake baada ya kuwagawia hao wanaume sehemu yao!! Hivyo mirathi ya baba yao lazima iheshimiwe.
 
Back
Top Bottom