Ndugu yangu amenipa sharti la kuacha kazi ya kuajiriwa ili anipe mtaji wa Tshs 200M nianze shughuli yangu mwenyewe lakini sijui nifanye shughuli gani!

Kama kasema ukifilisika ni shauri yako hatakudai.... kwanini akulazimishe uache kazi? Kama kaamua kukupa mtaji si akuache upange unavyoona inafaa???

Nina mashaka na huo msaada
Kweli! Kwa mini Msaada unaanza na Masharti ya Kuacha kazi yako kwanza!!


Anyway, Unaweza ukachukua likizo kwanza Muamalo usome kwanza!
 
Kw Kwa kweli huyo ndugu anakutakia mema sana.
 
Mkuu, sualala kwamba hatatoa hiyo hela halipo kabisa. In fact hiyo hela nina acces nayo, ni suala la kuamua tu. Yaani scenario iko hivi, kama ukiamua, transfer hiyo amount utumie kwenye hiyo shughuli, ila usifanye hivyo hadi unihakikishie umeacha kazi kama tulivyokubaliana. Kwa jinsi uhusano wetu ulivyo, siwezi kudanganya, na yeye anajua siwezi kabisa kumdanganya.

Kumbuka, nina access ya hela zake kwa kuwa ananiamini, na hata amesema kama kiti kikimtokea nifanye nini na account zake. Sasa ikiwa yeye ananiamini kiasi hicho, kwa nini nimdanganye?
 
Mkuu kama hutajali kazi yako ni profession ipi? Maaana kama unaimudu pia unaweza kuifanya kama consultant km ni kazi yenye demand na utaweza kufanya marketing
 
Fanya biashara ya spea za magari na pikipiki .Tafuta miji inayokua kwa Kasi kubwa fungua hiyo biashara inalipa.Mzigo kachukue Dubai hela inazaa hela.Ukichukua Dubai spea manake sokoni utapunguza Bei ili upate wateja wengi .

Kumbuka!:Sio Kila mtu amezaliwa ili afanye biashara .
 
Hiyo pesa ukianzisha duka la Mangi la vitu vya kawaida la JUMLA location iwe nzuri na bei nzuri mwanzoni tu utapata profit above laki 5 kwa siku,
Tahadhari ni udhibiti viana wasikuibie kwa kuwa faida ya bidhaa hizo ni ndogo sana.
By 2 years utakua mbali sana na profit itaboost kuwa zaidi ya 2m per month
 
Bro ako yuko na upeo mkubwa tambua kuwa kila mwajiriwa ni mtumwa kwa bosi wake, Ushauri wangu chukua likizo ya siku 28 au siku 14 tu nenda mbali na mazingira uliozoea explore nature muda huo ujitenge na watu kidogo uwe peke yako jitathmin then ukitoka huko akili itakuwa imekukaa sawa utamwelewa zaidi bro ako nini anataka ufanye.
 
Yote kwa yote fedha ziingie kabla hujaacha. Uhai umuondoka binadamu kwa sekunde 1 tu. Punguza risk.
 
Unaroho ya kitajiri au maisha mazuri? Jua upo wap kati ya hapo. Utapata jibu
 
Hiyo milioni 200 ni hela ndogo sana.
Kama umeoa na una watoto baki na kazi yako ya kuajiriwa (Tshs. 1.5M). Unaoneka huna plan.

Tshs. 200M sio nyingi kama haujui nini cha kufanya. Unaweza kujikuta umebakiwa na 10M baada ya miaka 5.
 
Fungua duka la hard ware litakulipa chukua m.40 leta mzigo wa mbao aina zote,nunua cement jumla m.15,weka na bidhaa misumari,bawaba,komeo vifaa vya electronic na no ambavyo weka m.10 anzia na hizo.Ila waweza pia ongeza eneo fyatua tofali fanya installation ya machine ya umeme na nunua na dump truck ifanye biashara kwa umakini within one year ni billionaire
 
Mil 100 wekeza kwemye bondi za Benki Kuu afu mil 50 wekeza kwa UTT, afu 50 ya mwisho Anza biashara ya mazao...buying and selling... usitume mtu fanya mwenyewe.
 
Unasubiri nini mkuu? Achana na umaskini huo, 1.5 ndo kitu gani? ukiwa na 200 m Unaweza hata kutengeneza 20m kwa mwezi hiyo 1.5 ikaishia kuwa budget ya mtoto wako tu kwa mwezi. Usimsikileze mkeo akili yake tayari isharidhika na umaskini, Changamka mkuu
 
Hiyo hela nyingi anzisha biashara ya jumla unatoboa fasta.upo mkoa gani .leo hii ukiwa na 200 ukienda kwenye makampuni makubwa ukinunu mzigo mzigo wa milioni 200 wanakuongezea hata 80 kama mteja mwaminifu kama bidhaa za azam
 
Mkuu nenda Goba nunua viwanja vya kutosha jenga nyumba na vyumba vya kupangisha. Kula hela umekaa nyumbani na glass yako ya maziwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…