Ndugu zangu naombeni ushauri, ujauzito huu ni wa nani au nifanye nini?

Ndugu zangu naombeni ushauri, ujauzito huu ni wa nani au nifanye nini?

Habari wakuu,

Naamini ni wazima wa afya.

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada..

Ndugu zangu, nina miaka kadhaa tangu 6/2012 nimuoe shemeji yenu, tumekuwa tukihangaika kupata mtoto lakini mpaka mwaka huu ikawa imeshindikana bila mimi kuwa na shida yoyote na yeye mke wangu alikuwa na matatizo madogo dogo (majibu ya hosptal) ambayo tulishasolve lakini bado ikawa bado mtoto kupatikana.

Sasa kufikia tar 20/08/2016 tukashauriwa tumuone Dr. fulani hivi ni mtaalamu wa wanawake na alikuwa amesaidia wengi tu, Tarehe hiyo hiyo mke wangu alikuwa kwenye siku zake ndo ilikuwa inaanza alipewa dawa za siku 5 kila mwezi atapoingia bleed lakini kuanzia alipoanza kutumia hizi dawa kulikuwa na madiliko katika mwili wake uke unakuwa na ute wa kutosha wakati wa kukutana na wife, na Dr kutokana tarehe hizo alizoingia Bleed akatueleza kuwa kuanza Tar 01-05/09/2016 tuanze kukutana na mke wangu kwani si siku nzuri za kupata ujauzito.

Sasa hapa naomba wataalamu kuhesabu tarehe za mwanamke kushika Mimba wachukue nafas hasa huu wa siku 28 kufika tarehe 29 au 30/08/2016 nakumbuka nilikutana na mke wangu usiku kwa furaha tu.

Lakini kufika tareh 02/9 jioni mke wangu aliniomba ruhusa ya msibani lakini sikumjibu chochote ili badae kidogo niombe chakula ya usiku nikapewa lakini si kwa furaha kivile kama alinitengea tu nilipomaliza nikampa jibu kuwa hakuna kwenda msibani lakini asubuhi aliondoka kienyeji tu na akasafiri akaenda mkoani kwa hawara yake aliyekuwa anachat naye kwa siri sana.

Akaenda akalala naye{inauma} huko Jumamosi kuamakia Jumapili jioni ndo akaingia home nilimbana sana aeleze alipokuwa alikataa kusema japo tayari nilishajua kama wiki hivi alikubali baada ya ugomvi mkubwa sana tukasuluhisha nimamsamehe lakini baada wiki mbili alikuwa mjamzito lakini aliogopa kusema mojamoja kwangu mpaka siku ya 3 ndo kuniambia na mimi nikakataa na kumuuliza hii mimba ya nani? Anajibu yangu nikauliza kwanini na kipi vipi? Ooh yule mwanaume hasimamishi vizuri{inauma}

Sikukubali tareh 22/10/2016 tukaenda kuchek ultrasound ili nijue kama inaweza ku-calculate mimba hii ni ya siku ngapi lakini majibu ujauzito ni wa 7 weeks na siku kadhaa.

Sasa ndugu zangu naombeni ushauri ujauzito huu ni wa nani au nifanye nini?

Nipo njia panda ndugu yenu sina majibu kabisa please

Samahani kama nimechanganya au sijaeleweka sehemu maana natumia simu kuandika.

Asante.
Pole sana ndugu mwanamke hakufai kabisa, ameshapigwa mti na mimba kakuletea dah wanawake wengine ni sawa na mashetani achana naye lakini kama huwezi kumuacha lea mtoto wa hawara wa mkeo ili akikua huyo akuletee mwingine wa nje. Shukuru Mungu umejua mapema kuliko hali hiyo ingekukuta uzeeni alafu ndio unaambia watoto wote wanababa yao wewe ni baba mlezi tu tena ukiangalia uzee umekuingia sawa sawa hata uwezo wa kutafuta binti huna nadhani ungekufa kihoro
 
Fanya DNA mtoto akizaliwa
Usimdanganye hesabu ziko wazi mimba sio yake.Jamaa yangu imemtokea hiyo mwaka huu na miezi ndio hiyo hiyo,yeye ni hakimu mahakama fulani hivi anampenda sana mke wake lakini jamaa kila akitoka kwenda kwenye shughuli zake mkewe anaenda kwa hawara kupigwa miti. Siku moja nikiwa safari nikakutana naye kwenye basi akiwa hawara lakini mimi sikumtambua kwakua kila mtu alikua na yake,basi ikawa kama bahati mbaya kwake guest niliyokwenda kulala nayeye alilala guest hiyo hiyo na hawara yake hadi asubuhi sasa wakati wa kutoka tukagongana uso kwa uso kwasababu tulikua tunawahi usafiri.Baada ya wiki moja mwanamke alirudi nyumbani huku mumewe akijua mkewe ametoka kusalimia ndugu na bahati mbaya aliporudi alikuta mmewe ni mgonjwa na ilimchukua zaidi ya mwezi hali ikiwa bado haijatengemaa wakati huo hawakuwahi kukutana, chaajabu mwanamke akaonekana kunawiri na kutapika mara kwa mara akisikia harufu ya samaki ndipo bwana akaanza kuingia mashaka juu ya mke wake kuwa mjamzito. Akaniita nimsindikize akapime alafu nije nimpe feedback kwakweli nilishindwa kwakua najua niliwahi kumkuta na mtu mwingine hivyo nikamshauri akipona waende yeye na mke wake lakini kabla hajafanya hivyo mkewe akaanza kumwambia waachane eti amemchoka,bwana kashindwa kutoa maamuzi akamjibu mke wake yeye hatoi talaka ndipo mke akaondoka kwenda kujipangia vyumba viwili na mimba sasa haijifichi. Kwaiyo wanawake wa hivyo hakuna sababu ya kupima zaidi ya kuwaacha mapema kwasababu ni aibu mkeo abebe mimba nje nawewe uliyeoa kihalali upo [emoji17] [emoji17] [emoji17]
 
Aisee hii kesi ni ngumu sana hata kwa sisi wazee...

Huyu mleta mada ni mtu jasiri sana...

Mwanamke kaondoka bila kuaga akaenda kwa hawara yake katika tarehe ambayo daktari alishamhakikishia ndio nzuri ya kushika ujauzito... akalala huko usiku kucha. Akakiri jamaa kamlamba... Akapata ujauzito lakini "akaogopa" kusema... baadaye akasema. Kisha anakuambia mimba ni yako kwa kuwa jamaa "hadindishi vizuri"

Hapa kwa sisi wazee wa zamani tunahesabu makosa yafuatayo kwa mwanamke huyu:

1. Mkaidi na mkorofi (Kuondoka kwa jeuri kwenda kwa hawara yake)
2. Mzinzi (kulalwa na hawara yake usiku kucha)
3. Asiyejali (kulalwa na hawara bila kutumia kinga)
4. Muongo (kudanganya hawara aliyemfungia safari kumfuata huko aliko hadindishi vizuri)
5. Mlaghai (kumbambikiza mmewe mimba hewa)

Kwa haya machache tu, baraza la wazee tunamtunukia mleta mada kwa ujasiri uliotukuka aliokuwa nao, kwa maana hakika hapa alipaswa kutuambia sababu zilizomfanya amtaliki mkewe na wala si kutuuliza mimba ile ni ya nani.

Mke haachwi ila kwa zinaa. Kuna kusameheana lakini kosa hili la kudhamiria, lililoambatana na kiburi na ufedhuli wa hali ya juu... hapana bhana!!

Ila kwakuwa wahenga walishatudanganya kitanda hakizai kharamu, basi ngoja tumwache afuate ushauri wa JK... Akili za kuambiwa, changanya na zako.

Baada ya kusema hayo, tafazali nipelekee salamu zangu za dhati kwa mwalimu snowhite na michepuko yangu Heaven Sent , Heaven on Earth , Honey Faith ,atoto Valentina .

Unasalimiwa na shemeji yako geniveros

cc Kaizer
 
Bibkia inasema unaweza kumwacha mkewako au mume wako kwa sababu ya zinaa, wewe unakaa nae wa nini na ameshakubali mwenyewe na kibaya zaidi ana li mzigo usilolojua?

We ni Mwanaume "Bwege" ref Bushoke
 
Aiseeeee wanaume wa siku hizi sijui tupoje tupoje yaani hapo mambo yapo wazi kabisa kuwa mkeo aligongwa na hawara yake alafu mnasuluhishwa na wewe unakubali

siku mbili anakwambia kuwa ana mimba yako alafu unakuja kulia lia humu kuomba ushauri

Timua huyo ni malaya sio mke...mambo mengine hayaitaji kabisa kupeana ushauri yaani umenikera kuliko Magufuli aaaaaarg
Hata sielew mapenz gani..

Mie rafk zangu huwa hawaniombi ushaur kwenye upumbav, naweza kumkata mtu makofi ya chukuchuku..
 
Aisee hii kesi ni ngumu sana hata kwa sisi wazee...

Huyu mleta mada ni mtu jasiri sana...

Mwanamke kaondoka bila kuaga akaenda kwa hawara yake katika tarehe ambayo daktari alishamhakikishia ndio nzuri ya kushika ujauzito... akalala huko usiku kucha. Akakiri jamaa kamlamba... Akapata ujauzito lakini "akaogopa" kusema... baadaye akasema. Kisha anakuambia mimba ni yako kwa kuwa jamaa "hadindishi vizuri"

Hapa kwa sisi wazee wa zamani tunahesabu makosa yafuatayo kwa mwanamke huyu:

1. Mkaidi na mkorofi (Kuondoka kwa jeuri kwenda kwa hawara yake)
2. Mzinzi (kulalwa na hawara yake usiku kucha)
3. Asiyejali (kulalwa na hawara bila kutumia kinga)
4. Muongo (kudanganya hawara aliyemfungia safari kumfuata huko aliko hadindishi vizuri)
5. Mlaghai (kumbambikiza mmewe mimba hewa)

Kwa haya machache tu, baraza la wazee tunamtunukia mleta mada kwa ujasiri uliotukuka aliokuwa nao, kwa maana hakika hapa alipaswa kutuambia sababu zilizomfanya amtaliki mkewe na wala si kutuuliza mimba ile ni ya nani.

Mke haachwi ila kwa zinaa. Kuna kusameheana lakini kosa hili la kudhamiria, lililoambatana na kiburi na ufedhuli wa hali ya juu... hapana bhana!!

Ila kwakuwa wahenga walishatudanganya kitanda hakizai kharamu, basi ngoja tumwache afuate ushauri wa JK... Akili za kuambiwa, changanya na zako.

Baada ya kusema hayo, tafazali nipelekee salamu zangu za dhati kwa mwalimu snowhite na michepuko yangu Heaven Sent , Heaven on Earth , Honey Faith ,atoto Valentina .

Unasalimiwa na shemeji yako geniveros

cc Kaizer


Na hili ndilo neno la Babu...na watu wote waseme Amen.


Thread closed isipokuwa kwa kujibu salamu tu!
 
Na hili ndilo neno la Babu...na watu wote waseme Amen.


Thread closed isipokuwa kwa kujibu salamu tu!
Kwa mamlaka niliyopewa, nakuamuru utangaze eneo na muda ili tukutane tudumishe mila. Uje na wawili kabisa ili tufanye na tambiko letu lile...
 
Aisee hii kesi ni ngumu sana hata kwa sisi wazee...

Huyu mleta mada ni mtu jasiri sana...

Mwanamke kaondoka bila kuaga akaenda kwa hawara yake katika tarehe ambayo daktari alishamhakikishia ndio nzuri ya kushika ujauzito... akalala huko usiku kucha. Akakiri jamaa kamlamba... Akapata ujauzito lakini "akaogopa" kusema... baadaye akasema. Kisha anakuambia mimba ni yako kwa kuwa jamaa "hadindishi vizuri"

Hapa kwa sisi wazee wa zamani tunahesabu makosa yafuatayo kwa mwanamke huyu:

1. Mkaidi na mkorofi (Kuondoka kwa jeuri kwenda kwa hawara yake)
2. Mzinzi (kulalwa na hawara yake usiku kucha)
3. Asiyejali (kulalwa na hawara bila kutumia kinga)
4. Muongo (kudanganya hawara aliyemfungia safari kumfuata huko aliko hadindishi vizuri)
5. Mlaghai (kumbambikiza mmewe mimba hewa)

Kwa haya machache tu, baraza la wazee tunamtunukia mleta mada kwa ujasiri uliotukuka aliokuwa nao, kwa maana hakika hapa alipaswa kutuambia sababu zilizomfanya amtaliki mkewe na wala si kutuuliza mimba ile ni ya nani.

Mke haachwi ila kwa zinaa. Kuna kusameheana lakini kosa hili la kudhamiria, lililoambatana na kiburi na ufedhuli wa hali ya juu... hapana bhana!!

Ila kwakuwa wahenga walishatudanganya kitanda hakizai kharamu, basi ngoja tumwache afuate ushauri wa JK... Akili za kuambiwa, changanya na zako.

Baada ya kusema hayo, tafazali nipelekee salamu zangu za dhati kwa mwalimu snowhite na michepuko yangu Heaven Sent , Heaven on Earth , Honey Faith ,atoto Valentina .

Unasalimiwa na shemeji yako geniveros

cc Kaizer

Mzee mwenzangu hapo naomba nisiongeze neno.

CC atoto
 
Usimdanganye hesabu ziko wazi mimba sio yake.Jamaa yangu imemtokea hiyo mwaka huu na miezi ndio hiyo hiyo,yeye ni hakimu mahakama fulani hivi anampenda sana mke wake lakini jamaa kila akitoka kwenda kwenye shughuli zake mkewe anaenda kwa hawara kupigwa miti. Siku moja nikiwa safari nikakutana naye kwenye basi akiwa hawara lakini mimi sikumtambua kwakua kila mtu alikua na yake,basi ikawa kama bahati mbaya kwake guest niliyokwenda kulala nayeye alilala guest hiyo hiyo na hawara yake hadi asubuhi sasa wakati wa kutoka tukagongana uso kwa uso kwasababu tulikua tunawahi usafiri.Baada ya wiki moja mwanamke alirudi nyumbani huku mumewe akijua mkewe ametoka kusalimia ndugu na bahati mbaya aliporudi alikuta mmewe ni mgonjwa na ilimchukua zaidi ya mwezi hali ikiwa bado haijatengemaa wakati huo hawakuwahi kukutana, chaajabu mwanamke akaonekana kunawiri na kutapika mara kwa mara akisikia harufu ya samaki ndipo bwana akaanza kuingia mashaka juu ya mke wake kuwa mjamzito. Akaniita nimsindikize akapime alafu nije nimpe feedback kwakweli nilishindwa kwakua najua niliwahi kumkuta na mtu mwingine hivyo nikamshauri akipona waende yeye na mke wake lakini kabla hajafanya hivyo mkewe akaanza kumwambia waachane eti amemchoka,bwana kashindwa kutoa maamuzi akamjibu mke wake yeye hatoi talaka ndipo mke akaondoka kwenda kujipangia vyumba viwili na mimba sasa haijifichi. Kwaiyo wanawake wa hivyo hakuna sababu ya kupima zaidi ya kuwaacha mapema kwasababu ni aibu mkeo abebe mimba nje nawewe uliyeoa kihalali upo [emoji17] [emoji17] [emoji17]

Sasa jamaa yako si huyu, akikimbia kumbe mtoto kweli wake?
Suluhisho ni DNA full stop! Km akikuta mtoto si wake si basi kwani nini?
 
kwanza pole sana.
Inaonekana wewe umetawaliwa na mkeo(huo ni ujinga).
Mimba hiyo sio yako ila pia inaweza isiwe ya huyo jamaa aliekwenda kwake. Inaonesha mkeo alikuwa na tabia ya kujalibu kutafuta mabwana wengine kama njia ya kutafuta suluhu ya tatizo lake(alikuwa na mashaka na uzazi wako).
Na baada ya kupata hawezi kukuheshimu tena na ndio mana anakutamkia maneno kama hayo.
SITAKI KUUMA MANENO HAPA CHA KUFANYA ACHANA NA HUYO MWANAMKE.
ILA KAMA UMEFUGWA AU UNAO UWEZO WA KUVUMILIA KULEA MTOTO SI WAKO,DHARAU NA VITUKO VYA HUYO MWANAMKE, BASI ENDELEA KUISHI NAE.
 
Fanya DNA mtoto akizaliwa
Huu n ujinga ulee mimba ya dume lenzio ukiwa unajua kabsa kwa akili ya kawaida mimba hujamtia ww unasubir vipimo vya mzungu na biology yake DNA acha uzuzu JIPU ILO TUMBUAA
 
Huu n ujinga ulee mimba ya dume lenzio ukiwa unajua kabsa kwa akili ya kawaida mimba hujamtia ww unasubir vipimo vya mzungu na biology yake DNA acha uzuzu JIPU ILO TUMBUAA

Wewe mwenye akili umegundua nini zaidi ya judgments kuliko Mungu? Nipishe!
Siku zote mama anajua baba wa mtoto nani, kama anadanganya wkt anajua kuna vipimo atakuwa na akili nyingi kama zako.
 
Wewe jamaa kweli ni bwege kweli, yaani mwanamke unamwambia asiende msibani anakataa na kutimkia mkoani kabisa halafu anakwambia kwamba hawara yake hasimamishi na wewe bado unaendelea naye tu! Huenda tabia aliyonayo na wewe unayo ndio maana unaona ni kawaida tu. Huyo mwanamke ni malaya na inaonekana ulioa kwa kumlazimisha sana.

Ndege wafananao huruka pamoja. Kama unaweza kuishi na malaya huku wewe huna tabia hiyo basi endelea kuishi naye tu, ulee mtoto wa mwanaume mwenzako huku ukiendelea kusaidiwa na wanaume wenzako.
 
..nimeipenda hiyo {Inauma}!!

Lkn we jamaa ni mzima kweli!?? Mkeo(wa ndoa) ankuacha anenda nje kudhini alaf anarudi unamsamehe!?? Je Akikuletea UKIMWI utakuja kuomba msaada hapa!??...

..Eti ansema huyo jamaa "hasimamishi vizuri"!! kwa hali ya kawaida huyo jamaa angekuwa HANITHI mkeo angeenda kufuata "PIRA/MSHEDEDE"!!??

Bro tumia akili..dhambi ya uzinifu kwenye ndoa inatosha kabisa kuvunja ndoa!??

DONT BE DUMB...HUYO MWANAMKE ATAKULETEA WATOTO WA MAJAMBAZI HUMO NDANI..

...Inauma!!...Inauma..!!
Yaani kitendo cha kusafiri kwenda mkoani tu ni sababu tosha ya kumtimua. Huyo mwanamke akimpata mwanaume anayepiga show kubwa anaweza kumuwekea sumu huyu jamaa ili hawara yake amrithi.

 
Sasa jamaa yako si huyu, akikimbia kumbe mtoto kweli wake?
Suluhisho ni DNA full stop! Km akikuta mtoto si wake si basi kwani nini?
DNA kwa bongo ni siasa tupu maana wanaona vipimo vikitolewa na kuonesha baba wa mtoto ni mwingine itasababisha mifarakano na mtoto kukosa matunzo.
 
Wewe mwenye akili umegundua nini zaidi ya judgments kuliko Mungu? Nipishe!
Siku zote mama anajua baba wa mtoto nani, kama anadanganya wkt anajua kuna vipimo atakuwa na akili nyingi kama zako.
[HASHTAG]#Clueless14[/HASHTAG] nahisi wewe pia ni mmoja wao kama umeolewa lazima utakua umemletea mmeo mtoto wa nje siamini kabisa unavyotetea ujinga wa mwanamke mwenzio khaaa !! [emoji86] [emoji86] [emoji86]
 
Back
Top Bottom