Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 57,951
- 32,619
Ndullu akataa kutaja adhabu'waliochemsha' BoT
Na Reuben Kagaruki
GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndullu, amesema hatarajii kutangaza leo wala kesho hatua watakazochukuliwa watumishi wa benki hiyo wanaodaiwa kuhusika kufanikisha kampuni 22 kuchota kiasi cha sh. bilioni 133 katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).
Akizungumza na gazeti hili juzi baada ya kumalizika mjadala kuhusu aliyekuwa Gavana wa benki hiyo, marehemu Gilman Tutihinda, uliofanyika Dar es Salaam , Prof. Ndulu, alisisitiza kuwa atatangaza hatua za kuwachukulia baada ya mchakato wa kuwahoji na kuwasikiliza kumalizika.
"Kamati inayoshughulikia suala hili inafanya hivyo ili kutafuta haki, sitarajii kutangaza matokeo leo wala kesho," alisisitiza Prof. Ndullu.
Huku akikaata kueleza hatua za uchunguzi na kuwahoji zilipofikia, Prof. Ndullu hakuwa tayari kutaja idadi yao. Alipobanwa na gazeti hili ataje ni wafanyakazi wangapi wa benki hiyo wanadaiwa kuhusika, alisema 'sijui.'
Alipobanwa zaidi kuhusu suala hilo , Prof. Ndullu alisema tayari suala hilo alishawaeleza waandishi wa habari na kumtaka mwandishi wa habari hizi kurejea kumbukumbu zake.
Awali akifungua mjadala huo, Prof. Ndullu, aliwataka wahisani mbalimbali kujitokeza kuchangia mfuko wa Elimu wa Gilman Rutihinda ambao umeweza kusomesha watu wengi.
Alisema baadhi ya watu wamesomeshwa shahada ya pili na mfuko huo. Alisema wanafunzi 17 wanaofanya vizuri katika maeneo yaliyoainishwa wamekuwa wakisomeshwa na mfuko huo.
"Mfuko utaendelea kutoa udhamini, tunatoa mwito kwa wadau wote waendelee kuuchangia," amesema.
Kwa upande wake mtoto wake hayati Rutuhinda, Renatha Rutihinda aliwashukuru wote ambao wamekuwa wakijitolea kuendeleza mfuko huo na kuwataka waendeleze moyo huo.
Na Reuben Kagaruki
GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Benno Ndullu, amesema hatarajii kutangaza leo wala kesho hatua watakazochukuliwa watumishi wa benki hiyo wanaodaiwa kuhusika kufanikisha kampuni 22 kuchota kiasi cha sh. bilioni 133 katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).
Akizungumza na gazeti hili juzi baada ya kumalizika mjadala kuhusu aliyekuwa Gavana wa benki hiyo, marehemu Gilman Tutihinda, uliofanyika Dar es Salaam , Prof. Ndulu, alisisitiza kuwa atatangaza hatua za kuwachukulia baada ya mchakato wa kuwahoji na kuwasikiliza kumalizika.
"Kamati inayoshughulikia suala hili inafanya hivyo ili kutafuta haki, sitarajii kutangaza matokeo leo wala kesho," alisisitiza Prof. Ndullu.
Huku akikaata kueleza hatua za uchunguzi na kuwahoji zilipofikia, Prof. Ndullu hakuwa tayari kutaja idadi yao. Alipobanwa na gazeti hili ataje ni wafanyakazi wangapi wa benki hiyo wanadaiwa kuhusika, alisema 'sijui.'
Alipobanwa zaidi kuhusu suala hilo , Prof. Ndullu alisema tayari suala hilo alishawaeleza waandishi wa habari na kumtaka mwandishi wa habari hizi kurejea kumbukumbu zake.
Awali akifungua mjadala huo, Prof. Ndullu, aliwataka wahisani mbalimbali kujitokeza kuchangia mfuko wa Elimu wa Gilman Rutihinda ambao umeweza kusomesha watu wengi.
Alisema baadhi ya watu wamesomeshwa shahada ya pili na mfuko huo. Alisema wanafunzi 17 wanaofanya vizuri katika maeneo yaliyoainishwa wamekuwa wakisomeshwa na mfuko huo.
"Mfuko utaendelea kutoa udhamini, tunatoa mwito kwa wadau wote waendelee kuuchangia," amesema.
Kwa upande wake mtoto wake hayati Rutuhinda, Renatha Rutihinda aliwashukuru wote ambao wamekuwa wakijitolea kuendeleza mfuko huo na kuwataka waendeleze moyo huo.