NE-YO kutua nchini Tanzania; Kufanya Tamasha Mwanza, Mei 21

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
16,515
Reaction score
28,506


Mwanamuziki nguli kutoka nchini Marekani NE-YO ambaye amekuwa akitamba kwa muziki ya mahadhi laini, anatarajiwa kuwasili nchini Mei 19 kwa mwaliko wa Kampuni ya Mawasiliano ya Vodacom Tanzania kwa kushirikiana na Jembe Media Limited.

Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 36 Mmarekani mwenye asili ya Kiafrika, anatarajiwa kufanya onyesho mei 21 jijini Mwanza kwenye uwanja wa CCM kirumba kwenye tamasha lililopewa jina la JEMBEKA NA VODACOM 2016.

Kwa mujibu wa waratibu wa Tamasha hilo, NE_YO pia anatarajiwa kushiriki kwenye shughuli za kusaidia jamii kupitia taasisi ya Vodacom.

Source: Channel ten
 
neyo ni league ndogo bhana, hana nyimbo za kubengisha
 
nyie mnataka kuanzisha ligi na team pinzani..... Lel see
 
chriss brown ndo habari ya town.
hivyo kama wangemleta nngekuwa tayari hata kulipia 500k ili nione tu tamasha lake
 
Neyo wa Sasa ni ligi ndogo, watuletee Lil Wayne au hip hop chic nick Minaj
 
Neyo alikuwa zamani bwana, sahv kama Dudubaya tu
 
Nipo mwanza lakini siwezi kuharibu hela yangu kwenda kwa huyu jamaa
 
Daaah huyu atakuwa kafulia sana aisee yani anashindana mpaka na diamond??duuuh!!!
 
Kwa nini wasimlete JB Mpiana na kikosi chake chote waone kazi na single kali iitwayo 'Kindoki'
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…