Elections 2010 NEC kushurutisha wapiga kura kurudi majumbani badala ya kusubiri matokeo vituoni!

Kwa mwanaume mwenye akili zako timamu kuomba omba ni dalili mbaya
 
Tuhuma hii ailyoitoa Dr. Slaa ni nzito ni vyema ikachunguzwa ipasavyo na mhusika akachukiliwa hatua za kinidhamu haraka iwezekanavyo ili kuiokoa demokrasia yetu ambayo kweli bado ni changa:-


Kukaa kimya kwa serikali kunamaanisha ya kuwa wao ndiyo waliomtuma huyu askari uchwara kusambaza kauli zinazohatarisha amani hapa nchini
 
Ila TANESCO nao wana makusudi kuwakatia wenzao umeme ndio nini ila kama ni zengwe toka kwa Mwakipesile siwezi shangaa mzee ana fitna sana huyu
 
Kaka kwa sasa hivi hakuna hatakaye tucheka akiona tuna kufa kwa ajili ya ukombozi wa taifa letu,atutakuwa wa kwanza.
 
Tatizo lako malaria sugu ni kwamba kutokana na ushabiki wako wa vyama sasa unaamua kuchukua hoja za vyama vingine unavyopenda kuzielewa wewe (you take them complitely out of context), huko ni kukosa umakini. Alichokisema Slaa siyo kwamba atakimbilia kwa nchi wafadhili, kasema kama kura zao zikiibiwa atashtaki kwa vyombo vya kimataifa, na hilo liko wazi kwamba vyombo vya ndani na nje ya nchi viko vinaangalia mwenendo wa kampeni na vitakuwa vikiangalia mwenendo wa uchaguzi wetu unavyoenenda.
 

Fafanua hoja yako, akishindwa kihalali kwenye sanduku la kura au akinyanganywa ushindi kama atashinda? Sidhani kama Dr Slaa akishindwa ndani ya sanduku la kura atalalamika popote lakini hata ningekuwa mimi nikishinda halafu atangazwe mtu mwingine lazima nilalame
 
Niazimeni kamusi tafadhali.

Yeye mwenyewe anaitwa malaria sugu, ni mgonjwa, msameheni, hajui atendalo.Sana sana ashauriwe aende kutibiwa hospitali maalumu, Muhimbili, Kibong'oto au Mirembe
 
Jamani tuendelee kupeana mbinu wanazotumia Awenzetu chchem kuiba kura hii itatusaidia,kumbuka pamoja kwamba wanazunguka kupiga campain, kuchakachua kura ndilo wanalolifikilia zaidi kuliko kuzunguka kwenye campn.AMKENI.
 
Do not argue with a fool, because if you do that, people may not notice the difference!
 
Malaria Sugu ni case ya Milembe Hospital, :llama::llama::llama::llama::llama::llama::llama::llama::llama:
 
Hili swala nadhani hata usarama wa Taifa litakuwa linawaumiza sana kichwa.
 
Swali zuri ila kwa kuwa wana ccm wako humu nafikiri subiri uchaguzi utajua wamejipangaje
 
Hivi hii issue ya JWTZ kutumika kusambaza mabox ya kupigia kura ni kweli? na ni kwanini mwaka huu tu?
Nina wasiwasi mkubwa na hili kama litatokea, maana yake kama wiki moja iliyopita nilipita bara bara ya Kinyerezi kwenda Mbezi nikakuta lori la JWTZ likiwa na askari lime park na jamaa sikuelewa wana fanya nini, lilikuwa na askari kadhaa , isije kuwa ndio uchakachuaji wenyewe huo wakati wa kusafirisha viafaa..
 
malaria sugu hii hoja haina maana kwa sababu dr slaa bado hajashindwa uchaguzi na baadhi ya wachambuzi wanampa uwezekano mkubwa wa kushinda mfano humu jf ambapo wewe mwenyewe, licha a kutengeneza mamia ya usernames na kutoonekana humu jamvini kama ms, bado ws anaendelea kuongoza. hivyo hiyo hoja ni unwarranted.

aidha nakushauri usilazimishe wakuu kufuata trend ya fikra zako kwa sababu uwezo wa kuwa flexible huna katika fikra zako.

kwa mfano, uliposhindwa kwenye kura za maoni za ubunge kupitia ccm kwenye jimbo lililopo huko mwanza kwa mizengwe ya hali ya juu na kushauriwa ujiunge na chadema na chama chako (kama hukuridhika na matokeo), bado umeendelea kung'ang'ania ccm.

hivyo, kujadili kuhusu ws kushindwa sasa ni kama kuingilia kazi ya nec kama ulivyotutangazia hivi karibuni kura yako licha ya kwamba kura ni siri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…