Uchaguzi 2020 NEC: Tulifanya uteuzi wa wabunge wa viti maalum baada ya orodha ya majina hayo kuwasilishwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA 19 Novemba 2020

CHADEMA wateue mbunge viti maalum akatolewe gerezani na kufutiwa kesi usiku wa manane tena anashitakiwa na jamhuri? fikiri upya mzee

Tuvute subira ndugu yangu. Japo napata ukakasi kwanini NEC hawajaweka hadharani barua ya CDM?

Vyovyote vile, siasa ni zaidi ya ukahaba. Pia masikini hana kiapo.
 
Wafungue kesi kwa mahakama ipi ambayo itatenda haki? hivi CHADEMA wateue mbunge wa viti maalum akatolewe gerezani usiku wa manane kuja kuapisha tena anashitakiwa na jamhuri?
Kama wanachama wenu wana weza kugushiwa sahihi na wakakubali basi hakuna chama hapo.
 
Hiyo kesi wanafungulia mahakama ya nchi gani?
Basi hamna viongozi wenye msimamo kama hata mtu akiwaita njoo wana kwenda basi mjue hamna chama hapo.
 
Mbona hamtaji Kwa majina huyo karibu mkuu wa CDM .... Weka hadharani hiyo barua ya katibu mkuu
Kwani CDM ina Makatibu Wakuu wangapi mkuu? Pia kumbuka Katibu Mkuu ni Ofisi siyo jina la mtu. Kuna ma signatories wanaoruhusiwa kusaini kwa niaba ya Katibu Mkuu labda ilisainiwa na Kiongozi mwingine wa CDM ambaye anayo mandate ya kusaini hiyo barua.
 
Kumekucha jamaa anavitumia vyombo Kama hotpot la nyama ni kutii maagizo tu. Afrika Raha sana ukiwa mtawala we ndo katiba we ndo sheria
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…