B
Binafsi sina ugomvi na tafsiri yako juu ya mapendekezo ya Jaji Kaijage wa NEC kwani kila mtu anayo haki ya kutafsiri kitu kadri alivyo elewa na kufuatana na mawazo, mapenzi, matakwa na ushabiki wake kwenye hoja au suala husika.
Hivyo nami nasema kuwa Jaji Kaijage anataka NEC iwe "huru" kwa kupitia kutungiwa Sheria yao ILI waweze kufanya mambo yao ya usimamizi wa NEC na kazi zake zote BILA kutegemea wafanyakazi wa Serikali au kusubiri mgao wa fedha in a form of RUZUKU.
Jaji Kaijage anataka awe na afanye kazi kama "AGENCY", ili apate mgao wa fedha moja kwa moja kwenye bajeti yao na NEC iwe na bajeti yake inayo eleweka, siyo kusubiri kupewa pesa kutoka Hazina kwa ajili ya uendeshaji wa NEC na iwe na wafanyakazi watakao wajibika moja kwa moja kwa NEC na siyo kwa mamlaka na madaraka nyingine ya ajira.
Hii ndiyo tafsiri yangu siyo kuwa eti "wanabanwa" na Serikali katika kufanya maamuzi yao eti kwa vile hawana Sheria yao wenyewe. This is my take.