NECTA:hatihati ikafutwa.

Mzee wa fund

JF-Expert Member
Joined
Oct 24, 2010
Posts
514
Reaction score
89
Kuna mpango unao andaliwa kufuta baraza la mitihani la Tanzania(NECTA).Habari za uhakika kutoka wilaya ya mbozi(mbeya) zasema kuwa kikao cha wadau wa elimu kilifanyika 5/3/2013 kilihusisha wafuatao:mkurugenzi,mkuu wa milaya,madiwani,waratibu elimu kata,wakuu wa shule,watendaji wa kata na vijiji.Inasemekana vikao hivyo ni kwa wilaya zote Tanzania bara na visiwani na ni agizo toka kwa mkuu wa kaya.
Tusubiri tuone.ni suala la muda tuu.
 
aisee umeamka au bado umelala, kwani NECTA wanaingia darasani kufundisha, au NECTA wanasambaza walimu kwenye mashule, AU NECTA wanazuia watoto wasisome waende beach na kufanya mapenzi na waendesha BODABODA
 
aisee umeamka au bado umelala, kwani NECTA wanaingia darasani kufundisha, au NECTA wanasambaza walimu kwenye mashule, AU NECTA wanazuia watoto wasisome waende beach na kufanya mapenzi na waendesha BODABODA

Liwalo na liwe mimi sijui.nilicho fanya mimi ni kutoa taarifa tuu.
 
Hapo
umebugi men
kwa hiyo taarifa yako Eti "madiwani,waratibu elimu kata,wakuu wa shule,watendaji wa kata na vijiji."
ndio waifute NECTA teh teh Teh necta kazi zake unazijua na wizara ya Elimu kazi zake unazijua
 
Maswali ni mengi ikiwemo: Je sheria iliyoiweka NECTA inasemaje juu ya kuivunja? Nani mwenye mamlaka? Je NECTA ikivunjwa nini mbadala wake?
Japo siamini. Ila kwa Tanzania kila ovu linawekena.
 
Wewe upo nchi gani? Wilaya ina mamlaka gani NECTA? Someni shule hata kidogo ili unaposikia jua ukweli then changanya na akili zako ndipo upost kwa watu wenye akili....Mods mtakuwa mnabore sana kama hata threads ambazo hazina maana nyinyi mnapost tu....
 
Mzee wa fund mkuu wa milaya ndo yupi hapo kwenye post yako?
 
Last edited by a moderator:
Wishful thinking....jamaa ana usongo na NECTA km ambavyo nina usongo nao. Tutakapokuwa makini na kufanya maamuzi mazito ya kuinusuru elimu yetu, NECTA itakuwa miongoni mwa taasisi ambazo zinapaswa kumomonyolewa km tutakuwa makini na hatutaathiriwa na mihemuko ama shinikizo kutoka kwa 'wateule'.
 
Du. Mbeya Kuifuta NECTA.? Tutasikia mengi sana. Mpaka leo sijaelewa uhusika wa NECTa kwenye kufeli wanafunzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…