NECTA yaijibu Green Acres.

NECTA yaijibu Green Acres.

Acheni siasa/porojo za vijiweni
kwenye mambo ya kitaalam
kama elimu, tuachieni
wataalam tujadili na
kurekebisha dosari
zilizosababisha kufeli kwa form
four 2013! Nashangaa
MALUMPENI wamekurupuka
from no where kila mtu na
hoja zake dhaifu za vijiweni
mmesomea wapi ualimu au
mnadhani walimu
wanachaguliwa kwa kufumba
macho na kunyosha mikono
juu!!

Sijakuelewa mkuu hizo stori za vijiweni au siasa ni zipi kwenye hii thread wakati sisi tunajadili NECTA ilivyokosoa habari za haya magazeti tajwa
dancani huyu jamaa ameikopy iyo post huko anapojua yeye na kaipaste hapa bila kuangalia topic inasemaje..

kama angekua kaandika yeye isingejibana upande mmoja ie kushoto, hii inatokea endapo mtu unacopy na kupaste..
 
Last edited by a moderator:
Mimi sipendi na wala sitawalaumu waandishi wa HABARI hata siku moja na nitakuwa wa mwisho pekee yangu kufanya hivyo. HUYU MKURUGENZI WA GREEN ACRES alidanganywa na CLOUDS RADIO kuhidhalilisha NECTA eti kwasababu NECTA WAMEWALALAMIKIWA WAO KWA KUMPROMOTE YULE DOGO MWAKA JANA ALIEANDIKA BONGO FLAVA KAMA SHUJAA. Sasa mwaka huu vijana wamemchukulia yule kijana kama role model wao then kuchora kwingi. Sasa waandishi wameripoti vile vielelezo alivyovitoa yule mkurugenzi ambayo pia ni journalism. Clouds ni radio ya MABWEGEEEEEEE

Mimi nikisema hao Clouds wanapromote ufreemason nchi nzima watu wananuna
 
Mpango na mkakati wa makusudi kuonyesha umma kwamba kufeli kwa wanafunzi si kwa sababu ya mazingira mabovu ya kazi, mazingira mabovu ya kutolea elimu na ukosefu wa vifaa vya elimu.

Wanataka kuaminisha umma kwamba wanafunzi hawa waliofeli wameonewa na baraza la mitihani

Kwamba baraza la mitihani limechanganya changanya matokeo na kuwafelisha wengine makusudi.

Pengine haya yote ni kutaka kuhalalisha maamuzi ya kufunika kombe mwanaharamu apite, yanayozungumzwa kwamba wanafuzni waliofeli warudie mitihani kwa gharama za serikali.

1. Waliofeli wote warudie mitihani kwa gharama za serikali kwa sababu NECTA ni chombo cha serikali na ndio kimefanya uzembe au kuwafelisha kwa makusudi.

2. Kuhakikisha Mkurugenzi wa NECTA anaandamwa na hata kutolewa kafara kuonyesha serikali imechukua hatua.

Je ni sahihi kutumia kiasi kikubwa cha kodi za wananchi kwa ajili ya maamuzi yasiyotegemewa kubadili uhalisia wa ufaulu?.

Serikali itagharamia pia maandalizi na mafunzo ya hawa wanafunzi?

Je watalazimisha wanafunzi watakaofanya mitihani ya marudio wapewe ufaulu usiostahili kwa maslahi ya kisiasa?

Je huu uamuzi ni sahihi kwa maslahi ya nchi?.

Tafakari
 
Huyu mkurugenzi hana nidhamu hata kama ingekuwa ni kweli necta walikosea ilibidi afuate chain nzuri yeye akiwa kama mdau wa elimu ili kujua tatizo kabla hajakimbilia kwenye vyombo vya habari kupotosha uma kuhusu necta.mimi nadhani serikali ifike sehemu ichunguze na itengeneze mfumu sawa kwenye elimu..Hawa watu wanaojiita WAKURUGENZI,NA MAMENEJA Kwenye shule wanatoka wapi?kwa maana nyingine hizi ni kampuni na kampuni zipo kibiashara zaidi.Hii inadhibitishwa na baadhi ya wakurugenzi hao kuchukua matokeo ya mitihani na kuyatangaza kwenye vyombo vya habari ili wapate wateja.hii ni hatari miaka ya nyuma walikuwa wanafanya mbinu za kuiba mitihani ili shule zao zionekane zipo juu lakina baada ya mama NDALICHAKO kujitahidi kupunguza wizi huo kwakiwango kikubwa sasa wanajaribu kutafuta kila aina ya mbinu chafu ili kumharibia mama huyu aondolewe ili waendelee na mbinu zao chafu.nNDALICHAKO SONGA MBELE USIBABAISHWE
 
Huyu mkurugenzi nae hamnazo kabla ya kupublicise si angecheki na NECTA sasa aibu imemkumba
Vijana wa kitaa husema mtu mzima hovyooooooooooooo
 
Ajabu tu Tanzania; vilaza wanamiliki shule za sekondari hadi wageni wanaona wawapatie shahada za uzamivu kwa ujasiri wao.
 
Huyu mkurugenzi hana nidhamu hata kama ingekuwa ni kweli necta walikosea ilibidi afuate chain nzuri yeye akiwa kama mdau wa elimu ili kujua tatizo kabla hajakimbilia kwenye vyombo vya habari kupotosha uma kuhusu necta.mimi nadhani serikali ifike sehemu ichunguze na itengeneze mfumu sawa kwenye elimu..Hawa watu wanaojiita WAKURUGENZI,NA MAMENEJA Kwenye shule wanatoka wapi?kwa maana nyingine hizi ni kampuni na kampuni zipo kibiashara zaidi.Hii inadhibitishwa na baadhi ya wakurugenzi hao kuchukua matokeo ya mitihani na kuyatangaza kwenye vyombo vya habari ili wapate wateja.hii ni hatari miaka ya nyuma walikuwa wanafanya mbinu za kuiba mitihani ili shule zao zionekane zipo juu lakina baada ya mama NDALICHAKO kujitahidi kupunguza wizi huo kwakiwango kikubwa sasa wanajaribu kutafuta kila aina ya mbinu chafu ili kumharibia mama huyu aondolewe ili waendelee na mbinu zao chafu.nNDALICHAKO SONGA MBELE USIBABAISHWE
Wanasheria wanaandaa mashtaka dhidi ya Bujugo ya kuchafua jina la NECTA.
 
Pamoja sana mpaka mwisho wa dahari mkuu

Hivi kati ya Clouds na Kawambwa anayeharibu wanafunzi na kusababisha matokeo mabaya ni nani manake nawashangaa sana wanaoitisha maandamano kumkomalia Kawambwa ajiuzulu badala ya kudai Clouds ifungiwe kwa kuharibu wanafunzi; eti ooh sijui after school bash, mara ooh bush party, mara ooh mashindano ya vitoto kucheza au kuimba, nk ama kweli nyani haoni kundule.
 
This is very unprofessional.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Hivi kati ya Clouds na Kawambwa anayeharibu wanafunzi na kusababisha matokeo mabaya ni nani manake nawashangaa sana wanaoitisha maandamano kumkomalia Kawambwa ajiuzulu badala ya kudai Clouds ifungiwe kwa kuharibu wanafunzi; eti ooh sijui after school bash, mara ooh bush party, mara ooh mashindano ya vitoto kucheza au kuimba, nk ama kweli nyani haoni kundule.
Hii radio ingekuwa amri yangu ingefutwa, sio sherehe na matukio tu kwaajili ya wanafunzi bali hata kuharibu lugha, kuwazawadia wanafunzi wanaofanya vibaya na kuwapopurize kama yule wa mwaka jana, vijana kuacha shule na kuwainingiza kwenye the so-called THT, kunyonya na kuwaangusha wasanii makusudi kabisaaa hasa wale WENYE UWEZO MKUBWA WA KUFIKIRI, NK. Halafu wajinga wanapojifanya wa akili zaidi ya mwenye nazo inanikera sana, HAPA NATUMIA MSEMO WA MHESHIMIWA CHG ALIPOMQUOTE SIMKUMBI NANI ALISEMA "inakera sana pale akili ndogo inapotawala akili KUBWA" Sasa hawa clouds na ujinga wao wote eti wao ndio wajanja wa mjini hapa na wanajua kila kitu wakti ni MBUMBUMBU.
 
Bujugo ni mfanyabiashara kama wengine wasiopenda kusikia wala kupata hasara kwenye biashara anayoiendesha. Ni mtu mhuni tu ambae kaamua kutoa habari kwa vyombo vya habari ambavyo si makini ili wazazi waliowahi kuwa na imani na shule zake wachanganyikiwe. Nasema tena, mfanyabiashara hutakiwi kuingilia utaratibu wa shughuli za shule we imiza elimu bora na standards. Sasa bujugo this time kashindwa kununua mitihani na kuwapa wanafunzi wake na results zimetoka kulingana na elimu anayoitoa. Sasa kaanza visa. Always garbage in garbage out. Bujugo acha uhuni. Naomba kuanzia sasa hata registrar wa private schools aende mbele zaidi kabla ya kusajili manake si kila mwenye hela na majengo aruhusiwe kumiliki shule
 
Back
Top Bottom