NEEMA KUU: Bwawa la Nyerere kuzalisha umeme wenye thamani sawa na 50% ya makusanyo ya TRA nchi nzima, (Trillion 12 kwa mwaka)

sijasema kwamba hiyo pesa ni faida, nimesema kwamba ni thamani tu ya umeme utakaozalishwa nje ya ule ambao tunazalisha sasa hivi.

Weka risiti ya mwisho uliyonunua umeme, tuone bei uliyokatwa

Umeona hapo 20,000 unapata unit 56

20,000 gawanya 56 ni 357
Ukifanya kabla ya kodi hio 16,000 gawanya 56 ni kama 297

Hizo ndio gharama za umeme za Unit za kawaida kabla na baada ya Vat na Makato mengine.

Hivyo hio figure ya 600 ni Uongo, na mpaka umefikia hio figure kuna possibility kubwa wewe ni tegemezi unatupigia tu kelele humu.

Pia Kwenye Biashara huwezi tumia bei ya mwisho ya mlaji halafu ndio useme ni thamani ya Raw Material.

Leo nikienda Shamba la mpunga halafu nilipigie thamani kwa idadi ya sahani za wali za mama ntilie ni sahihi?
 
Calculations za kutosha utafikir wapo serious kutatua tatizo la umeme 🤣🤣🤣🤣. Bwawa litaanza still sarakas za umeme hazitoisha!! Tupo hapa...
 
Inategemea na kodi ya majengo umekatwa vipi. Kwa case yako wewe tufanye ni 400 kwa unit, kwa hesabu zile zile (400 / 600) ni 2/3 ya makadirio yangu ya awali, 2/3 ya 12 trillion ni Trillion 8 kwa mwaka..., twende na hiyo. Trillion 8 kwa mwaka.

Around 40% ya makusanyo yote ya TRA kwa mwaka mzima.

Pia sijasema hiyo ni faida, bali thamani ya umeme unaozalishwa.
 
TUna uhuni mwingi unaendelea kumbe

Mungu atuokoe
 
Hii ni taarifa nzuri kabisa, kwamba, Sasa kwa miezi 12 tunafanya mara 12, hivyo tutapata Trillion 12 kwa mwaka, ambayo ni 50% ya makusanyo yote ya TRA kwa mwaka mzima! Hakika 🙄uchumi unakuwa🤫 na ukijumulisha na zile $7billioni alizozidai Mh. January Makamba(Waziri) kuwa zitaingia kwenye Uchumi, basi afueni.

Sibishi. Ila, yote hayo yatageuka kuwa ni sufuri pale Mdubai atakapokuja kuendesha TANESCO?

Kwa lugha nyingine, mkae kuvurugwa Kisaikilojia, apparently, tena!
 
sijasema kwamba hiyo pesa ni faida, nimesema kwamba ni thamani tu ya umeme utakaozalishwa nje ya ule ambao tunazalisha sasa hivi.

Weka risiti ya mwisho uliyonunua umeme, tuone bei uliyokatwa

Kwenye Hesabu nilizoweka hakuna 400 hata moja umeitunga tena.

Nimekupa mfano shamba la mpunga na sahani ya Wali, huwezi kupima thamani ya Mpunga kwa market value ya sahani ya Wali kwa mama ntilie, huo mpunga unataka kukobolewa, usafirishwe, uende Kwa muuzaji wa Jumla, Rejareja, anunue Mama ntilie, apike etc.

Mambo ni hivyo hivyo kwa Hilo bwawa huo Umeme ukitengenezwa unapitia process kibao, unaweza kuta hapo thamani ya unit ni 20 ama 30 ila ukishapita process zote ndio unafika Hio 297.
 
Hiyo 400 nime-round off kurahisisha maelewano. Pia Sijasema hiyo ni faida au ni net, mimi naongelea kiasi cha pesa ambacho watu hutakiwa kulipa kwa kiwango tajwa cha uniti.
 
Mimi nimekuwa nanunua units 28 kwa shilingi 10,000. Which means each unit (1kwh) nanunua kwa sh 357.

Tueleze iyo tshs 600 per unit wewe umeitolea wapi?
 
Magu had a great vision
 
Unit moja ya umeme hapa Tanganyika ni 600/=
Duh hii ni bei ya kuzalisha unit Moja au bei tunayouziwa umeme na Tanesco? Unachanganya gharama za uendeshaji, bei ya kuuza, bei ya soko, thamani, Mapato, na faida!! Hivi vitu havifanani kabisa. Cha ajabu umepiga hesabu ya Mapato hujapiga hesabu ya gharama za uendeshaji Bwawa!! More over ume assume Bwawa litafanya kazi at excess capacity tokea siku ya kwanza mpka mwisho wa mwaka mmoja bila kuzimwa, bila maintenance, n.k
 
Hiyo ni bei, sio gharama, na ndicho ninachomaanisha, bei.
 
Hamna uzalishaji wa ivo😂 Machines zinapataga breakdown ya kutosha,kuna mda wa service na kubadili baadhi spare parts ambozo ni za kuagiza sasa ukipigia kwa kila siku ni uongo hai
 
Hamna udhakishaji waivo😂 Machine zinapataka breakdown ya kutosha,kuna mda wa service na kubadili baadhu spare part ambozi ni za kuagiza sasa ukipigia kwa kila siku ni uongo hai
Hata kama kuna breakdown, ila picha halisi kwa makadirio ndio hiyo.., haichezi mbali na hapo
 
Kwa makato hayo TANESCO katika elfu 20 yao ni 78% ambayo ni tsh 16,393.5

Bei ya unit 16,393.5/56.1 = 292.2

Market Unit price (292.2) = unit cost of production + profit margin.

Kwa hivyo umeme unaweza kuwa umezalishwa labda 250 per unit cost. Hiyo ni average cost of production maana wanavyanzo vingi vyenye costs tofauti.

Faida ya TANESCO hapo labda ni tsh 42.2 tu per unit na yenyewe ina profit tax ya 30%, wanabaki na tsh 29.4 profit after tax.

Ujinga sasa ni baada ya bwawa la Nyerere kuisha na kukizi mahitaji ya nchi; wameingia mikataba ya umeme ambayo ina unit costs za juu kwa manunuzi ya umeme ambayo hawana shida nayo. Wakati mwaka huu kwenye statement yao wamelipa karibu tsh 250 billion kwa sababu ya kununua umeme + na hayo malipo ya mbeleni waliojiongezea kwa mikataba isiyo na lazima na kujipunguzia mapato.

At the same time wao wenyewe kulipa madeni yao awawezi, revenue bado ndogo sana na other income imejaa magumashi tupu labda 40% of that is acceptable mengine ni utunzi hawana hiyo income in accordance with revenue recognition rules za IFRS.

Walau Maharage is honest and has good intentions na shirika, ila financial advisors hana na apunguze deal za waliomweka hapo Makamba na ‘bi tozo’ ndio chaka lao la kupiga hapo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…