Nelly, Chris Brown na Kerrueche wamshobokea Diamond

Nelly, Chris Brown na Kerrueche wamshobokea Diamond

Status
Not open for further replies.

warumi

R I P
Joined
May 6, 2013
Posts
16,218
Reaction score
18,440
Staa wa Bongo Fleva ambaye kwa sasa anafanya kweli kimataifa, Nasibu Abdul ' Diamond Platnumz ' ameandika historia kwenye Tuzo za Black Entertainment Television ( BET) 2014 huku akiwatia kiwewe mastaa wakubwa kama Cornell Iral Haynes ' Nelly ' , Christopher Maurice ' Chris Brown' na wengine kibao.

Tukio hilo lilijiri usiku wa kuamkia Jumatatu wiki hii kwenye Ukumbi wa Nokia Theatre jijini Los Angeles , Marekani ambapo Diamond alikuwa ameteuliwa kuwania Kipengele cha Mwanamuziki Bora kutoka Afrika akiwa sambamba na mwanamuziki Davido ( Nigeria ) , Mafikizolo ( Afrika Kusini) , Tiwa Savage ( Nigeria ) , Toofan ( Togo ) na Sarkodie ( Ghana) .

TUZO YAENDA KWA DAVIDO

Tuzo hiyo haikuwa bahati kwa Diamond kwani ilikwenda kwa Davido . Licha ya kukosa tuzo hiyo , yapo mengi ambayo Diamond ameweka historia au rekodi katika ' event' huku kuunganishwa na mastaa hao ikiwa topiki muhimu.

MCHUMBA WA CHRISS BROWN AMSHOBOKEA

Katika hali ya kushangaza, mwanamitindo maarufu Marekani ambaye ni mchumba wa Chris Brown, Karrueche Tran alionekana kumshobokea Diamond mara alipokutana naye uso kwa uso.

Karrueche alijikuta hajiwezi alipokuwa akimhoji Diamond ambapo moja kwa moja alimvutia kipaza sauti na kuanza kumpiga maswali huku akionesha kuvutiwa naye kwa muonekano aliokuwa nao .

Akihojiwa na demu wa Chris Brown. Karrueche alikuwa akijichekeshachekesha huku akimhoji kuhusiana na mwanamuziki ambaye Diamond anamkubali ambapo alijibu ni Chris Brown, wote wakajikuta wakiangua kicheko.

Kana kwamba hiyo haitoshi , Karrueche muda wote aliendelea kumshangaa na mwisho wa siku wakabadilishana namba za simu.

MASTAA MACHO JUU

Ulipofika wakati wa utoaji tuzo katika kategori ya Mwanamuziki Bora kutoka Afrika, lilipotajwa tu jina la Diamond kutoka Tanzania na wimbo wake wa Number One RMX , mastaa kibao walionesha kushangaa na ndipo macho yote yakahamia eneo aliokuwa amekaa.

Wengi walionekana kutoa maneno ya chinichini sambamba na kumuoneshea vidole wakionesha kumkubali kwa kutinga mjengoni hapo.

NELLY, CHRIS BROWN WAINGIWA KIWEWE

Wakati Diamond anaingia ukumbini , mastaa mbalimbali duniani walionekana kumshangaa na kati yao alikuwa ni Nelly ambaye aliushikilia mkono wa Diamond kwa sekunde kadhaa akitaka waendelee kupiga stori. Diamond akiwa kwenye pozi Wakiwa katika zulia maalum jekundu , Nelly aliyewahi kutamba na wimbo wake maarufu wa Dilemma alionekana na kutaka kumfahamu zaidi Diamond .

Kila sehemu aliyokuwa akienda , Nelly hakutaka kumuacha na alionekana kuambatana naye kwa kumng'ang'ania mkono kila kona akipiga naye picha na kuzunguka eneo lote wakiwa pamoja.

Naye Chris Brown ambaye aliangusha bonge la shoo alionekana kumshangaa Diamond huku akitamani kuendelea kukaa naye.

Kwa mujibu wa shuhuda wetu ukumbini humo , maswali mengi yaliibuka kuwa iweje , kwa Mtanzania kama yule kukanyaga katika mjengo mmoja na mstaa wa dunia.

TYSON , MAYWEATHER WADUWAA

Mabondia maarufu duniani akiwemo Floyd Mayweather na Mike Tyson walijikuta wakiduwaa kwa kumshangaa kwa kila hatua aliyokuwa anapiga.Macho yao hayakuwa mbali naye na hata katika zulia jekundu , Maywearher , baada ya kumaliza kupiga picha akiwa na mkewe alimfuata.

MASTAA KIBAO WAGOMBEA NAMBA


Wakati shoo hiyo ikiendelea baadhi ya msataa waliokuwa pembeni na Diamond walionekana kumfagilia na hata wengine kuomba namba za simu kwa malengo tofauti ikiwa ni pamoja na kutaka kufanya naye kolabo katika siku za usoni.
 
habari yako ni ya kweli hata Christian Ronaldo anamshobokea mrisho ngasa, na hata mimi nilipofika ulaya kuanzia cabin crews wa kike mpaka wauza maduka ya nguo na super market wote walikuwa wananishobokea kila nikiingia kwenye maduka yao kwa tabasamu bashasha.
 
Naona mmeshakosa tuzo mnaaanza kujifariji na uongo...ok uongo mwema..lkn mtandanganya hao hao shuleless..!
 
Last edited by a moderator:
Hongera zake kaka diamond

Huyo mussa mateja atakuwa na mapepo, jamani ndo ametufanya watanzania wajinga ivi? Hawa waandishi wa shigongo sio wazima, sasa nani alisema akina chriss brown wamemuomba namba ndomo au akina nelly ndo wamemwambia shigongo? Wapuuzi sana hawa eti wamemwomba afanye collabo mmh kaz ipo
 
Ha ha ha nipo marekani hata promo hakupata na watu hawamjui khaaah

Huyo dogo anaharibiwa kwa kupewa Sifa za kishenzi na akina Ruge..
Shigongo and the likes...

He is too low!!!
 
habari yako ni ya kweli hata Christian Ronaldo anamshobokea mrisho ngasa, na hata mimi nilipofika ulaya kuanzia cabin crews wa kike mpaka wauza maduka ya nguo na super market wote walikuwa wananishobokea kila nikiingia kwenye maduka yao kwa tabasamu bashasha.

Mkuu mbona siku hizi humpambi au dadako wema kaachwa?
 
huyo mussa mateja atakuwa na mapepo, jamani ndo ametufanya watanzania wajinga ivi? Hawa waandishi wa shigongo sio wazima, sasa nani alisema akina chriss brown wamemuomba namba ndomo au akina nelly ndo wamemwambia shigongo? Wapuuzi sana hawa eti wamemwomba afanye collabo mmh kaz ipo
mkuu hii habari umeleta wewe tena unaipinga!
 
Huyo mussa mateja atakuwa na mapepo, jamani ndo ametufanya watanzania wajinga ivi? Hawa waandishi wa shigongo sio wazima, sasa nani alisema akina chriss brown wamemuomba namba ndomo au akina nelly ndo wamemwambia shigongo? Wapuuzi sana hawa eti wamemwomba afanye collabo mmh kaz ipo

wamekosa story za mafumanizi naona wako wanaokoteza habari
 
blog za fb zimejaa habari hii
 
Diamond ile ya kwenye blood diamond au diamond ya mwadui..???


Sent from my Philips.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom