Nembo ya Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam na maneno yaliyoko katika logo hiyo ni vitu vya kutazamwa upya kwani viko kisiasa zaidi kuliko kitaaluma

Nembo ya Chuo Kikuu cha Dar-es-Salaam na maneno yaliyoko katika logo hiyo ni vitu vya kutazamwa upya kwani viko kisiasa zaidi kuliko kitaaluma

Habari wakuu,

Binafsi napenda kushauri viongozi wa Chuo hiki kuitazama upya nembo ya chuo kama kweli nembo hiyo inastahili kubaki kama ilivyo au ifanyiwe marekebisho madogo ili iwezeke kusadifu zaidi maswala ya academic kuliko ilivo sasa ambapo,kwa mtazamo wangu,inasadifu zaidi siasa za miaka ya nyuma.

Naposema imekaa kisiasa zaidi simanishi haibebi ujumbe wowote wa kitaaluma, bali ni kwasababu imetoa nafasi kubwa kwa maswala ya kisiasa {mchoro wa Mwenge} kwenye nembo huku mchoro wa kitabu ukipewa nafasi ndogo wakati kazi ya msingi ya chuo ni kuzalisha wataalamu.

Nachojiuliza,mchoro wa Mwenge kwenye nembo ya taasisi inayotoa taaluma inasaidifu nini? Inawezekana nembo ya chuo hiki ni ile ile tangu uhuru hivyo kwa wakati huo, labda kulikuwa na sababu ya kuweka mchoro wa mwenge katika nembo ya chuo ila sidhani kama ni sahihi kuendelea kuwa na mchoro huo kwa wakati tulionao.

Ukiacha mbali swala la mchoro huo wa mwenge,hata maneno yaliyoko katika slogan hiyo nayo sidhani kama yana uhusiano wowote na chuo hicho ambacho kazi yake kubwa ni kuzalisha wataalam(wasomi).

Maneno yaliyoko katika nembo hiyo ni haya:hekima ni uhuru.

Nembo husika ni hii:


Kwa maneno hayo ambayo bila shaka ndio kauli mbiu ya chuo,ni wazi yanaturudisha kule kule kwenye mchoro wa mwenge wa uhuru jambo linalonifanya nijiulize ilitokea tu kama coincedence au ni jambo lililokuwa limekusudiwa?

Nadhani wakati umefika nembo hii itazamwe upya na ifanyiwe marekebisho madogo ingawa jambo hili nalo linaweza kuwa na changamoto zake ingawa sitaki kuamini changamoto hizo ndio zinaweza kuwa kikwazo zaidi tu ya kukosekana dhamira ya kuifanyia mabadiliko nembo hiyo na pengine ni kwakuwa tumeridhika nayo,tumeizoea na hatuoni kasoro yoyote katika hiyo nembo.

Hembu tazameni nembo ya chuo hki kichanga lakini inayosadifu zaidi taaluma kuliko mambo mengine yote katika nembo hiyo bila kusahau uchaguzi mzuri wa maneno yaliyowekwa katika nembo husika.


Jambo hili inawezekana liko hata katika taasisi nyingine lakini haimanishi tukae kimya.

Kama wahusika mpo humu,basi tupeni ufafanuzi wa hiyo logo na hiyo kauli mbiu(moto) labda tunaweza kuelewa.
Hivi hii nembo ndiyo inawazuia msiingie Ikulu? By the way kila siku nyie ni mambo ya kupinga tu hapa JF
 
MTOA MADA NI MMOJA KATI YA WAPUMBAVU (BONGOLALA). HIYO LOGOS YA TUMAINI NYOKA ANAMAANISHA NINI?
 
Una tatizo tu na mwenge,halafu nembo haisomeshi wala kukupunguzia akili
Mwenge maana yake ni taa,mwangaza nuru,ukisoma pale utaelimika na kupata mwanga zaidi wa kimaisha
Kiufupi ni kwamba mwenge wa UDSM utakutoa kwenye giza nene la kielimu na kifikra
Sasa wewe unaleta nembo ya tumaini,kwamba inasadifu zaidi taaluma,wasio wafuasi wa kristo watakwambia msalaba kwao ni tatizo,usitegemee chuo cha taifa kikaweka msalaba kwenye logo yake kamanda
Kina Zitto na lissu wametokana na mwenge huo huo
 
Naomba nitofautiane na wewe; lengo la msingi la chuo kikuu ni kupata KNOWLEDGE not WISDOM! Ni kupata MAARIFA sio HEKIMA! Hakuna mahali popote darasani uliwahi kukaa ili ufundishwe HEKIMA; tunaingia darasani kupata MAARIFA. Huwezi kuniambia wote ambao hawajafikia elimu ya chuo kikuu au ambao hawajasoma (darasani) kabisa hawana HEKIMA!

"Where is the wisdom we have lost in knowledge? Where is the knowledge we have lost in information?" —T.S. Eliot. Knowledge is gathered from learning and education, while most say that wisdom is gathered from day-to-day experiences and is a state of being wise. Knowledge is merely having clarity of facts and truths, while wisdom is the practical ability to make consistently good decisions in life.
Maarifa ya sahihi ya kutosha ndio hiyo inayo itwa HEKIMA.
Unaweza kufanya maamuzi sahihi kama una maarifa sahihi ya kitu unacho taka kufanyia maamuzi.

Ukifanya kitu vibaya unaonekana umefanya jambo bila kutumia hekima. Ukianza kupigna na mtu adharani sababu kakukosea wakati ipo sheria inayoweza kumuadhibu mkosaji wako unanekana hauna hekima.
Hekima hapo ni nini? Ni kukosa maarifa ya namna ya kumuadhibu au kumrekebisha mkosaji wako bila madhara makubwa kwako au kwa jamii.
 
Kwa nini unaamini kwamba huo ni mwenge wa uhuru? Kama ni kweli basi uko sawa.

Lakini pengine huo ni mwanga wa kawaida ukiakisi ukipata elimu umepata mwanga.


Kwa nini maneno yawe na shida.

Hekima ni uhuru. Kwa maana nyingine Elimu bila hekima ni bure.
 
Knowledge is merely having clarity of facts and truths, while wisdom is the practical ability to make consistently good decisions in life.
Jamani....!!! How can you be practically able to make consistent good decisions without having clarity of facts and truths on the situation in hand? "There is no wisdom based on mere intuitions" by TUJITEGEMEE on 17/02/2020.
 
Naomba nitofautiane na wewe; lengo la msingi la chuo kikuu ni kupata KNOWLEDGE not WISDOM! Ni kupata MAARIFA sio HEKIMA! Hakuna mahali popote darasani uliwahi kukaa ili ufundishwe HEKIMA; tunaingia darasani kupata MAARIFA. Huwezi kuniambia wote ambao hawajafikia elimu ya chuo kikuu au ambao hawajasoma (darasani) kabisa hawana HEKIMA!

"Where is the wisdom we have lost in knowledge? Where is the knowledge we have lost in information?" —T.S. Eliot. Knowledge is gathered from learning and education, while most say that wisdom is gathered from day-to-day experiences and is a state of being wise. Knowledge is merely having clarity of facts and truths, while wisdom is the practical ability to make consistently good decisions in life.
Descartes
“Through wisdom, we hear not only prudence in business, but a perfect knowledge of all things that man can know, both the conduct of his life by preserving his health and the invention of all arts. ”

Aristotle
“The wise man has the knowledge of all things, insofar as possible”

Heraclitus
“Wisdom is one thing. It is to know the thought by which all things are led by all things

Utaona hao wana falsafa wote wanasema wisdom ni maarifa ya vitu vyote.
Na maarifa (knowledge) umesema ndio hupatikana kwenye mojawapo ya kazi za vyuo vikuu.

Jee huyo T.S. Eliot anaweza kuwa challenge hao philosophers?
 
Ukiacha tafsiri iliyojificha, hata tafsiri ya moja kwa moja bado ina mashiko kwa huo moto wa UDSM. Tukumbuke hicho chuo kimeanzishwa mwaka 1961, mwaka tuliopata uhuru. Pia, ni chuo kilichoongoza mijadala ya harakati za uhuru Africa. Kina Walter Rodney hawakuja Tanzania (na kufanya kazi UDSM) kuchoma mahindi, walikuja sababu UDSM ilikuwa tanuru la fikra.

Hata ukichukua maana iliyojificha, bado moto huo una maana kwa taasisi za elimu ya juu. Chuo kikuu hakuna NECTA, wigo wa kujipatia maarifa na hekima umepanuliwa sana tofauti na shule za sekondari. Mtu yuko huru kufikiri tofauti, ili mradi tu awe na hoja za kutetea anachoamini. Elimu ya chuo kikuu inakupa hekima ya kujua baya na jema ktk maisha, kwahiyo unakuwa huru. Hufungwi na danganya toto za watawala wala sheria zao mbaya. Hufungwi na tamaduni zilizopitwa na wakati, uko huru kuwaza na kutenda kinyume na tamaduni maana umepewa hekima ya kujua lililo jema.

Mwisho, sio haki kukiweka UDSM na Tumaini Makumira ktk sentensi moja. Huo utakuwa ukoo wa Kambale, mtoto, mama na baba wote wana ndevu. Makumira kuwa na moto wa Teaching, Research and Service ni sawa na kusema kazi ya mama mzazi ni kuzaa-stating the obvious.
 
Ukiacha tafsiri iliyojificha, hata tafsiri ya moja kwa moja bado ina mashiko kwa huo moto wa UDSM. Tukumbuke hicho chuo kimeanzishwa mwaka 1961, mwaka tuliopata uhuru. Pia, ni chuo kilichoongoza mijadala ya harakati za uhuru Africa. Kina Walter Rodney hawakuja Tanzania (na kufanya kazi UDSM) kuchoma mahindi, walikuja sababu UDSM ilikuwa tanuru la fikra.

Hata ukichukua maana iliyojificha, bado moto huo una maana kwa taasisi za elimu ya juu. Chuo kikuu hakuna NECTA, wigo wa kujipatia maarifa na hekima umepanuliwa sana tofauti na shule za sekondari. Mtu yuko huru kufikiri tofauti, ili mradi tu awe na hoja za kutetea anachoamini. Elimu ya chuo kikuu inakupa hekima ya kujua baya na jema ktk maisha, kwahiyo unakuwa huru. Hufungwi na danganya toto za watawala wala sheria zao mbaya. Hufungwi na tamaduni zilizopitwa na wakati, uko huru kuwaza na kutenda kinyume na tamaduni maana umepewa hekima ya kujua lililo jema.

Mwisho, sio haki kukiweka UDSM na Tumaini Makumira ktk sentensi moja. Huo utakuwa ukoo wa Kambale, mtoto, mama na baba wote wana ndevu. Makumira kuwa na moto wa Teaching, Research and Service ni sawa na kusema kazi ya mama mzazi ni kuzaa-stating the obvious.
Hiyo hidden mining unayoiongelea bado hainishawashi na ninaamini siasa ndio ilitumika/ ili-influence katika kubuni hiyo logo miaka hiyo ya sisi kupata uhuru.
 
Kama alivyobainisha kwa usahihi ndugu Sooth hapo juu, UDSM ilianzishwa katika mazingira mahususi ya kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni.

Miaka ya mwanzoni mwa 1960, waasisi, pamoja na mambo mengine, waliichukulia elimu ya Chuo Kikuu kama nyenzo muhimu katika kuandaa rasilimali watu bora - yenye ujuzi, maarifa na uzoefu - katika fani mbalimbali, kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu.

Watu walioelimika vyema, ni dhahiri, wangeonyesha kiwango cha juu cha hekima na wangekuwa huru dhidi ya ujinga, maradhi, umaskini na hatimaye kuchangia katika kupiga vita vitisho vya ukoloni mamboleo vya ndani na nje ya nchi.

Kwa sababu hiyo, logo ya UDSM imeakisi, inaendelea kuakisi na hapana shaka itaendelea kuakisi ndoto na matarajio ya waanzilishi wake.
 
Habari wakuu,

Binafsi napenda kushauri viongozi wa Chuo hiki kuitazama upya nembo ya chuo kama kweli nembo hiyo inastahili kubaki kama ilivyo au ifanyiwe marekebisho madogo ili iwezeke kusadifu zaidi maswala ya academic kuliko ilivo sasa ambapo,kwa mtazamo wangu,inasadifu zaidi siasa za miaka ya nyuma.

Naposema imekaa kisiasa zaidi simanishi haibebi ujumbe wowote wa kitaaluma, bali ni kwasababu imetoa nafasi kubwa kwa maswala ya kisiasa {mchoro wa Mwenge} kwenye nembo huku mchoro wa kitabu ukipewa nafasi ndogo wakati kazi ya msingi ya chuo ni kuzalisha wataalamu.

Nachojiuliza,mchoro wa Mwenge kwenye nembo ya taasisi inayotoa taaluma inasaidifu nini? Inawezekana nembo ya chuo hiki ni ile ile tangu uhuru hivyo kwa wakati huo, labda kulikuwa na sababu ya kuweka mchoro wa mwenge katika nembo ya chuo ila sidhani kama ni sahihi kuendelea kuwa na mchoro huo kwa wakati tulionao.

Ukiacha mbali swala la mchoro huo wa mwenge,hata maneno yaliyoko katika slogan hiyo nayo sidhani kama yana uhusiano wowote na chuo hicho ambacho kazi yake kubwa ni kuzalisha wataalam(wasomi).

Maneno yaliyoko katika nembo hiyo ni haya:hekima ni uhuru.

Nembo husika ni hii:


Kwa maneno hayo ambayo bila shaka ndio kauli mbiu ya chuo,ni wazi yanaturudisha kule kule kwenye mchoro wa mwenge wa uhuru jambo linalonifanya nijiulize ilitokea tu kama coincedence au ni jambo lililokuwa limekusudiwa?

Nadhani wakati umefika nembo hii itazamwe upya na ifanyiwe marekebisho madogo ingawa jambo hili nalo linaweza kuwa na changamoto zake ingawa sitaki kuamini changamoto hizo ndio zinaweza kuwa kikwazo zaidi tu ya kukosekana dhamira ya kuifanyia mabadiliko nembo hiyo na pengine ni kwakuwa tumeridhika nayo,tumeizoea na hatuoni kasoro yoyote katika hiyo nembo.

Hembu tazameni nembo ya chuo hki kichanga lakini inayosadifu zaidi taaluma kuliko mambo mengine yote katika nembo hiyo bila kusahau uchaguzi mzuri wa maneno yaliyowekwa katika nembo husika.


Jambo hili inawezekana liko hata katika taasisi nyingine lakini haimanishi tukae kimya.

Kama wahusika mpo humu,basi tupeni ufafanuzi wa hiyo logo na hiyo kauli mbiu(moto) labda tunaweza kuelewa.
Ni kawaida ya watu wavivu wanapokuwa kwenye hali ngumu (kwa ajili ya uvivu wao) hujaribu kutafuta visingizio vya kila aina ili tu ionekana tatizo siyo wao bali linaletwa na kitu kingine. Hata ungekuwa na nembo ya aina gani kama hufanyi kazi kwa bidii na maarifa ni bure tu.
 
Ni kawaida ya watu wavivu wanapokuwa kwenye hali ngumu (kwa ajili ya uvivu wao) hujaribu kutafuta visingizio vya kila aina ili tu ionekana tatizo siyo wao bali linaletwa na kitu kingine. Hata ungekuwa na nembo ya aina gani kama hufanyi kazi kwa bidii na maarifa ni bure tu.
Huu utumbo mpelekeo mkeo akakupikie sio kutuletea hapa mtandaoni.
 
Kama alivyobainisha kwa usahihi ndugu Sooth hapo juu, UDSM ilianzishwa katika mazingira mahususi ya kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni.

Miaka ya mwanzoni mwa 1960, waasisi, pamoja na mambo mengine, waliichukulia elimu ya Chuo Kikuu kama nyenzo muhimu katika kuandaa rasilimali watu bora - yenye ujuzi, maarifa na uzoefu - katika fani mbalimbali, kwa ajili ya maendeleo ya taifa letu.

Watu walioelimika vyema, ni dhahiri, wangeonyesha kiwango cha juu cha hekima na wangekuwa huru dhidi ya ujinga, maradhi, umaskini na hatimaye kuchangia katika kupiga vita vitisho vya ukoloni mamboleo vya ndani na nje ya nchi.

Kwa sababu hiyo, logo ya UDSM imeakisi, inaendelea kuakisi na hapana shaka itaendelea kuakisi ndoto na matarajio ya waanzilishi wake.
Bado nasisitiza mjitafakari kuhusu hiyo logo yenu.
 
Mkuu Salary Slip, mimi si mwanafunzi wala mtumishi wa UDSM; sipo katika nafasi ya kukataa ama kukubali mawazo yako. Maoni yangu ni matokeo ya matumizi ya uhuru na haki zangu za kuwa na maoni na kujieleza.

Hata hivyo, kama mwanafunzi wa zamani wa UDSM, nakumbuka vizuri jinsi logo hiyo, hususani maneno 'hekima ni uhuru' - katika fomu za usajili wa mihula, prospectus, karatasi za mitihani na nyaraka na maeneo mengine muhimu - yalivyokuwa yananikumbusha: umuhimu wa kutafuta, kuwasilisha na kusimamia ukweli; na kudhihirisha hekima kupitia matendo na maneno.

Chuo husika bado kinakabiliwa na vikwazo vingi katika kutoa huduma bora na endelevu kwa wadau wake. Sidhani kama logo ni kikwazo kimojawapo.

Hata hivyo, huenda, hatimaye, wahusika wakatafuta mantiki katikati ya michango yetu.
 
Watu wanasema Tanzania tunatumia mwenge, mwenge ni agano la kishetani na ndio maana nchi yetu maskini.
Naomba niwaulize mbona Marekani wanatumia hiyo alama ya mwenge kwenye ile sanamu kubwa inayoitwa The Statue of Liberty kwanini wao hawajalaaniwa na kubaki maskini.

Pia naomba niulize wale wanao jinadi kupigania Uhuru na Demokrasia huku wakipinga mwenge kwa vigezo vya kidini, kwanini wanafungwa na imani za kidini?
Kwanini serikali ilazimishwe kuamini mambo ya kidini? Uhuru na haki viko wapi hapo kwa maana kuna watu wasio amini ktk mambo ya dini zinazo sema mwenge ni laana au agano na shetani.

Uhuru kamili wa taifa lolote huja kwa kuzingatia kutenganisha dola na dini (Separation of religion and state) na hiyo ndio demokrasia na kutenda haki kwa makundi yote..
 
Back
Top Bottom