NEMC: Huku Mitaani Tunateseka Kelele za Miziki Bar Zimezidi

NEMC: Huku Mitaani Tunateseka Kelele za Miziki Bar Zimezidi

Faana

JF-Expert Member
Joined
Dec 12, 2011
Posts
38,657
Reaction score
44,759
Naandika kwako Mkurugenzi wa NEMC - HQ kwamba huku mitaani hasa katika miji kelele za miziki kwenye ma bar, pub saloon za vinyozi, wauza CD, vigodoro pamoja na nyumba za ibada zimekuwa kero kiasi kwamba Mamlaka yako inaonekana ipo tu kama bendera inatumia fedha za serikali bila tija. Kuna namba za simu 0800110115 imekuwa ukipiga kutoa taarifa hazina msaada wowote, wanaokuwa directed kushughulikia kero hawana hata kipimo cha kupimia uzito wa kelele.

Nakushauri utengeneze kikosi kazi cha kitaifa, kazi yake iwe kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi na kuyafanyia kazi moja kwa moja kutokea ofisini kwako kwasababu wawakilishi wenu walioko kwenye miji hawafanyii kazi kero wanazopelekewa kutokana na kupokea rushwa.

Ikiwa kikosi kazi chako kitakuwa na ufanisi, upo uwezekano wa NEMC kukusanya fine kwa wingi kutoka kwa wavunja sheria hao na kuiongezea serikali mapato.

Kiuhalisia hali ilivyo hivi sasa ni kama Mamlaka yako haipo, na kama ipo basi watendaji wako wameshindwa kazi kabisa.

Tunaomba ulichukulie suala hili kwa uzito wake.

Nawasilisha
 
Nemc ni moja ya mashiriki yenye wafanyakazi wasio natija nchi hii..wapo kula hela za walipakodi tu..hakuna ufanisi..na kungangania hela za eia tu..nchi inageuka jangwa wapo tu wamekalia matako maofisini mwao..uchafuzi wa mazingira kila siku unaongezeka..mifuko laini ya plastik inarudi kwa kasi..hopeless authority.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naandika kwako Mkurugenzi wa NEMC - HQ kwamba huku mitaani hasa katika miji kelele za miziki kwenye ma bar, pub saloon za vinyozi, wauza CD, vigodoro pamoja na nyumba za ibada zimekuwa kero kiasi kwamba Mamlaka yako inaonekana ipo tu kama bendera inatumia fedha za serikali bila tija. Kuna namba za simu 0800110115 imekuwa ukipiga kutoa taarifa hazina msaada wowote, wanaokuwa directed kushughulikia kero hawana hata kipimo cha kupimia uzito wa kelele.

Nakushauri utengeneze kikosi kazi cha kitaifa, kazi yake iwe kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi na kuyafanyia kazi moja kwa moja kutokea ofisini kwako kwasababu wawakilishi wenu walioko kwenye miji hawafanyii kazi kero wanazopelekewa kutokana na kupokea rushwa.

Ikiwa kikosi kazi chako kitakuwa na ufanisi, upo uwezekano wa NEMC kukusanya fine kwa wingi kutoka kwa wavunja sheria hao na kuiongezea serikali mapato.

Kiuhalisia hali ilivyo hivi sasa ni kama Mamlaka yako haipo, na kama ipo basi watendaji wako wameshindwa kazi kabisa.

Tunaomba ulichukulie suala hili kwa uzito wake.

Nawasilisha
Ungetaja jina la bar na kanisa. Kimara tumewakomesha wajinga fulani wanajiita LA CASA PUB walikuwa wajinga sana kelele mtindo mmoja kisa ilikuwa sijui na mahusiano na Kitila Mkumbo. Hawa wenye hizi bar hawaheshimu kbs afya ya masikio. Paza sauti.
 
Asilimia kubwa ya watendaji kwenye hizi Mamlala za Serikali wanatekeleza majukumu yao kwa kuangalia maslahi yao Binafsi. Kama suala halina maslahi kwao, sahau kuhusu wao kuhangaika nalo..!
 
Kama Sinza na Kijitonyama ni balaa. Hakuna utaratibu kabisa
 
Kibongo bongo asilimia kubwa ya watumishi wa serikali wakipiga hela zao tu za madili kitu cha kwanza kuwekeza ni vi grocery na bar. Sasa unategema watu kama hao wasimamie kelele za bar ikiwa wana maslahi ya moja kwa moja.

Kama sio wamiliki wa hizo bar basi ni wateja wakuu wa bar hizo.
 
Maisha ya kiafrika hayo ni shida tupu sijui tumeumbwaje kuna hatari watu kuwa nusu viziwi.
 
Ungetaja jina la bar na kanisa. Kimara tumewakomesha wajinga fulani wanajiita LA CASA PUB walikuwa wajinga sana kelele mtindo mmoja kisa ilikuwa sijui na mahusiano na Kitila Mkumbo. Hawa wenye hizi bar hawaheshimu kbs afya ya masikio. Paza sauti.
Barikiwa mkuu
 
Nemc ni moja ya mashiriki yenye wafanyakazi wasio natija nchi hii..wapo kula hela za walipakodi tu..hakuna ufanisi..na kungangania hela za eia tu..nchi inageuka jangwa wapo tu wamekalia matako maofisini mwao..uchafuzi wa mazingira kila siku unaongezeka..mifuko laini ya plastik inarudi kwa kasi..hopeless authority.

#MaendeleoHayanaChama

Sent using Jamii Forums mobile app
Umegongelea msumari wa moto mkuu, ipo haja Rais aifumue hii Mamlaka hawana kazi yoyote ni miongoni mwa watumiaji wabaya kabisa za umma bila faida
 
hizi akili za uwekezaji kwenye bar na grocery, ingekuwa zinatumika kwenye viwanda vidogo vidogo na kufanya production Taifa lingekuwa mbali sana....
 
Hakuna haja ya kuwalalamikia hao kwa sababu hao pia wwnatoka katika jamii isiyojielewa

Hivi kweli mnapanda Bus na mziki unapigwa safari ya masaa 10 na mmekaa kimya tu nyie ni misukule?

Unaingie salon unakuta mziki mpaka wote unashindwa kusema naomba mpunguze mziki halafu unasubiri so called NEMC waje wawanyamazishe wakati na wao wananyoa humo humo

Nilitwa kunyoa na kijana mmoja nikamwambia kwa mziki huo siwezi kuingia humo
Aliniita kwa heshima zote na kuzima mziki mpaka namaliza
Watoto wadogo wanaongoza wanavyotaka wao na nyie mnakubali
Mkiitwa majina ya ajabu mtakataa

Nchi zingine huwezi kukuta huu upumbavu hata kwenye Train na buses utakuta polite notice inasema ongea na simu polepole
Yaani sauti yako unaambiwa punguza
Mziki wala redio hakuna
Na kama ni mziki kwenye hotels ni mdogo sana kiasi ambacho watu mnasikilizana na kuelewana vizuri tu

Mnaendekeza sana haya mambo na kuyakubali kama maisha ya kawaida na kufikiri ndio maendeleo kumbe ni ujinga
Kemea kila mahali hata ukiwa kwenye Bus waambia zimeni hatuna shida na kelele
 
Ungetaja jina la bar na kanisa. Kimara tumewakomesha wajinga fulani wanajiita LA CASA PUB walikuwa wajinga sana kelele mtindo mmoja kisa ilikuwa sijui na mahusiano na Kitila Mkumbo. Hawa wenye hizi bar hawaheshimu kbs afya ya masikio. Paza sauti.
La casa hawa wajomba kelele usiku kucha sjui kama bado wanaendelea na huu upuuzi
 
Ungetaja jina la bar na kanisa. Kimara tumewakomesha wajinga fulani wanajiita LA CASA PUB walikuwa wajinga sana kelele mtindo mmoja kisa ilikuwa sijui na mahusiano na Kitila Mkumbo. Hawa wenye hizi bar hawaheshimu kbs afya ya masikio. Paza sauti.
Mkuu naona bar imekua kimya sana siku hz..mlitumia mbinu gani mkuu
 
Wivu tu.
Acha watu wapige hela. Sasa wakipunguza mziki wanapata vipi wateja. Watu wanataka sehemu pahappen.
Mara hela watengeneze viwanda. Sasa hiyo si kiwanda tosha. Wacha wafanye biashara.
Na bar zitengenezwe nyingi. Kula starehe maisha mafupi. Saloon, ibadani, bar , kwenye basi hata chumbani kula muziki ya kutoshaa weweee..
Nawakilisha.
 
Naandika kwako Mkurugenzi wa NEMC - HQ kwamba huku mitaani hasa katika miji kelele za miziki kwenye ma bar, pub saloon za vinyozi, wauza CD, vigodoro pamoja na nyumba za ibada zimekuwa kero kiasi kwamba Mamlaka yako inaonekana ipo tu kama bendera inatumia fedha za serikali bila tija. Kuna namba za simu 0800110115 imekuwa ukipiga kutoa taarifa hazina msaada wowote, wanaokuwa directed kushughulikia kero hawana hata kipimo cha kupimia uzito wa kelele.

Nakushauri utengeneze kikosi kazi cha kitaifa, kazi yake iwe kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi na kuyafanyia kazi moja kwa moja kutokea ofisini kwako kwasababu wawakilishi wenu walioko kwenye miji hawafanyii kazi kero wanazopelekewa kutokana na kupokea rushwa.

Ikiwa kikosi kazi chako kitakuwa na ufanisi, upo uwezekano wa NEMC kukusanya fine kwa wingi kutoka kwa wavunja sheria hao na kuiongezea serikali mapato.

Kiuhalisia hali ilivyo hivi sasa ni kama Mamlaka yako haipo, na kama ipo basi watendaji wako wameshindwa kazi kabisa.

Tunaomba ulichukulie suala hili kwa uzito wake.

Nawasilisha
mleta mada umekuja na
Mada yenye kuhitaji ufumbuzi,

hili kwa kweli limekuwa ni kero na sina uhakika kama ni mamlaka ipi yenye kusimamia hili kwa sababu kwenye makazi ya watu ndipo pia kunayo makanisa,baa na grocery na hata wakati mwinhine unaweza kuta kunayo hata maduka yenye kuuza albam za muziki hizi biashara tajwa zote wanasumbua sana usiku kwa kelele zao hawawapi watu nafasi ya kulala ili kesho yake waamke wakiwa safi na waweze kuyawahi majukumu

kwa
Kawaida kwa mtu mwenye kujitambua na kuijali afya yake usiku ni muda wa kulala baada ya mtu kuwa amechoka na kwa sababu pia anahitaji kuamka akiwa mwenye afya ya
mwili na akili ili aweze kwenda tekeleza tena majukumu

ikiwa atafunguliwa muziki kwa muda huo hii inasababisha shida kwa afya yake na hata kuzorotesha utendaji wake wa kazi kwa siku inayofuata

Ninashauri baa na hata grocery ziwepo lakini hii sehemu ya kupata huduma ya kinywaji na isiwe ni ya kupata huduma ya muziki
Huduma ya
Muziki ipatikane kwenye majumba ya muziki na ambayo yamewezeshwa kutengenezwa kwa namna ambayo sauti haitoki nje kuwabugudhi wasiohitaji huduma hiyo ili mtaani kuwe na ustaarabu
 
Back
Top Bottom