NEMC: Msako wa wapiga kelele uko pale pale

NEMC: Msako wa wapiga kelele uko pale pale

NEMC wakazie hapo hapo Kuna baa nyingi hakuna kelele na watu wanajaa wenye mabaa wafate sheria
 
Wengine wanakunywa kwa sababu kuna bendi au mziki

Upo kwa ajili ya ligi mkuu na ubishi wa kiwaki. Mziki sio lazima kelele ziwe juu kuzidi viwango mbona kila kitu kipo wazi sheria nazo zinafafanua viwango vizuri kabisa. Chalamila anaongea kama tahira. Hakuna aliyekataza mziki wala kelele. Lakini wamekata kuzidi viwango na sheria zipo sio mtu kalopoka tu Kama yeye tahira maandazi
 
Katika tukio la hivi karibuni, Mkurugenzi wa Baraza la Uhifadhi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Samuel Gwamaka, amezungumza kuhusu operesheni ya msako inayoendelea dhidi ya wanaokiuka sheria za mazingira. Dkt. Gwamaka alisema kuwa wale watakaokamatwa katika msako huo watafuata taratibu za kisheria, na adhabu itatolewa kulingana na kosa lililofanywa. Alibainisha kuwa faini ya milioni tano itatozwa kwa wanaorudia kukiuka sheria hizo, na faini ya milioni mbili kwa wale ambao wanakiuka sheria kwa mara ya kwanza.

Kwa upande mwingine, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, alitoa maoni yake kuhusu suala la kelele katika mji huo. Alisema kuwa Dar es Salaam ni mji wa biashara, na ili kufanikisha uchumi wa mji huo, ni muhimu kuendelea na shughuli za biashara. Hata hivyo, aliwasihi wafanyabiashara kutafuta njia za kuepuka kelele zisizo za lazima. Alieleza kuwa bia bila kelele ni kama juice, ikisisitiza umuhimu wa kuzingatia mazingira ya biashara yanayofaa.

Kwa habari nyingine, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Amos Makalla, ametoa agizo la kufunguliwa kwa baa na kumbi za starehe ambazo zilikuwa zimefungiwa na NEMC kutokana na kelele zilizozidi viwango vilivyowekwa. Aidha, Makalla alipiga marufuku operesheni ya kamata kamata na uviziaji iliyokuwa ikifanywa na NEMC kwa kushirikiana na jeshi la polisi. Agizo hilo linalenga kuimarisha mazingira ya biashara na kuhakikisha kuwa hatua zinazochukuliwa zinafuata utaratibu na sheria.

Habari hizi zinaendelea kutoa mwelekeo kuhusu hatua zinazochukuliwa kudhibiti kelele na kusimamia sheria za mazingira katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania. Ni muhimu kuzingatia sheria na kanuni ili kuhakikisha kuwa mazingira ya biashara yanakuwa endelevu na yanayofaa kwa wote.

Tutakuendelea kuwaletea taarifa zaidi kuhusu suala hili na matukio mengine muhimu.
afadhali tarehe 28 nemc walipumua vizuri na watu walilala vizuri bila makelele
 
Twendeni na chalamila
Hatuwezi kwenda na Chalamila ambaye anachoangalia ni kuwafurahisha wafanyabiashara na anayetaka kupindisha sheria kwa utashi wake binafsi ,kiongozi mzuri ni yule anayefuata sheria na sio kutumia maoni yake ,makelele yana kero na madhara makubwa lakini yeye hatambui hilo ,hatuwezi kuwa na jamii ya viongozi wanaokanyaga sheria
 
Watu waachwe walewe masaa 24,bar ziwe wazi masaa 24 ili kukuza uchumi.
Haya ya kupangiana mda wa kulewa Karne hii ni upumbavu mkubwa kabisa kwani wanapewa Hela ya kulewa.
Mda wako wa kazi ni mda wa mapumziko wa mwingine,ukilala usiku wengine ndo wapo kazini,ukilala mchana wenzako wapo kazini.
Hili litazamwe
Hakuna anayepangiwa muda ,kinachosimamiwa ni usalama wa mazingira, makelele yamekuwa na madhara makubwa kwa watoto kuwa viziwi na kufariki ,kuleta matatizo ya moyo na imesababisha vifo ,watoto wameshindwa kujisomea ,watu kukosa utulivu na muda wa kupumzika yote haya ni madhara hasi kwa jamii ,sauti ipigwe kwa kiwango kilicho salama kama ambavyo sheria inataka ,tukizingatia biaahara tu tutakuwa na jamii ambayo haina afya na imeathirika ,NEMC inao wajibu kisheria kusimamia uhai wa mazingira na viumbe hai nao wanatekeleza wajibu wao kisheria
 
Hao si ni mambwaa tu yakikaliaa kiti wanaona rahis kucontrol wengne ila akifukuzwaa kazi ndo anajua uhalisia ulivyo
NEMC hawa control wengine bali mazingira ,NEMC wanasimamia na kulinda usalama na ustawi wa mazingira na viumbe hai ,maisha ni zaidi ya fedha bali afya ni jambo la msingi saana ,tena tuwapongeze sana NEMC kwa kutekeleza majukumu yao bila kumuonea mtu haya , wafanyakazi wanao wajibu wa kutekeleza kazi zao kwa kufuata sheria za Nchi na kwa umaksusi hizi za mazingira ,kwanini wamiliki wa ma BAR wasipige mziki ambao hautakuwa kero kwa makazi ya watu ?? Kuna haja gani ya kusumbua walio nyumbani?? Hii haikubaliki NEMC wachape kazi hatutaki makelele
 
Hakuna anayepangiwa muda ,kinachosimamiwa ni usalama wa mazingira, makelele yamekuwa na madhara makubwa kwa watoto kuwa viziwi na kufariki ,kuleta matatizo ya moyo na imesababisha vifo ,watoto wameshindwa kujisomea ,watu kukosa utulivu na muda wa kupumzika yote haya ni madhara hasi kwa jamii ,sauti ipigwe kwa kiwango kilicho salama kama ambavyo sheria inataka ,tukizingatia biaahara tu tutakuwa na jamii ambayo haina afya na imeathirika ,NEMC inao wajibu kisheria kusimamia uhai wa mazingira na viumbe hai nao wanatekeleza wajibu wao kisheria
Mazingira ya Dar kelele hazikwepeki sababu ya mipango miji mibovu
 
Katika tukio la hivi karibuni, Mkurugenzi wa Baraza la Uhifadhi wa Mazingira (NEMC), Dkt. Samuel Gwamaka, amezungumza kuhusu operesheni ya msako inayoendelea dhidi ya wanaokiuka sheria za mazingira. Dkt. Gwamaka alisema kuwa wale watakaokamatwa katika msako huo watafuata taratibu za kisheria, na adhabu itatolewa kulingana na kosa lililofanywa. Alibainisha kuwa faini ya milioni tano itatozwa kwa wanaorudia kukiuka sheria hizo, na faini ya milioni mbili kwa wale ambao wanakiuka sheria kwa mara ya kwanza.

Kwa upande mwingine, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, alitoa maoni yake kuhusu suala la kelele katika mji huo. Alisema kuwa Dar es Salaam ni mji wa biashara, na ili kufanikisha uchumi wa mji huo, ni muhimu kuendelea na shughuli za biashara. Hata hivyo, aliwasihi wafanyabiashara kutafuta njia za kuepuka kelele zisizo za lazima. Alieleza kuwa bia bila kelele ni kama juice, ikisisitiza umuhimu wa kuzingatia mazingira ya biashara yanayofaa.

Kwa habari nyingine, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Amos Makalla, ametoa agizo la kufunguliwa kwa baa na kumbi za starehe ambazo zilikuwa zimefungiwa na NEMC kutokana na kelele zilizozidi viwango vilivyowekwa. Aidha, Makalla alipiga marufuku operesheni ya kamata kamata na uviziaji iliyokuwa ikifanywa na NEMC kwa kushirikiana na jeshi la polisi. Agizo hilo linalenga kuimarisha mazingira ya biashara na kuhakikisha kuwa hatua zinazochukuliwa zinafuata utaratibu na sheria.

Habari hizi zinaendelea kutoa mwelekeo kuhusu hatua zinazochukuliwa kudhibiti kelele na kusimamia sheria za mazingira katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania. Ni muhimu kuzingatia sheria na kanuni ili kuhakikisha kuwa mazingira ya biashara yanakuwa endelevu na yanayofaa kwa wote.

Tutakuendelea kuwaletea taarifa zaidi kuhusu suala hili na matukio mengine muhimu.
Uendeleee bado tunahitaji kustopisha kabisa hizi zilizidi kelele mlichofanya NEMC nichakupongezwa ila msitishwe na hawa wakina Msukuma ambao wao wanaangalia matumbo yao tu na kulinda biashara zao kazeni pitieni mpaka waseme basi sisi watu wamtaani bado tunawapongeza japo siasa imeingia
 
Hatuwezi kwenda na Chalamila ambaye anachoangalia ni kuwafurahisha wafanyabiashara na anayetaka kupindisha sheria kwa utashi wake binafsi ,kiongozi mzuri ni yule anayefuata sheria na sio kutumia maoni yake ,makelele yana kero na madhara makubwa lakini yeye hatambui hilo ,hatuwezi kuwa na jamii ya viongozi wanaokanyaga sheria
Umeongea vizuri sana lakini kwa kuwa baadhi ya watanzania hawajui wakitakacho hawatakuelewa...
 
Back
Top Bottom