New administration under Samia Suluhu gives hope after 5 years of hopelessness

MADEREVA WA WABUNGE WANALIA MACHOZI.

Na Thadei Ole Mushi.

Baada ya kufichua marupurupu ya Mbunge pamoja na Mshahara wao madereva wa wabunge wameomba watanzania wawafikishie kilio Chao Kwa Spika.

1. Wanadai kuwa hakuna Dereva ambaye ana Mkataba hata mmoja wa Kazi yake hivyo KUISHI Kwa wasiwasi kuwa Mbunge anaweza kuamka asubuhi na kumtimua kazi. Hivyo wanaomba watambuliwe kisheria na wapewe mikataba ili wafanye Kazi yao kwa weledi na bila hofu. Wanadai kila mara ukimchukiza Mbunge tu Kwa kuwa huna Mkataba hukufukuza na Stahiki zako zote hupotea.

2. Wamesema Kwa siku Mbunge akiwa Dodoma Dereva hulipwa Shilingi 70,000 kama Posho. Kwa maana hiyo katika kipindi chote Cha Bunge la budget siku 97 wanapaswa kulipwa Shilingi 6,790,000 lakini wanadai Fedha hizi wabunge husaini lakini hazifiki kwao wabunge wanabaki Nazo.

3. Wanaomba Mishahara yao upitie kwenye Account zao Moja kwa Moja badala ya kupitia kwenye account ya Mbunge. Wanadai Kwa kuwa hawana Mkataba na Mbunge ni Bosi wake hawathubutu Kuwadai Mishahara na badala yake mara nyingine hawalipwi huishia kununulia Nyama choma biashara inaisha.

4. Wanadai kuwa Spika aangalie uwezekano wa kuwaongezea mshahara toka 170,000 kwenda laki Tano Kwa kuwa nao Wana familia zinazowategemea. Wanadai ukichukua mshahara wanaolipwa Sasa hivi ni sawa na Kwa Siku analipwa Shilingi 5,000 mshahara huu hata kibarua wa fundi ujenzi huwezi mlipa huko mtaani.

Wabeba Roho za waheshimiwa ni sahihi kufanyiwa hivi?

Share Hadi imfikie Dereva unayemjua.

Ole Mushi
0712702602
 
ELIMU YA BURE YA GARI LAKO

Matairi ya gari muda wake rasmi wa matumizi ni miaka minne ( 4 ) tu toka yatengenezwe (Sio toka uyafunge kwenye gari lako).......Ikishapita miaka minne toka tairi litengenezwe linaweza kupasuka wakati wowote.

Jinsi ya kutambua tairi lilitengenezwa lini tafuta alama kwenye tairi iliyoandikwa kwa mfumo huu (2603) kuna kuwa na alama ya nyota mwanzo na mwisho wa hizo namba nne. Namba mbili za kwanza zinaonyesha tairi lilitengenezwa wiki ya ngapi katika wiki 52 za mwaka na namba mbili za mwisho zinaonyesha mwaka tairi lilipo tengenezwa.

Kwa mfano 2603 inamaanisha tairi lilitengenezwa wiki ya 26 ya mwaka 2003 au 2699 inamaanisha tairi lilitengenezwa wiki ya 26 ya mwaka 1999. KAGUA MATAIRI YAKO USITUMIE TAIRI LILILO PITA ZAIDI YA MIAKA MINNE KWANI LINAWEZA PASUKA WAKATI WOWOTE......hapo ndio inapotokea tairi mpya umenunua juzi kisha baada ya Wiki moja ya matumizi inapasuka puu ukiwa kwenye mwendo na kuanza kutafuta chanzo na usikione kuumbe lilisha Expire ivo ni vema kuchukua tahadhari.

Pia kila tairi limeandikwa uwezo wa spidi yake ukikimbiza zaidi ya uwezo wake itapasuka na hizo spidi zimeandikwa kwa herufi Kama ifuatavyo.

CODE. SPIDI
F========80
G ========90
J ========100
K ========110
L ========120
M ========130
N ========140
P ========150
Q ========160
R ========170
S ========180
T ========190
H ========200

Huandikwa hivi
280/R/70/13/560/S
hiyo herufi ya mwisho ndio speed ya mwisho ya tair kama
Hapo herufi S inawakilisha Spidi,180.

Share na marafiki ili wawe salama na kwa ununuzi sahihi wa tairi la gari lako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…