New administration under Samia Suluhu gives hope after 5 years of hopelessness

New administration under Samia Suluhu gives hope after 5 years of hopelessness




Hakuna fursa tulizozipoteza acha kuongopa.

Tunayo matatizo ya uwezekaji na usimamizi lakini DUBAI PORTS WORLD au mwingine siyo majibu ya utatuzi wa kero tajwa.


Kwanza hakuna mwekezaji atakayewekeza nchini bali yupo wa kukopa kwenye mabenki kwa dhamana yetu na atashindwa marejesho na kutuaachia mzigo wa madeni na riba kibao huku sehemu kubwa ya hela alizozikopa kutoziwekeza hapa nchini bali kuzitumia kujenga hoja nchi nyingine za kupewa fursa za kuendesha bandari zao.


Pili, tuache kujidanganya ya kuwa uwekezaji huu utapunguza urasimu. DP WORLD atakuja na trafiki polisi wake kukomesha rushwa mabarabarani?

Tatu, tuache kupotosha ya kuwa hapatakuwepo msongamano baada ya DP WORLD wakichukua bandari zetu. Kwanza hawatawekeza kama walivyoahidi. Kigugumizi cha ukwasi alichokuwa nacho TISS kinamhusu kwa ukwasi tajwa hana na ndiyo maana hataki kujitia kitanzi cha huo uwekezaji utaanza lini na utakuwa wa namna gani.

Nne, DP WORLD hana sauti juu ya mfumo wa njia zetu za usafirishaji. Itabidi tumpe na TANROADS, TARULA na TRL ili aondoe vikwazo vilivyoko barabarani. Itabidi misururu ya maroli kwenye mizania aidha sheria zitenguliwe au akayakusanye hayo mapato mwenyewe.

Ubovu na ufinyu wa barabara zetu utamkwaza.

Itabidi TRA nayo apewe ili aharakishe makusanyo ya kodi na kuondoa misururu ya malori mipakani. Pia aidha afute kodi zote au kuzipunguza ili kuwavutia watakaozitumia bandari zetu. Vinginevyo, misongamano iko pale pale.

Itabidi pia mizigo yote inayopitia kwake iwe yake kwani wenye mizigo huchelewesha kuikomboa kwa kuilipia na hata wengine kuikacha.

Tunatoa hii mifano kubeza hoja za huyu mpotoshaji.


Kifupi, ili khoja ya huyu mtaalamu itelezeke itabidi DP WORLD watutawale na kuunda serikali, bunge na kusimamia shughuli zote za serikali siyo nchini tu pia na kwa majirani zetu jambo ambalo kamwe halitatokea.


Hatuna matatizo na mizigo inakotokea bali ikifika bandari zetu ndiyo tuna changamoto


Kwa hiyo, kuzungumzia kero ambazo hazipo ni ushuhuda anaongelea mambo ambayo hata hayafahamu na hii hoja yake kuwa amelitumikia TPA kitambo haina mashiko kama upembuzi wenyewe ndiyo huu.
 
Punda kachoka wajamani!
PSX_20230621_195619.jpg
 
DEMOKRASIA IWE YA WANANCHI WA TANZANIA BADALA YA VYAMA VYA SIASA!





Kama unafuatilia kwa karibu sanaaaaaaa mijadala bungeni utabaini yafuatayo:-

a) Wabunge wa CCM wote Mungu wao ni matumbo yao na ndiyo maana kazi kubwa wanayoifanya ni kuisifia serikali badala ya kuisimamia.

b) Umasikini ndiyo mtaji mkuu wa CCM wa kutawala na kwa hiyo kamwe hawataupunguza bali kuuchochea ili hizo peremende wanazowatupia raia waendeelee kuwasujudia.

c) Gharama kubwa ya kuliendesha bunge ni mzigo mkubwa kwa wananchi hususani ukizingatia halina tija.


d) Mahudhurio ya wabunge hayana uhusiano wowote na jinsi wanavyolipwa. Wanalipwa posho za vikao wahudhurie au wasihudhurie. Tunahitaji tekinolojia ya viti vya wabunge viwekewe AI na kunakiri kila sekunde mbunge akiwa kakaa kwenye kiti na alipwe kwa angalau kupasha joto kiti.

e) Wabunge wote wa CCM huunga mkono hoja sasa kama kazi ni hiyo kwanini wako bungeni? Kama kila kitu cha watendaji serikalini wanakikubali kwanini waendelee kuwepo bungeni?

f) Wabunge wote wa CCM hawakuchaguliwa na wananchi na ndiyo maana wanakaza buti kujikomba kwa Rais ili majina yao yasifyekwe 2025.


USHAURI


Kulipa bunge meno inabidi tutoke kwenye demokrasia ya vyama vya siasa na tuhamie kwenye demokrasia ya wananchi wa Tanzania.


Tukifika huko, mgombea wa nafasi yoyote ya umma hahitaji udhamini wa chama cha siasa bali ni kuungwa mkono na wapigakura waliosajiliwa kwa asilimia tano ya jimbo husika au chini ya hapo. Kipimo ni idadi ya sahihi za wapigakura kwa kila jimbo husika na wala siyo vinginevyo.


Demokrasia ya vyama vya siasa imedhoofisha uwakilishi kwa kuwa utetezi wa viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa badala ya wapigakura.

Unafiki wa wawakilishi wote wa vyama vya siasa unatokana na demokrasia yetu kuwa ya vyama vya siasa badala ya wananchi na hili tunapingana na amri za Mwenyezi Mungu ambazo zinasema yafuatayo:-

"Nendeni mkatawale dunia.."

Sisi kwa vile tunamchukia Mwenyezi Mungu tunaasi amri tajwa na kuamua ndani ya katiba kukataa demokrasia itutumikie na badala yake sisi tumekuwa vijakazi wa demokrasia.

Badala ya demokrasia kuwa kwa manufaa ya raia tumeifanya iwe kwa manufaa viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa na vyama tajwa vina wenyewe siyo vya raia wa kawaida.


Kwa wale wote hudai katiba mpya mjue zoezi hilo litaanza pale mtakapokataa DEMOKRASIA YA VYAMA VYA SIASA na kuwa DEMOKRASIA YA WANANCHI WA TANZANIA.

Demokrasia iwe kijakazi wetu badala ya mfumo uliopo wa sasa ambao sisi ni watumwa wa demokrasia na matokeo yake uwakilishi wetu ni haramu na umekithiri uongo, unafiki, kujikomba na udanganyifu.
 
TUNDU LISSU AKOSOLEWA.


Tundu Lissu juzi kadai wabunge wa CCM Mungu wao ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (JMT).


Hii kauli siyo sahihi na inapotosha ukweli.

Kauli sahihi ni kuwa viongozi wote wa nchi hii wakiwemo wa upinzani Mungu wao ni matumbo yao na huwasujudia wale wa kitaifa ili wasiwafungie nje milango ya mlo.


Na ndiyo maana Tundu Lissu kamwe hatajiona ni mnafiki yeye binafsi na bosi wake Mbowe kuikosoa taasisi ya Urais kuwa ni ya umangimeza wakati hata wao nafasi zao ndani ya Chadema ni za umangimeza.

Chadema walipinga genge la wabunge wa CCM lililoibua vuguvugu la kuondoa ukomo wa Urais kwenye katiba ili Mwendazake atawale maisha yake yote wakati wao walifuta ukomo wa nafasi za uongozi wa Chadema kwa minajili ya kutawala chama hicho cha siasa maisha yao yote! Hawa wapuuzwe ni ndumila kuwili tu


Viongozi wa vyama vya upinzani hawana ukomo wa madaraka na kupoteza uhalali wa kuhoji Rais wa JMT kuhodhi madaraka makubwa.

Kwa lugha nyepesi, Tundu Lissu na Mbowe ni wanafiki kudai katiba ya nchi irekebishwe ili kuwarahisishia kutwaa dola wakati huo wema hawawatendei wale waliopo chini yao ndani ya Chadema.

Kauli mbiu ya Chadema ya

"PEOPLE'S POWER...." Ni utapeli usio na mithili.

Kuishinda CCM, Chadema na vyama vyote vya upinzani lazima viwe ni mfano wa katiba ya kuigwa lakini kwa jinsi katiba zao zilivyo mbaya hata kuzidi ya CCM wamejipora wao wenyewe uhalali wa kuhoji madhaifu ya katiba ya JMT.

Charity begins at home, and Chadema has miserably failed to pass this simple test!
 
Ubinafsishaji unathibitisha wanasiasa wameshindwa kuusimamia uchumi na sasa wameamua kuwasimamia askari wa mamluki.

Wasichojua kama wameshindwana na wamatumbi watawaweza wakuja ambao kulingana na hoja yao ya kuwadhulumu wazawa wenye uraia pacha haki zao za uraia sasa itabidi waamini mamluki ambao siyo wazalendo wawatatulie matatizo ambayo wazalendo kwa maana ya uraia wameshindwa.
 
BARUA YA WAZI KWA WAZIRI WA KILIMO: FUTA KODI ZA MAZAO YA VYAKULA NA RUZUKU YA MBOLEA. Unakwama wapi?



Mpakani Kenya hawawapi vibali malori ya TZ kupita inabidi mzigo ushushwe na kupakiwa malori ya Kenya kwa sababu hizo hizo malori ya TZ hayajasajiliwa Kenya kama kampuni na hivyo hawalipi kodi

Mwisho wa siku ni mkulima anaumia na mlaji pia.

Jibu ni kufuta kodi kwenye biashara ya vyakula hapo walaji na wakulima watafaidi.

Kama wawekezaji kutoka nje mwendo mdundo hawalipi kodi kwa kigezo cha kusadikika cha kuwavutia tunapata wapi kigugumizi kumpa ruzuku mkulima na mlaji?

Ruzuku ya mbolea haimfikii mkulima kwani mbolea ya bei poa utaikuta nchi za jirani inauzwa kama njugu na wakulima wetu wala hawafaidiki ila wafanyabiashara na wachuuzi tu.

Futa kodi za mazao ya chakula na ondoa ruzuku ya mbolea kusawazisha pengo la bajeti.

Mchuuzi aandike maumivu huku mzalishaji na mlaji wachekelee.

Sera za Bashe hazimsaidii mkulima, mlaji wala serikali. Ukirtimba unazaa rushwa tu labda hilo ndilo analipalilia kwa masilahi yake anayoyajua.
 
Pokeeni maelekezo tuliyoyapata kutoka mbinguni mida hii!


Ni ujumbe mzito unamhusu yule kinara wa awamu ya nne ambaye ndiye aliusimika huu utawala dhalimu ambao haukutokana na Mwenyezi Mungu.

Yule dudumuzi anayempekecha tayari kapewa maagizo ya kumalizana naye


Ukisikia kalazwa kitandani ujue ni kwa kheri ya kuonana.

Bwana alitoa Bwana kajitwalia.


Haya yatafanyika kuzuia mapigano ya wenyewe kwa wenyewe kutokana na maliasili za nchi kuuziwa wageni huku raia wanateseka na umasikini wasio stahili


Na neno la Mungu litimie lisemalo:-


Maadui wangu nimewapa kazi ya kukusanya mali ili wawakabidhi wenye haki wale.


Nitampiga jemedari wao na chawa wake watatawanyika na baadaye nitawaangamiza pia hao chawa wake ambao wanamsujudia badala ya kunisujudia Mimi....Asema BWANA.


Jina la Bwana lihidimiwe!
 
KUITETEA SERIKALI KWENYE SWALA LA BANDARI MTAIPONZA NCHI

VYOMBO VYA HABARI;
Najua kutangaza habari ni taaluma yenu ila kuna wakati hamtendi haki kwani hamzingatii weredi kwani mnapenda kutangaza habari zao na kuzivalia njuga wakati hoja zetu wananchi mnazikwepa hoja za wananchi juu ya uwekezaji bandari.
Lakini hata msipozipa kipaumbele bado taarifa ya mtu kwa mtu na mitandao ya kijamii itafikisha hoja zetu na maamuzi ya walio wengi.

BUNGE/WABUNGE
Napata mashaka kuwa wengi wenu hamkupata ubunge kihalali je? Ninyi ni wenye akili sana (spika) kuwadhidi wengine kwani wanaohoji mitandaoni hawana haki ya kusikilizwa (sauti ya dharau nikasikia wakati wa kupitisha azimio la uwekezaji)
Kama mlipata ubunge kihalali mbona hamuwasikilizi wananchi.

Mnapitisha azimio la makubaliano yasiyoonyesha ukomo wa mwekezaji halafu mwekezaji yeye amewawekea masharti yake ambayo mmejifanya hayaoni, mnadai yatarekebishwa wakati wa kuingia kwenye mkataba wa uwekezaji sasa mtarekebisha nini kama mmekubari kuwa kwa namna ye yote makubaliano hayata vunjika?
au mnazani mnakula na kipofu?
Tupo macho bora ufanyike uwekezaji kwenye bunge lakini sio bandari.

MSEMAJI WA SERIKALI
Kweli kazi yako ni kuisemea serikali hili natambua lakini hamjiulizi kwa nini wananchi walio wengi wameyakataa hayo makubaliano yenu na Dp world?
Unatuambia kuwa hayo ni makubaliano tu! kwani huoni kuna vipengele vyenye utata humo na mmevikubari?
Msizibe masikio na kuwapuuza wananchi (mbio za kilema hazitimui vumbi)
Binafsi naungana na wanaopinga uwekezaji kwenye bandari zetu vinginevyo makubaliano yatazamwe upya na sehemu zenye utata zibadilishwe.

WAZEE NA HEKIMA ZAO..! UMRI UMEENDA LAKINI ANA MANENO YA BUSARA
IMG-20230624-WA0015.jpg
 
MATATIZO YETU NI YA KIMFUMO SIYO UTAALAMU.



Uhuru wa kiuchumi Afrika utaanza pale ambapo tutakuwa na uraia mmoja.

Ukisema ninajivunia kuwa mzanzibara swali unalopaswa kujiuliza ni nani alikuita hivyo? Jibu ni mkoloni.


Ukijigamba mimi ni Mtanganyika swali ambalo unapaswa ujiulize ni nani alikuita hivyo? Jibu ni mkoloni.

Mipaka yote iliyopo Afrika lengo lake ni kutudhoofisha ili mabeberu watugawe na kututawala.

Viongozi wote wa Afrika ni vibaraka wa ukoloni mamboleo na ndiyo maana hawako tayari kuruhusu Afrika ikaungana na kuwa nchi moja.

Pamoja na kuhofu kupoteza nyadhifa zao pia wanafurahia kuwa vibaraka wa ukoloni mamboleo na ndiyo maana huwa kiguu kwa njia kuwafungulia fursa mabeberu huku wakiwakwaza watu wao.

Haingii kichwani mkulima wa mazao ya vyakula alipe kodi wakati tumetunga sheria za kutokusanya kodi kwa wawekezaji kutoka nje. Tuko mstari wa mbele kuchochea lishe duni kwa raia wetu kwa kuongeza gharama za vyakula kwa kutoza kodi ili mradi tutoe ruzuku kwa wawekezaji kutoka nje.

Ikija uraia pacha tunawakana raia kwa kudai siyo wazalendo na tunajipanga kuweka mikakati ya kutengua uraia wao kwa kuuwekea mipaka ya ushiriki wa maendeleo ya nchi yao kwa kile tunachokiita "uraia maalumu".

Haki zinazonyofolewa kwenye "uraia maalumu" ni hakI za kushiriki kwenye siasa na utumishi wa umma kwa kudai raia pacha wana migongano ya uzalendo!

Akizuka mwekezaji mamluki kwenye sekta ya umma kama maji, nishati, ulinzi na usalama, bandari, kilimo n.k waumini wa uzalendo hutupilia mbali hoja ya uzalendo kwa wageni ambao hawana hata harufu ya uraia wetu na kuwafungulia fursa ya kukamata sekta tajwa na nyinginezo za umma! Hawakumbuki kuwa uwekezaji kutoka nje una migongano ya uzalendo, la hasha na hata huwatumia hawa askari mamluki kuwawezesha kuiba kura wabaki madarakani.

Lakini, tatizo la kumdhulumu Mwenyezi Mungu ni kuwa hatutafanikiwa. Maendeleo tutayasikia kwenye bomba tu. Tutayadhamiria kwenye makaratasi na kuyahubiri kwa sauti ya juu kwenye majukwaa mbalimbali lakini utekelezaji wake utaishia kwenye makabrasha tu.

Tutabakia kuwalaumu wataalamu na wananchi kwa matatizo ya mfumo mbovu uliozaa siasa mbaya, uongozi duni na ukosefu wa uelewa usiyo na kifani.


Hata EAC hadi leo hatuna uraia mmoja lakini tunajigamba tuna jumuiya. Jumuiya gani hiyo ambayo haitoi uraia mmoja kwa watu wake?

Jumuiya gani hiyo ambayo kampuni ikisajiliwa nchi moja usajili wake hautambuliwi nchi nyingine?

Jumuiya gani haina idara moja ya uhamiaji, fedha, kodi, ulinzi na mambo ya nje?


Ikija taasisi za kidunia tuko mbele kuzishutumu mapungufu yake ambayo yako nje ya uwezo wetu lakini ya taasisi zetu nazo zina ukakasi huohuo lakini hatuoni.


Majibu ya maendeleo ya Afrika yataanza kwa kufuta mipaka ya mkoloni na kutekeleza kwa vitendo:-

UMOJA NI NGUVU NA UTENGANO NI UDHAIFU.

Hebu jiulize kwanini wachina wako wengi kwa zaidi ya bilioni na wana nchi kubwa lakini wameichukua Hong-Kong na wako tayari kumwaga damu kuungana na Taiwan?


Wanajua kuwa na sauti humu duniani ni lazima waungane wawe kitu kimoja sisi miaka zaidi ya 60 ya uhuru bado tunajivunia utengano wetu tuliowekewa na wakoloni.

Kwa kuchagua utengano tujue fika tumechagua kutawaliwa.


Matatizo yote ya uwekezaji Afrika ukiyatafakari sana yanatokana na mipaka ambayo mkoloni alituwekea tusiivuke na hivyo atutawale.

Afrika ikiwa nchi moja tutagundua hatuhitaji uwekezaji wa aina yoyote kutoka nje ya Afrika maana kila kitu tunacho.
 
Wakati viongozi wetu wanahimiza tuzaane na huku wanakaza buti kutufungia fursa za ajira huku wakiwafungulia wageni nafasi hizo hizo wajue fika wanakoleza moto wa machafuko ya wenyewe kwa wenyewe.

Hawa watoto tunaowazaa watamulika hii dhuluma na watachukua hatua ya kujipatia uhuru wa kiuchumi na kufanikiwa itabidi wajitoe mhanga na kuwatimua wawekezaji uchwara.

Idi Amin Dada wa Uganda alituachia urithi mkubwa penye udhia weka musuli na wahindi wote aliwatimua na kuwawezesha raia wake


Mugabe wa Zimbabwe ni urithi wetu penye uporaji nasi tutapora kurekebisha na kukemea dhuluma na haya lazima yatatokea.
 
Serikali yoyote ile duniani inayoendesha nchi kama biashara ya mtu binafsi imepoteza uhalali wa kutawala.

Huwezi ukarukia ndege ukaenda nje ya nchi na kusaini mikataba feki bila ridhaa ya wananchi.

Urais siyo nafasi ya kujifanyia utakavyo bali kuipeleka nchi kwa utashi wa wengi.

Kura ya maoni inahitajika kabla njia kuu za uchumi hatujaporwa.

Inabidi tuulizwe kupitia kura ya maoni kama tunaafiki kuwatajirisha waarabu na kuwafukarisha vizazi vijavyo pia na hata sasa kujinyima nafasi ya kuendesha na kujiamulia mambo yetu wenyewe.

Hata kama mtu umeamua kula halahala usitutapikie matapishi yako.


Bunge ambalo hatujalichagua halina mamlaka ya kutuuza mchana kweupe. Huo ndiyo ukweli wao. Wezi wa kura hawawezi kututendea haki hata siku moja.

Kama kura zetu hawakuhesabu ila walipika matokeo yao wayajuayo wao basi wajue Mwenyezi Mungu hayuko nao na lolote wafanyalo Mwenyezi Mungu atawakwamisha.


Ninawahakikishieni hawa DP WORLD na vibaraka wao hapa nchini wataangukia pua hawaendi mahali asema BWANA kwani atawakemea.
 
Ubinafsishaji maana yake tunakiri tumeshindwa kujitawala wenyewe.


Sasa kama hii ni kweli turudi UN na kuwaambia Nyerere alikuwa tapeli aliwadanganya sisi bado hatuko tayari kujitawala tunaomba mtupe nchi kubwa hata kama hao waarabu wa Dubai watuandae kujitawala teh teh teh [emoji2] [emoji3] [emoji1] [emoji16] [emoji1787] [emoji23] [emoji2] [emoji3]

Hilo hawa vibaraka wa ukoloni mamboleo watapinga kwa nguvu zao zote maana ugali wao hatihati ila kuuza maliasili mstari wa mbele kwa minajili ya kujimilikisha mali za umma kupitia kivuli cha uwekezaji kutoka nje.


(kleptocracy + Kakistocracy = Foolishness)
 
Orodha ya mama ya wagombea urais kupitia CCM 2030.


1) Ummy - afya


2) Axweso - Maji

3) Spika

4) Mwinyi - Zanzibara

5)...........

Ambao hawana sifa ni waziri mkuu na makamu wa Rais. (Tutafafanua.)


Tunabashiri Axweso ndiye ataibuka kidedea na kugombea Urais kwa tiketi ya CCM 2030 na atashinda kihalali hatahitaji kuiba kura ya mtu. (Tutadadavua siku zijazo)


Tunawaeleza mapema ili itakapotokea msishangae maana tuliwatonya.

Huyu Makamu ataendelea kujikomba lakini wenzie wameishamshtukia ni mnafiki wa kupindukia anachoongea mdomoni hakiko moyoni. Hivyo, hawamwamini hata chembe atabakia hapo hapo hadi utawala wa mama uishie 2030 na watastaafu pamoja. Huyu mama aliwatahadharisha lakini hakuna anayemsikiliza labda huyo Axweso. Alisema macho yake malegevu lakini yanaona watajua alimaanisha nini 2030.

Huyu Waziri Mkuu hana hata mweleko wa uongozi wanamshangaa Mwendazake kwanini hakuona hilo.


January Makamba anaweza kujaza nafasi ya 5 kama mzee wa usoga atakuwepo lakini tuna mashaka kama atakuwepo 2030 kushawishi hilo. Kama hatakuwepo, basi tutaongeza jina la 5 wakati mwafaka ukifika.

Na huyu wa uchukuzi wanamtumia tu lakini hawatamteua ajaribu bahati yake ingawaje pia hili swala la DP WORLD limemmaliza kisiasa kabisa hakuna anayeweza kumwamini tena. Alipaswa kumshauri bosi wake madhara ya kisiasa ya kuingia huu mkataba na DP WORLD kwa hiyo itabidi afuate nyayo za Kolimba na Malecela uwajibikaji wa kisiasa. Huwezi kudadavua faida za kiuchumi tu bila kujumlisha na athari za kisiasa. Ukifanya hivyo, kuna siku utawajibika kisiasa.
 



Msichojua DP WORLD hakuna kukusanya kodi na TRA. Serikali italipwa chochote DP WORLD wataamua kuwapa baada ya kuondoa gharama zao.

Bila ya kuwa free port malengo ya kushusha, kupakuwa mizigo na kuisafirisha iendako itakuwa hadithi ya abunuwas. Urasimu wala siyo uwezo wa mitambo utazorotesha shughuli zote bandarini.

Pili, magendo uwekezaji huu kamwe hawatauzuia na inawezekana ukaongezeka kwa sababu mwekezaji yuko kimapato zaidi. Kwa hiyo, tutarajie nyara za serikali, madawa ya kulevya n.k yamepata ahueni.

Tatu, hakuna ushahidi mwekezaji atawekeza lolote lile kama siyo kuutumia mkataba huohuo kuombea mikopo tena kwa riba kubwa na kwa udhamini wetu. Na hata akisomba hiyo mikopo kwa dhamana yetu hawajibiki kuwekeza lolote chini ya huu mkataba.

Nne, upo uwezekano kwa vile habanwi muda na aina ya uwekezaji anaweza kutumia mkataba huu kuhodhi bandari kavu nchi za jirani na kuingilia uhuru wao wa kujiamulia mambo yao wenyewe na sisi tutakuwa na mchango mkubwa kwenye hili!

Tano, hoja zote za JPM ni majungu kwa sababu hakuna mtendaji hata mmoja aliwahi kufikishwa mahakamani mbali ya kutiwa hatiani kwa mlolongo wa jinai aliolalamikia.

Sita, hata kama tukimpa faida ya mashaka inatosha kubaini ya kuwa jinai inayoongelewa inaenda hadi kwenye vyombo vya usalama na mitandao ya kibenki na kuufanya huu uwekezaji kutoweza kuzuia matukio ya kihalifu ya namna hii.

Saba, hata taarifa ya CAG iliyonukuliwa ni majungu kwa sababu CAG alijuaje juu ya meli ambazo hata kwenye kumbukumbu hazimo? Kazi ya CAG siyo kusaka jinai bali kukagua kama taratibu za kiuhasibu zilozingatiwa.

Nane, kwa CAG kuzungumzia kwenye taarifa yake meli 60 hewa ni dhahiri alifanyia kazi umbea alioupata hapo bandarini na hivyo kuvuka mipaka ya kazi yake.
 
THE THIEVES IN OUR BUS
[emoji4][emoji4][emoji4][emoji4][emoji4][emoji4][emoji4][emoji4][emoji4]

A teacher received his salary and boarded a crowded bus back to his home, and there was a thief in the bus.

The thief stole the teacher's money from his pocket.

After the teacher reached his destination, the driver asked for his fare, the Teacher deep his hand into his pocket and found nothing.

The teacher's face became blushed, and his tongue stuck on the rooftop. He was utterly embarrassed. The driver, who is now angry, said mockingly to the teacher that: "Shame on you, you consider yourself a respected person while you can not afford your transport fare!."

The teacher was again very much embarrassed.
As this was going on, pride hit a potion of the thief's ego, and he was moved to say the angry driver: "My brother, the teacher's fare is on me!."

That is the thief offered to help the teacher, who is his victim.
He helped not out of pity for the poor teacher but to buy other passengers' trust and confidence and to use some of the stolen money to earn respect before the rest of the passengers on the bus.

The poor teacher who did not understand what was happening smiled and said to the thief: "May GOD bless you and multiply your likes, sir!."

Then some of the passengers in the bus also praised the thief, praised his kindness, and also prayed for him and that GOD should increase his kinds.

Since then, the number of thieves in our bus have increased, and they continue to receive our thanks and appreciation;

We are all on the bus where thieves are stealing from us and use the stolen money to buy our trust and earn our respect in a way that we keep thanking them for their "kindness and generosity".

This is the metaphor of the state of our nation

The thieves in our bus are increasing all the time because we continue praising them for returning crumbs, peanuts, and leftovers from the colossal loot they stole from us.

NB: I saw this somewhere, and I felt the compassionate need to share it with you.
 
STATEMENT IN RESPECT TO THE INTERGOVERNMENTAL AGREEMENT (IGA) BETWEEN THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA AND THE EMIRATE OF DUBAI CONCERNING THE ECONOMIC AND SOCIAL PARTNERSHIP FOR DEVELOPMENT AND IMPROVING THE PERFORMANCE OF SEA AND LAKE PORTS IN TANZANIA DATED 25TH OCTOBER 2022.





Tanganyika Law Society is a professional body established by the Tanganyika Law Society Act, Cap. 307 R.E. 2002. As stated in Section 4 of the Act, the Society's aims include, among other things: aiding the Government, Parliament, and Courts in matters affecting legislation, administration, and and practice of the law in Tanzania; representing, protecting, and assisting members of the Tanzanian legal profession in practice conditions and other areas; and protecting and assisting the Tanzanian public in all matters touching, ancillary or incidental to the law. Besides, In addition, according to Article 27(1) of the Constitution of the United Republic of Tanzania, Cap. 2, R.E. 2002, every person has the duty to protect the natural resources of the United Republic, the property of the state authority, all property collectively owned by the people, and also to respect another person’s property. Sub-article (2) obligates all persons by law to protect state authority's property and all property collectively owned by the people,, fight against all forms of waste and squander, and manage the national economy diligently as people in control of their nation's destiny. The Tanganyika Law Society is conscious of the public discourse around the ratification process and content of the the Intergovernmental Agreement (IGA) between the United Republic of Tanzania and the Emirate of Dubai concerning Economic and Social Partnership for the Development and Improving Performance of Sea and Lake Ports in Tanzania. Given the agreement's characteristics, possible impact, urgency, and sensitivity, on 7th June 2023, the TLS Governing Council assembled a team of specialists to examine the IGA, which at the time was still pending before the Tanzanian Parliament for ratification. The IGA was ratified by the Parliament of the United Republic of Tanzania on 10th June 2023. Since then, the Tanzanian Government, Media, Civil Society, Faith-based organizations, Private Sector, and various other stakeholders have voiced their opinions on the IGA, leading to conflicting conclusions and general lack of consensus. When the TLS Governing Council nominated this team of experts, they were tasked with the following specific objectives: 1. To dissect the proposed intergovernmental agreement between the United Republic of Tanzania and the Emirate of Dubai concerning economic and social partnership for development and improving the performance of sea and lake ports in Tanzania, dated October 2022. 2. To seek advice from relevant individuals who might provide additional insight to enhance the analysis, findings, and suggestions. 3. To conduct a comparative study on similar inter-governmental agreements in other jurisdictions, specifically those involving the Emirate of Dubai. 4. To submit a comprehensive analysis report with suggestions to the TLS Governing Council by 12th June 2023. On 12th June 2023, the team of experts delivered their report to the Governing Council as per their mandate. The report was discussed and contemplated by the Governing Council, and it is now intending to issue this statement.



Attached document





View attachment 2669695
 
Back
Top Bottom