New administration under Samia Suluhu gives hope after 5 years of hopelessness

Kama mfano wa Ghana ulivyoonyesha mikopo haiendi kuongeza uzalishaji bali kulainisha maisha kama huduma za elimu, afya, barabara n.k
 
Elimu kivuno chake ni makabrasha na hakuna ajira ya kuzalisha. Mhitimu yuko mtaani anasaga lami huku akihimizwa ajiajiri na hata ardhi aliyorithi kwa baba yake anaporwa ili amilikishwe mwekezaji ambaye sheria inamlinda asilipe kodi ya maana
 
Hivyo, hata tuwekeze vipi kwenye madarasa, nyumba za waalimu na maabara au hata ofisi za waalimu kamwe hatutarudisha mikopo ya kugharimia elimu kutokana na mfumo tulionao hauna uhusiano wowote kati ya elimu na uzalishaji
 
Afya simulizi ni ileile. Mahospitali kibao lakini afya za raia tangia lini zikalipa madeni ya kuboresha afya zao kama 70%+ hawana ajira?

Where is the lost money from the underemployed and unemployed if they are sickbed or even dead?

Hakuna hasara tunapata kama asiye na ajira hana afya nzuri hata akifa tuko vizuri tu😃 😀 😄 😁 🤣 😂 😃 😀
 
Barabara zinazalisha lakini hiyo hela inakwenda kujenga na kukarabati miundombinu nchi nzima na kuruzuku ufisadi wake pia. Hatuna ziada hapo ya kulipa madeni.

It is just hand to mouth, no surplus to pay up the debts, so to speak.
 
Tunajiamini kwenye hili ya kuwa mnikulu hawezi kuzijibu hoja zetu ya kuwa hakuna faida ya kukopa ili utoe huduma za jamii kama huduma hizo hazilipi madeni husika.

Na hili ndilo linaelezea kiundani mbona hatukomi kukopa tunabakia kuendelea kuombaomba tu kama tumepagawa vile 😢 😑 😫 ♥️ 💔 😳 😢

 
Tatizo kwa CCM ni kuwa sheria za kuwavutia wawekezaji zina uhusiano wa moja kwa moja na wao kubaki madarakani
 
Rushwa wanazolipwa na wawekezaji mbali ya kuwanufaisha wao binafsi bali pia hutumika kununua uchaguzi
 
Unatengeneza umasikini halafu unaupooza kwa kununua kadi za Chadema kwa elfu 20-25 tu badala ya kuja na sera za kuutokomeza umasikini
 
Mwendazake alipoona mbunge wa CCM kajiuzulu ubunge na alikuwa waziri wa zamani na kachomokea upinzani akajibu mapigo kwa kuwanunua madiwani na wabunge wa Chadema
 
Wa CCM kwenda Chadema alikuwa anakerwa na misimamo ya chama chake
 
Kuhama CCM na kwenda Chadema kulitokana na ndoto za urais kuzimwa
 
Hata basi alinunua na kulipaka rangi za kutukumbusha safari yake ya kwenda Ikulu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…