#COVID19 New World Order: My COVID-19 Passport

#COVID19 New World Order: My COVID-19 Passport

Nyani Ngabu

Platinum Member
Joined
May 15, 2006
Posts
94,296
Reaction score
122,540
AF4A9F1E-A438-402B-80E1-0CA6F248074F.jpeg


Happy Monday!

Popote ulipo mdau, kama una fursa ya kupata chanjo ya Corona, fanya hima uipate.

Kwa siku zijazo, itakurahisishia sana mambo mengi, ikiwemo safari za kimataifa.

Mimi nimechanjwa licha ya kwamba si mgonjwa.

Sikupatwa na mzio wowote ule kutokana na chanjo hiyo zaidi ya bega kuuma tu kidogo kwa siku kama mbili hivi.

Ukishadungwa, kwa pande hizi nilipo, wanakupa hako ka kadi kama uthibitisho wa kuchanjwa. Halafu ni bure kabisa!!

Chanjweni ili msije kupata usumbufu hapo baadaye.

Shime!
 
Hata Tz itakuja na mwenye kutaka atachanjwa, wasafiri wengi mno watachanjwa
 
EU na UK wameshasema kwamba wageni ili kuingia katika nchi zao ni lazima wawe na proof ya kupata chanjo ya COVID, sijui kama utaratibu huu umeshaanza rasmi au la, nadhani UAE nao ambao wanapata watalii wengi kwa mwaka nao wako mbioni kuweka taratibu hii. Wachina wametuletea balaa kubwa duniani halafu hadi hii leo bado wanaficha walichokifanya hadi kuibuka na COVID-19.
 
View attachment 1788516

Happy Monday!

Popote ulipo mdau, kama una fursa ya kupata chanjo ya Corona, fanya hima uipate.

Kwa siku zijazo, itakurahisishia sana mambo mengi, ikiwemo safari za kimataifa.

Mimi nimechanjwa licha ya kwamba si mgonjwa.

Sikupatwa na mzio wowote ule kutokana na chanjo hiyo zaidi ya bega kuuma tu kidogo kwa siku kama mbili hivi.

Ukishadungwa, kwa pande hizi nilipo, wanakupa hako ka kadi kama uthibitisho wa kuchanjwa. Halafu ni bure kabisa!!

Chanjweni ili msije kupata usumbufu hapo baadaye.

Shime!
kuuliza si ujinga. Hiyo chanjo ina expiry date baada ya kudungwa? ama hiyo expiry date ni ya dawa yenyewe hapo inayoonekana?
 
kuuliza si ujinga. Hiyo chanjo ina expiry date baada ya kudungwa? ama hiyo expiry date ni ya dawa yenyewe hapo inayoonekana?
Kwa kweli sijui hiyo exp. date ni ya nini.

Nahisi itakuwa ni ya dawa, endapo labda utakuwa umemiss second dose na hivyo kulazimika kuanza upya kuchanjwa, kwa zile chanjo zenye sindano mbili.

Huo ni usadiki wangu tu…sina hakika.
 
Back
Top Bottom