NEWCASTLE vs FULHAM: Somo la sheria linaendelea

Bila bila

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2016
Posts
22,168
Reaction score
39,118
Mpaka ninavyoandika kuna Mechi Kati ya Newcastle United na Fulham ikiwa ni dakika ya 77. Dakika ya 74 Fulham walipata penati baada ya VAR kuonyesha mchezaji wa Fulham alikwatuliwa akiwa ndani ya Penalt box. Fulham wakapewa penati Yao.

Wakati Mitrovic anapiga Ile penati kwa mguu wa kulia mpira ukamgonga mguu wa kushoto na kumpoteza kipa ukaingia wavuni.

Nasema somo linaendelea Kwa sababu baada ya goli la Man U laililokubaliwa Jana, Leo refa kakataa goli Hilo la Fulham na kuwapa Newcastle free kick kwa maelezo kuwa Ile ni double kick.

Kwangu shule ya sheria na kanuni za soka inaendelea bila ada.

Karibuni Wajuzi.
 
Sasa tufanyaje kuna msimu nadhani ni 20/21 uto walipgwa goli la mbali refa akaweka kona nadhani nipatie tafsiri ya hii kona
 
Hiyo iliisha jitokeza kipindi cha nyuma. Mara chache sana kutokea. Kama wewe ndio umeanza ushabiki hivi karibuni basi karibu.
 
Nimeanza kushabikia soka 1982, nimeangalia Kombe la Dunia runingani 1990.
Ukipata nafasi zitafute Sheria 17 za soka (laws of the game) uzisome maandishi yake. Utapata uelewa mpana sana.

Hutasubiria hata hawa wachambuzi wa bongo na wakati mwingine hata wa mbele hutasubiria maoni yao.

Kuna scenario zipo kwenye Sheria ambazo ni nadra sana kutokea ila wameshazieleza kuwa ikiwa itatokea maamuzi yake ni yapi.

Mf mtu akirusha mpira moja kwa moja ukaingia kwenye goli la wapinzani bila kuguswa na mtu unakuwa goal kick(sio goli)

Mf mtu akirusha mpira kuelekea golini kwake ukaingia bila kuguswa unakuwa corner wapinzani waje kupiga. Sio goli

Haya matukio ni adimu ila Sheria imeshaweka wazi bila kusubiri wachambuzi
 
Sheria hii ipo, penalty inatakiwa upige moja kwa moja
Sio kweli, ulichosema sio sahihi

Ni kwamba anaepiga penati, anatakiwa apige mpira mara moja kuelekea golini/nyavuni au kumpasia mwenzake. Lakini sio kujipasia mwenyewe au dribling au kukokota.

Alichokifanya huyo jamaa wa Fulham ni kuugusa mwenyewe mara mbili (mguu wa kulia na kushoto) kabla ya kuguswa na kipa au mchezaji mwenzake au mwingine
 
Labda hukunielewa au wewe sio mpenzi wa kuangalia mpira, tukio kama hilo lishatokea zaidi ya mara moja,kama dembele ishamtokea pia,ulichosema wewe ndio nimesema mimi na ipo hivyo siku zote,mpira ukikugusa sio goal
 
Labda hukunielewa au wewe sio mpenzi wa kuangalia mpira, tukio kama hilo lishatokea zaidi ya mara moja,kama dembele ishamtokea pia,ulichosema wewe ndio nimesema mimi na ipo hivyo siku zote,mpira ukikugusa sio goal
Sawa mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…